...UPDATES: Mhe.Mbowe anadokeza kwamba CHADEMA inamjenga kila raia wa taifa hili kujiamini na kutetea haki bila kuogopa chochote."Ndiyo maana kipindi kile Spika wa bunge Makinda alijaribu kutumia ubabe kuzima hoja zetu lakini walishindwa.Baadaye Kikwete alituita ikulu tukaenda Mimi Mbowe,Mhe.Mbatia na Prof.Lipumba.Kikwete alituomba tusitishe maandamano ya umoja wa vyama vya upinzani nchi nzima nasi tukasimama tukamwambia sharti madudu yaliyopitishwa na wabunge wa CCM kuhusu bunge la katiba yatupiliwe mbali na turudi tena bungeni kujadili...Rais Kikwete kwa kuogopa nguvu ya umma na ukweli uliojulikana wazi alikubaliana na msimamo wetu na matunda yake ni hii (ameonyesha rasimu ya katiba mpya)" Wananchi wanashangilia. Mhe.Mbowe anaongeza kwamba CCM walifikia hatua ya kumtuhumu Mhe.Warioba eti anachukua maoni ya CHADEMA tu alipopendekeza serikali tatu,je hayakuwa maoni yenu wananchi? (Watu wanamshangilia Mhe.Mbowe huku wengine wakisema CCM ilikufa na Nyerere).