Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 10,295
- 17,373
Je kuna uhusiano wowote wa hilo Tangazo na M4C au Movement for Change ya CHADEMA wanayoitangaza Tanzania nzima? Ninachomaanisha ni kwamba hao watu kwenye hicho kijiji wanaelewa hilo Tangazo linamaanisha nini? (Hiyo Picha siyo kijiji cha Tanzania)
Na kama hawaelewi Je aliyeliweka alikuwa anamlenga nani? Ni kwa nini ameliweka? Kwa nini asiandike kwa Lugha ambayo hao wataelewa?
Nimeuliza hivyo kwa sababu Bibi yangu Kijijini aliniuliza hivi hiyo M4C ndiyo nini, nikashindwa kumuelezea, nikabaki kujiuliza kama Bibi yangu yuko peke yake Tanzania, lkn alivyoona 'Nguvu Mpya Ari mpya' alielewa na hata kuanza kuhoji, hiyo nguvu mpya yenyewe wanayoiongelea iko wapi hawa CCM?