Akilihuru
JF-Expert Member
- May 20, 2022
- 1,444
- 2,833
Za asubuhi wakubwa, weekend inaendeleaje?
Leo nawaletea muendelezo wa kile kinachojiri huko Congo katika oparation ya jeshi la kanda yetu hii ya EAC. Oparation hii mahsusi imebuniwa kwa lengo la kuwapokonya silaha waasi wote waliopo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ila walengwa haswa wa oparation hii ni wale vijana walioshiba mafunzo ya kijeshi, wenye weledi wa kupambana na adui mchana au usiku, angani au ardhini, vijana hawa sio wengine bali ni lile kundi imara la waasi wa M23.
Kabla oparation hiyo haijapangwa, viongozi wa nchi zetu za maziwa makuu walitoa kwanza siku maalum na saa kwa makundi hayo kusalimisha silaha zao wenyewe, kuachia maeneo yao (walioyateka) na kusubiri michakato mingine ya kisheria itakayofanywa kwa waasi hao.
Baada ya kumaliza kutoa tamko hilo la kusalimisha silaha, ndipo viongozi wa nchi hizo wakatuma majeshi yao Congo kwa ajili ya kwenda kuwawajibisha waasi wote watakaokaidi kutii agizo hilo la serikali na nchi za maziwa makuu.
M23 ambalo ndio kundi imara na hatari kwa majeshi yaliokwenda huko, lilikaidi maagizo hayo na kusubiri kuona ni nini kitachofanywa na vikosi hivyo vilivyodai kwamba vinakwenda kusafisha uasi katika nchi hiyo ya pili kwa ukubwa barani Afrika.
Juzi M23 imefanya oparation zake inazofanyaga kila siku na kupelekea watu 50 kufariki dunia. Hii ni salam ya dhahiri kwa vikosi hivyo vya Burundi na Kenya vilivyopelekwa huko eti kujaribu kuwapokonya silaha 'wanajeshi' wenzao, kama vile mtu anapojaribu kumpokonya mtoto wake pipi.
Kifupi ishaonesha kuwa M23 ni maji marefu ndio maana kdf na fdnb wanashindwa kuthubutu kuingiza miguu katika maji yao (maeneo yao) wasije wakazama mazima ikawa aibu kwao na kwa nchi zao.
Ushauri wangu ni kuitaka serikali mpya ya Congo iangalie namna bora ya kuongea na kundi hili kwa mara ya mwisho kwa lengo la kuleta amani maeneo hayo. Ikishindikana ndio nguvu kubwa na ya pamoja itumike. Ila kuyategemea majeshi haya ya Burundi na Kenya kuleta amani ni kupoteza muda bure, maana hawana uwezo hata waku deal na mayi mayi achilia mbali vijana hatari wa M23.
Leo nawaletea muendelezo wa kile kinachojiri huko Congo katika oparation ya jeshi la kanda yetu hii ya EAC. Oparation hii mahsusi imebuniwa kwa lengo la kuwapokonya silaha waasi wote waliopo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ila walengwa haswa wa oparation hii ni wale vijana walioshiba mafunzo ya kijeshi, wenye weledi wa kupambana na adui mchana au usiku, angani au ardhini, vijana hawa sio wengine bali ni lile kundi imara la waasi wa M23.
Kabla oparation hiyo haijapangwa, viongozi wa nchi zetu za maziwa makuu walitoa kwanza siku maalum na saa kwa makundi hayo kusalimisha silaha zao wenyewe, kuachia maeneo yao (walioyateka) na kusubiri michakato mingine ya kisheria itakayofanywa kwa waasi hao.
Baada ya kumaliza kutoa tamko hilo la kusalimisha silaha, ndipo viongozi wa nchi hizo wakatuma majeshi yao Congo kwa ajili ya kwenda kuwawajibisha waasi wote watakaokaidi kutii agizo hilo la serikali na nchi za maziwa makuu.
M23 ambalo ndio kundi imara na hatari kwa majeshi yaliokwenda huko, lilikaidi maagizo hayo na kusubiri kuona ni nini kitachofanywa na vikosi hivyo vilivyodai kwamba vinakwenda kusafisha uasi katika nchi hiyo ya pili kwa ukubwa barani Afrika.
Juzi M23 imefanya oparation zake inazofanyaga kila siku na kupelekea watu 50 kufariki dunia. Hii ni salam ya dhahiri kwa vikosi hivyo vya Burundi na Kenya vilivyopelekwa huko eti kujaribu kuwapokonya silaha 'wanajeshi' wenzao, kama vile mtu anapojaribu kumpokonya mtoto wake pipi.
Kifupi ishaonesha kuwa M23 ni maji marefu ndio maana kdf na fdnb wanashindwa kuthubutu kuingiza miguu katika maji yao (maeneo yao) wasije wakazama mazima ikawa aibu kwao na kwa nchi zao.
Ushauri wangu ni kuitaka serikali mpya ya Congo iangalie namna bora ya kuongea na kundi hili kwa mara ya mwisho kwa lengo la kuleta amani maeneo hayo. Ikishindikana ndio nguvu kubwa na ya pamoja itumike. Ila kuyategemea majeshi haya ya Burundi na Kenya kuleta amani ni kupoteza muda bure, maana hawana uwezo hata waku deal na mayi mayi achilia mbali vijana hatari wa M23.