O-LEVEL ( Mambo Yakaanza Kubadilika)
Baada ya kupangiwa kibasila high school hapo Temeke sikufurahi kabisa yani niliona wamenionea sana mimi nilihitaji nipelekwe shule yeyote ya boarding mkoani na kwa bahati mbaya kilikuwa kipindi kibaya maishani mwangu baba yetu alipata mitihani mikubwa sana maisha yakawa magumu mno tulikuwa tukiishi nyumba ya kupanga mzee akashindwa kulipa kodi alikuwa ana boma lake kibaha huko akauza kwa bei ya hasara then akaenda kununua shamba mkuranga, alipofika kule alifikia kwa jamaa yake mmoja akampa hifadhi kwenye moja ya nyumba zake za udongo na hela alokuwa nayo mzee asingeweza kumudu kujenga nyumba kama nyumba ilibidi na yeye ajenge nyumba ya miti tena mdogo mdogo maana hela yenyewe naona ilishaanza kuisha. kule shamba alienda na mama na watoto kama wawili maana sehemu ya kukaa kulikua hakuna, Sisi wengine tulitawanywa kwa ndugu na jamaa mjini, Baada ya muda kidogo mama yetu alianza kuumwa sana ( Figo zilifeli, akapofuka macho, alikonda sana kbla alikuwa mnene kiasi ) mzee akazidi kuchanganyikiwa na kuacha kutufikiria sana wanae.
Picha linaanza mimi nlipelekwa kwa jamaa yake mmoja hapo nyumbani kwake alikua ana garage yake vijana wake wanafanya kazi jamaa alichojali ni hiyo garage
Jamaa alikuwa hanijali kabisa nauli sipewi kula kwa shida shule nikawa siendi mara kwa mara. Roho ilikuwa inaniuma sana nikawa sina la kufanya, midterm ikapita sikufanya mtihani wa kumwambia sina mzee yeye hata kutokea pale hatokei. Nilikaa pale mpaka mwezi kama wa tisahivi form 1 ndo nikaondoka pale nlitoroka nikajipeleka kwa mama mmoja alikuwa jirani yetu zamani, Kukaa pale na kwenyewe ilikuwa balaaa unafanya kazi zote ndani wewe, sipewi nauli ya shule, kula kwa tabu, kusingiziwa wizi mpaka majirani ndo wakawa wananisaidia saidia kidogo tu nikaona hapa mimi shule basi nkamaliza form one perfomance ilikuwa ni mbovu ila nlikuwa mtu wa kati kati yaani nlikuwa sisomi kabisa, darasani nlikuwa ndo hvo siingi lakini nlikuwa nkifanya mitihani yeyote nilipata 30- 60 najibia uelewa wangu binafsi tu, nkaingia form two nkahama hayo maeneo nkawa nakaa na mabraza tu wa mitaani nikajitahidi ili nianze vizuri kidogo shuleila bado changamoto zilikuwa nyingi hasa kukosa nauli ya shule uniforms na baadhi ya ada za shule nyingine, So nkaendelea kibishi tu na Automatically nkaanza kama kuichukia shule utoro ukaongezeka sana kuna wenzangu nlienda nao pale kibasila walikuwa among Geniouses wa pale kibasila mpaka wakawa wananishangaa jamaa yetu kakutwa na nini?
Form two mwendo huo huo mbovu mpaka mwezi wa nane mzee alikua ana kijana wake mmoja hivi anakaa vingunguti (brother Hoki) god bless you. Japo jamaa alikuwa maskini sana lakini alijitahidi sana kunisaidia, alikuwa anafanya kazi kwenye kiwanda cha mikate akilipwa sh 5000 - 6000 per day,ila alikiwa akinipa nauli na hela za misosi japo ni ndogo sana ila alinisaidia kwa miezi ile mitatu tu nilipiga msuli wa kufa mtu necta form 2 nikajitahidi kiasi maana pale wanaojua niwengi ila nlipata wastani wa 68 out of 100 masomo 11. Kuingia form three nikapangiwa science nikapania sana na nikaanza vizuri nlikua nakaa na bro wangu mmoja hivi alikua anajitahd kunisapot nikawa nasoma sana na napiga tuition mchikichini, mwanzo mtihani wa kwanza kufanya ulikuwa midterm form 3 nakumbuka mathematics ulikuwa mgumu sana ule mtihani nikapiga banda, Phys pia Banda , baada ya hapo mambo yakaanza kubadilika pia nikaanza utoro kias hela ya kwenda mchikichini sina, Tukaenda mwezi wa sita pia nikajitahidi kiasi tu ila baada ya pale majanga yakaanza tena nlienda kukaa na brather mwengine yeye alikuwa hana maisha kabisa kwa hiyo nikaanza kuunga unga tena, mwisho wa siku nikaichukia kabisa shule masimango ya wanafunzi wenzangu na walimu yakanishinda nkahamia kwenye magame ps nkawa master ps mitaani, nikaanza kuwa kama watoto wa mitaani jioni naenda kwenye vigodoro. Nakumbuka mara ya mwisho form 3 kwenda shule ilikuwa mwezi wa 8, baada ya hapo si kwenda tena shule mpaka walimu walipompigia mama yangu mdogo kuwa wananiulizia nipo wapi washamaliza kusajili wanafunzi kwa ajili ya necta, Ndo na wao wanashtuka kuwa nlikua siendi shule maana hapo kati nlikuwa nkipiga simu nawaambia naenda shule kama wanapata hela japo kwa mwezi mara moja wananitumia, Wakafunga safari kutoka mkoani mpaka dar, kunipeleka shule.
Itaendelea