LWAITAMA aunguruma juu ya WARAKA wa LEMA kwa Rais Jk!


Mimi naamini kwa dhati kabisa kabisa kwamba sasa kiama kinainyemelea nji hii kwa sababu kufuatia waraka wa GJL kwa JK na hayo aliyoyaainisha katika waraka huo umesababisha taharuki miongoni mwa wanachama wa CDM hususani vijana ambao wameonyesha kukunwa kwa kiasi kikubwa na misimamo ya GJL; kwa hiyo basi endapo lolote baya litamtokea Lema hata la kawaida tu la kimungu mungu; itakuwa vigumu sana kwa vijana wengi kukubali au kuamini kwamba GJL amedhurika kawaida hivi hivi na kwa sababu hiyo ile njozi ya JK kwamba Arusha imerejea katika amani itapotea kabisa na moto huo kusambaa nji nzima. Wapenda amani wote tumuombe Mungu pande zote busara itumike ili amani ishamiri.
Wataalamu wansema hivi; UKITAKA AMANI PIGANIA HAKI, penye dhuluma amani haistawi hata kidogo, kama nadanganya fuatilieni yanayojiri Tahrir square Cairo ambapo licha ya Dikteta Hosni Mubarak kuhukumiwa kifungo cha maisha bado vijana wanaamini haki haikutendeka kwa hiyo Tahrir square imeanza kufurika upya kudai haki itendeke; and that is a recipe for chaos.
 
Nawashangaa sana wafuasi wa CDM! Kwa kweli wanajidanya sana kusema eti Lema anakubalika sana Arusha,watu wa Arusha kwa sasa hawamtaki kabisa LEMA wanamtaka Lema ni vijana wa vijiweni ambao ugumu wa maisha katika kipindi ambacho Lema alikuwa mbunge wa kuleta vurugu wao walikuwa hawauoni sijui kwa sababu hawana kazi za kufanya.Lakini kwa watu wote waliojiajili,wafanyakazi na wafanyabiashara kubwa na ndogo ndogo hawamtaki kabisa .Na mtaliamini hilo pindi uchaguzi mdogo ukiitishwa na Lema na CDM kushindwa vibaya sana.CCM wameliona hilo na wamejipanga hivyo wanaodhani Lema anakubalika Arusha wasubili kupatwa na mshtuko wa moyo. Wiki iliyopita nilikuwa Arusha na watu wengi sana wanaongelea furaha yao ya maisha kuanza kurudi kwani hata mikutano mikubwa kama ulioisha jumamosi ilikuwa ni ngumu kuletwa Arusha,Wageni walikuwa hawaendi Arusha walikuwa wanatua Nairobi na kuja Tz kutembelea mbuga zetu au kutua KIA na kupelekwa moja kwa mbugani bila kukaa Arusha kama ilivyozoeleka kutokana na vurugu za LEMA na CDM yake.Hivyo chadema wanajidanganya wafanye research waone ili wajipange.
 
Maoni, machambuzi, malumbano Hoja makini Na Hoja Zembe.. All in all I real fall'n luv with JF.. Hasahasa Jukwaa la watu makini mno .. SIASA..

Kila mwerevu, kila Mtu makini, awazaye hatma ya mambo, ustawi wa nchi au machafuko, asiyependa kuonewa kimabavu, Mtu ANAYEJIAMINI Na kuuheshim Utu wake, lazima aongelee SIASA..
 

Acha kuwatusi watu wewe kuna mtu amekuja kwako kukuomba msaada unaosema wanakaa vijiweni ambao hawana kazi? tumia akili kama wewe unakuja Arusha leo unapata tasimini ya Arusha kwa family yako kuhusu Lema na Arusha kwamba hawamtaki Lema wambie familly yako wajipange wakulete ushahidi upya kwamaana umeacha kuwasikiliza watu wenye Arusha ukasikiliza familly yako huna akili hakuna asiye mkubali Lema kwani huo mkutano umeleta faida gani Arusha zaidi faida kwa baba mwanaasha kuja kutafuta mademu shivazi akijifanya anafanya mazoezi achakufundisha watu ujinga
 

Weye waweza kuwa great tinker mukichwa
 
hakuna ujinga ulio ujinga mtupu!

Kila lisemalwa duniani ni hakika kwa kiasi fulani tu! Hali hiyo hulazimisha wajuvi wa mambo kutafuta kiasi kilichobakia. Na huu ndio mwanzo wa asili ya utafiti wowote. Hakuna habari yeyote ambayo unaweza kudai ni ya kijinga kwa 100% qani lazima kuna chembechembe za ukweli ndani yake na huo ni lazima ufanyiwe kazi kwa manufaa ya ngurumbili wote.

Wakati wote fikiri kwa upana na kina stahili. Uckubali kuwa na fikira zilizo ndani ya sanduku.

BAzazi ni Bazazi!
 
.


Wanasema ukibahatika kuongezewa salio la akili kwenye wazo Basi usibweteke sana, jaribu kuongezea Na salio la akili zako kabla ya kumwaga ukijuacho mbele ya raia wenzako..

Mkutano Wa Benki ya Africa ya MAENDELEO hufanyika kila baada ya miaka mitatu au mwaka mmoja Kwa ile ya uongozi..

PLACE, VENUE, COUNTRY hujulikana mwaka mmoja kabla ya mkutano husika. Rais wa AfDB Dr. Donald Kaberuka mchumi na raia wa Rwanda, yeye na timu yake makini makosa madogo ya kukurupuka huwa hawafanyi.. Wao hutafiti Na kuchagua sehemu muafaka wa kufanyia mikutano Yao Na kuwajulisha wajumbe, nchi marafiki na wahisani mwaka mmoja kabla ya mkutano..

Arusha inapendwa Na wageni wengi Kwa sababu ya Hali ya Hewa, uoto Wa asili Na hifadhi ya maliasili kubwa sana ya nchi yetu.. DSM Ni mji wenye Joto sana, vumbi sana, msongamano, harufu Kali kila kona ambazo wageni wengi kwao ni kero..

Suala la Lema Na vuguvugu la Arusha limekuwepo kitambo, Na si kiivyo Kama inavyosemwa kwamba AR kulikuwa Kama Ivory cost ya juzi, misri ya Jana au Lebanon.. Mji ulikuwA shwari tu Na pilika za kila siku ziliendelea isipokiwa nyakati mbili tatu za vuguvugu ambazo zilijitokeza tena kwenye maeneo machache sana ya mji pasipo kujeneralize AR yote..hata Kama hukumu ya Lema ingekuwa bado mkutano ulikuwepo pale pale

Kwa hiyo kusema Lema alikuwa tatizo ni Ujinga kabisa Na akili iliyorogwa mbaya.. Mtu mmoja hawezi kuzuia mkutano mkubwa that way .. Na vilevile mikutano AICC ni kila mchao.. Rais kumwingiza Lema ni kumpandisha chati sana sana Na yeye kujishushia hadhi Na mamlaka ya urais wake.. Hapo Kwa kweli RAIS ALIKURUPUKA KUROPOKA!!
 
Mkuu Yericko,

Nilidhani na wewe ni great thinker kumbe hamna kitu unapoteza muda wako kusikiliza ujinga wa Lema kweli Tanzania ni masikini si kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya wananchi wake kuwaamini wanasiasa wa hovyo.
Sasa wewe ndio mjinga zaidi! Tanzania ni masikini kwasababu ya wananchi wake kuendelea kukiamini Chama cha Magamba, Mafisadi na Majambazi wa rasilimali zake! This is one of the stupid comments I have ever seen in JF!
 
why tuna discuss watu badala ya matatizo yanalolikumba taifa hili?? hamjua chama ni zaidi ya mtu?? tuache haya mambo bibi yangu kule kijijini haitaji jina la mtu wala pesonality kwake chama ni nani atamsaidia apate mbolea na soko la mawazao yake.let us think bigger na tukikumbuka hakuna chama hata kimmoja duniani kilichowahi kushinda mpaka kushika dola kwa kutegemea wanachama wake tu,wote wanashinda kwa kula za "moderate voters" wapiga kura wasio washabiki wa mtu wala chama ila washabiki wa sera bora zitakazotatua matatizo yao ya sasa,tusipoteze muda na hizi personality zipo leo tu na ni kwa muda mfupi sana chama kiwe zaidi ya watu na tuache kukipa chama sura ya watu,kumbukeni leo NCCR Mageuzi iko wapi?? kosa lao ni mmoja tu hawakujenga chama walitegemea personality ya mtu mmoja Liatonga Mrema.
 

Weboroya, kila unapochangia kuhusu Lema lazima utaje suala la mimba ya Lowasa. Kumbe kusema yule ana mimba ya lowasa kunaweza kumdharilisha mwanamke kiasi hicho? Lowasa na mke na watoto, je ni ajabu akipata mtoto kwa mke mwingine. Kama ikiwa lema alisema yule mama kafanya mapenzi na mbwa,hapo una haki ya kumshambulia Lema,lakn kufanya mapenzi na lowasa, si dhani kama ni issue kiasi hicho
 
Mimi kwa mawazo yangu ningependa kumshauri Godbless Lema na waTz wengine muache kulalama kila wakti ni vizuri mutumie njia sahihi za kudai haki zenu ambazo zipo wazi kabisa na zimebainishwa katika sharie za nchi yenu. yaani kutumia mahakama.

Kumbukeni Mbona Mnyika alishinda, Mbona wenje alishinda, mbona makongoro alishinda. Kama mnakubaliana na hayo yote kwanini msikubali GodBless Lema kushindwa kwa kupitia mahakama hizo hizo.
namshauri Lema ka
ma atakuwa makini aachane kabisa na kuandika Waraka bali arudi tena mahakamani kudai haki yake.

wasikutie ujinga hao akina Exavel Lwaitamwa ( mimi ni college mate wangu ) ambao siku hizi wamekuwa wanasiasa na kusahau maadili ya taaluma zao za political science na kuona kuwa wasiokupenda kwani hata siku moja waraka hauwezi kutengua maamuzi ya mahakama. Kinachoweza kutengua ni mahakama za juu na haki hiyo ipo wazi kwako.
 
Hingi Jr;4002425]
''Nawashangaa sana wafuasi wa CDM! Kwa kweli wanajidanya sana kusema eti Lema anakubalika sana Arusha,watu wa Arusha kwa sasa hawamtaki kabisa LEMA wanamtaka Lema ni vijana wa vijiweni ambao ugumu wa maisha katika kipindi ambacho Lema alikuwa mbunge wa kuleta vurugu wao walikuwa hawauoni sijui kwa sababu hawana kazi za kufanya.Lakini kwa watu wote waliojiajili,wafanyakazi na wafanyabiashara kubwa na ndogo ndogo hawamtaki kabisa .Na mtaliamini hilo pindi uchaguzi mdogo ukiitishwa na Lema na CDM kushindwa vibaya sana.CCM wameliona hilo na wamejipanga hivyo wanaodhani Lema anakubalika Arusha wasubili kupatwa na mshtuko wa moyo. Wiki iliyopita nilikuwa Arusha na watu wengi sana wanaongelea furaha yao ya maisha kuanza kurudi kwani hata mikutano....''

Ndugu Hingi Jr, hata kama unaweza kuwa na kibarua ,hiyo haiwezi kuwa sababu ya kuwa na dharau dhidi ya vijana wa kijiweni.
Elewa tu kuwa haya ni matokeo ya sera na mipango ya CCM.
Elewa pia kuwa thamani ya kura ya kijana wa kijiweni na ya mwenyekiti wa CCM mkoa haitofautiani!
Wote wanapiga kura moja tu!
Au mwenyekiti anapiga kura tano?
Una idadi kamili ya vijana wa kijiweni?
Unaweza kueleza umefikia hitimisho lako kwa kufanya utafiti?
Kama hilo huwezi umewahi kutembelea Arusha?unaifahamu vuzuri?
Inaelekea unaisoma magazetini!
Hakika, nakufahamisha kuwa laiti ungekuwa umefanya hayo mawili hapo juu usingekuwa mwepesi kutamka uliyotamka.
Tunaheshimu mawazo yako ingawa hatuyakubali.
 
Kwa mfumo wa intelijensia ya nchi yetu ni kuwa kila walipo watu kumi mmoja ni nyoka!

Nakubaliana na wewe lakini labda tuseme kwa kila watu kumi kuna manyoka wa vikundi tofauti... Maana kuna manyoka wa CCM, Manyoka wa Mafisadi, Manyoka wa kutetea Maslahi ya walowezi wanaolitafuna nchi hii....
 

kaul huweza kusaidia kumjua mtu,,,,na busara zake,,,,,kwa wazo la uislam,,,,nshakuelewa,,,,,je kama angekua muislam ila wa CHADEMA ungetafuta another option????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…