LWAITAMA aunguruma juu ya WARAKA wa LEMA kwa Rais Jk!

Hahaahaaa ebwanaeeee! Nashukuru kwa kumjibu maana kanitusi kwelikweli!

Daah! Sasa mkuu na wewe unafurahia Ngongo alivyojibiwa kutokana na kukutukana wewe wakati amekuomba msamaha ukamjibu ”poa kamanda pamoja” , sidhani kama umefanya ustaarabu ilitakiwa ukae kimya tu yaishe, na si kushabikia anapotukanwa na yeye!

Mbumbumbu Intelligent.
 
Mkuu PapokwaaPapo,

Ni kweli level aliyofikia Lema siwezi kuifkia hata siku moja.

[1] Sina mpango wa kuombea wafu wafufuke.

[2] Sina mpango wa kuandamana kwasababu za kijinga.

[3] Sina mpango wa kususia dhamana.

[4] Sina mpango wa kudharau akina Mama wajawazito.

Siwezi kuacha kukemea uovu kwasababu uovo wenyewe umetendwa zamani kama umefikia kiwango cha kutushawishi tuache kumsakama Lema kwasababu uovu aliotenda aliufanya zamani basi tusiwalaumu A Chenge kwasababu alitumia vibaya madaraka ya AG zamani.

Tusimlaumu Lowassa kwakuwa mkataba mbovu wa RICHMOND ni wa zamani,tusimlaumu B Mkapa kwakuwa alijiuzia Kiwira zamani .........


Ngongo acha chuki binafsi na Lema, Level aliyonayo Lema kwa sasa may be mpaka unaingia kaburini huwezi ifikia.
Acha kuwa na chuki za wakati uliopita ndugu.
Mungu akuangazie uweze ona nyota ya alfajiri
 
Tanzania namzaha wa Ajira kwa vijana



Nashukuru ndugu WANA JAMII FORUM kunipanafasi ili niweze kutoa maoni yangukuhusu tatizo la ajira ambalo limekuwa ni donda sugu katika jamii (mataifa)yanayoendelea ikiwemo Tanzania. Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kazi duniani 2011 inaonyesha kuwa nafasi za kazi milioni800,000 zinahitajika duniani ili kupunguza tatizo la ajira na ripoti ilitaadhalisha kuwa tatizo hili lisiposhughulikiwa litachochea migogorombalimbali duiniani. Lakini tukirudihapa kwetu Tanzania tatizo hili nikubwa hususani kwa vijana wenyemiaka 15 mpaka 35. Kundi hili ni nguvukazi kubwa katika mstakabali wa taifa hili. Pamoja na kundi hili kuwa nguvukazi muhimu bado hakuna jitihada mahususi za kutumia rasirimali hii nyeti.

Nimeandika makala hii kutokana nakugundua kuwa serikali haina mpango na nia madhubuti kutokana na taarifailiyotolewa hivi karibuni na waziri wa kazi na ajira. Waziri halikanusha kuwa tatizo la ajira sio kubwa kama watu wanavyolizungumzia. Hii ilitokana namatamshi yaliyotolewa na mbunge wa Monduli Edward Ngoyai Lowasa kuwa tatizo la ajira ni bomu linalosubiri kulipuka.Waziri akitoa takwimu alionyesha kuwa tatizo la ajira limepungua na kuwa tatizo si kubwa kama watuwanavyolizungumzia. Lakini taarifa ya waziri ilishindwa kubainisha ni vijanawangapi ambao huingia kwenye soko la ajira na ni wangapi huajiriwa katika sekta rasimi. Ni vigumu tatizo hili ambalonitishio kwa mstakabali wa taifa kushughulikiwa kama viongozi wenye dhamanawana mtizamo wa aina hii. Mtizamo huu wa waziri wa kazi na ajira hautofautianina kauli iliyotolewa na waziri anayehusika na utumishi wa umma Hawa Gasia ambaye katika bunge lilopita alitaja kuwavijana wengi hawaajiriwi kwa kuwa hawajui kuandika barua za maombi ya kazi.Swala la msingi hapa ni je, mbona hakuleta taarifa ya nafasi ngapi za ajiraambazo zimekosa watu kutokana na vijanakushindwa kuandika barua za maombi. Nilitarajia atutajie kinagaubaga kuna nafasi ngapi ambazo zikowazi ili ifahamike.

Sambamba na hilo viongozi wengi wamekuwa wakiwalaumu vijanakuwa sio wabunifu na hawana utaalaamu kulingana na fursa zilizopo lakini, kwahao waliokaa miaka nenda rudi utaalamu wao mbona haujajidhihirisha katikamaisha ya watanzania. Wengi wao ni wale waliopitisha mifumo ambayo imeletakilema katika uchumi wa taifa. Mwandishi mmoja wa China Mao Tse Tung kwenye kitabu chake cha (Four essays in Philosopy1966) , anaonyesha kuwa ukitaka kufahamu ukweli na utatuzi wa tatizo, lazimauwe umefanya jaribio ikiwa ina maanakwamba ukitaka kufahamu uzuri au ubaya wa kitu lazima ujue faida na hasarayake. Kwa hiyo hawa wazee hawajapitia mfumo wa maisha magumu ya ajira kwani waokabla hawajamaliza masomo tayari walikuwa wamekwisha pangiwa vituo vya kazi. Navijana wakizazi hiki wamepitia mfumo huu mgumu wa ajira hivyo wanajua tatizoliko wapi tatizo ni kupewa nafasi au kuwa na mhimili ambao utawezesha sauti namawazo yao kusikika.
Watu wengi wamekuwa wakipata kazikwa kujuana na wengi wanao pata ni wale ambao wazazi wao wanamajina. Kwa kuwavijana hawa wanaopewa kazi kwa kujuana hawajaonja ugumu na changamoto za kukosaajira basi hakuna mawazo tofati katika ufumbuzi wa tatizo hili. Kama kuna anayebisha naomba kafanye utafitialafu atupe ripoti wafanyakazi wa BOT kati yao ni wangapi wanatoka familia hoehae. Uliza maafisa waliomalizamafunzo ya maafisa ya jeshi la polisi(sasa wako vituoni) huliza walipataje,nenda mashirika ya umma kama NSSF, Bodi ya mikopo, NHIF ,SSRA na LAPF. Watukabla nafasi hazijatangazwa wanaitwa kujitolea huku wakipewa posho. Nafasizikitangazwa wao ndio kipau mbele. Tukiachana na dhana potofu kuwa vijanahawapendi kujitolea si kweli kwani ni vijana wengi wanatamani kujitolea kwenyetaasisi mbali mbali ili kupata uzoefu lakini hiyo nafasi kuipata si rahisi kamainavyozungumzwa na watu wanaopotosha(hasa viongozi).

Ni kweli fursa za ajira ni chachekwamba watu wote hawawezi kuajiriwa na serikali lakini ni lazima hata walewanaonyesha moyo wa kutaka kujiajiri waungwe mkono baada ya kuchukulia mambokisiasa. Kwa mfano kwenye mpango wa kilimo kwanza nguzo 8.1.8 inaonyesha kuwaserikali itawawezesha vijana wanaohitimu vyuo mbalimbali wanaotaka kujiajirikwenye kilimo pamoja na kuwapa ardhi. Mpango huo umeanza utekelezaji kuanzia mwaka2009, inabidi serikali itupe ripoti imewawezesha vijana wangapi wahitimu. Nivijana wengi wenye mawazo mazuri ya kupanua fursa za ajira lakini hawana nafasiyakupeleka mawazo yao.

Ardhi na mtaji mpaka sasa ni changamoto kubwa kwavijana. Kwa kijana aliyehitimu ni vigumu sana kukidhi masharti ya mikopo.
Kuanzishwa kwa wakala wa ajira(TAESA) nathubutu kusema kwamba watu waliowekwa wameshindwa kufikia malengo ya kuanzishwa kitengo hiki ambacho kikochini ya wizara ya kazi na ajira. Hii inatokana na kuwepo watu ambao wamebebwa, si wabunifu na mwisho wa siku hawajifanyii tathmini kwa kile wanachokifanya.Taasisi kama hii inahitaji vijana ambao wameonja joto la tatizo la ajira hivyowamefikiria sana na kuja na mawazo madhubuti jinsi ya kumaliza tatizo la ajirana si kupunguza kama mipango mingi ya serikali inavyoonyesha kwa mfano MKKUTA,dira ya maendeleo 2025 ambayo nadhani viongozi wengi hawajuhi inalenga nini aukama wanajua basi wanawaadaa wananchi kwa kutoa ripoti zinazoonyesha kuwaumasikini unapungua huku ugumu wa maishaukiongezeka mara dufu.

Kwa mujibu wa ripoti ya maendeleo ya haki za binadamu Tanzania ya2007, inaonyesha kati ya wahitimu 700,000 kila mwaka wanaoajiriwa kwenye sektarasimi ni 40,000 na kundi hili ni vijana ambao ni umri wa miaka 15 mpaka 35.Kundi hili linalobaki ni kubwa hivyo hatuhitaji siasa bali watu makini wenyeuwezo wakuwashirikisha vijana ili kutafuta ufumbuzi kuliko kurushiana mpira. Pia ripoti ya wizara ya fedha nauchumi ya mwaka 2010 kuhusu tathmini ya utekelezaji wa MKUKUTA inaonyesha kuongezeka kwa idadi ya wahitimu.Kuongezeka huko ripoti inaonyesha kuwani kiashiria moja wapo cha kufikiamaisha bora katika jamii. Lakini nivigumu kuwa na maisha bora kwa kuwa na cheti kizuri kilichowekwa urembo naufaulu mzuri. Maisha bora na elimu bora ni pale inapokuwezesha kukithi mahitajiyako ya kila siku. Pamoja na ongezeko hilo la wahitimu maisha yanazidi kuwa magumu kuliko siku za nyuma.Kwa ujumla naona hakuna haja yakujisifia kuwa elimu imeboreshwa kwani haijawawezesha vijana kutatua changamotokatika jamii. Kinachongezeka ni idadi tu. Ikumbukwe mwalimu Nyerere wakatianatunukiwa shaada ya heshima na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania tarehe 5 machi1998, alisisitiza kuwa elimu bora ni ile inayoendana na mazingira ikiwa inamaana kwamba kuwawezesha vijana wetu kujitegemea kwa kutumia rasirimalizilizopo. Aliendelea kusema kuwa elimu bora lazima isimfanye mtu kuwa mtumwabali imfanye kuwa huru. Lakini hata waandaaji wa mitaala yetu naona wanaandaamitaala ya kumfanya mtu akaajiriwe na si kujiajiri. Kutokana na dhana hii imewafanya watu wengi kuwa watumwa wa kutafuta kazi za kuajiriwa kwa kuwa hatawafundishaji wenyewe hutoa mfano wa msomi aliyefanikiwa kwa kuangalia ameajiriwa na taasisi gani na anapatashilingi ngapi . Kwa hiyo hata vijana wanaohitimu wanakuwa na fikra zilezile.
Nini kifanyike?
Kwanza mfumo wa elimukubadirishwa kutokana na kwamba umepigiwa kelele kwa muda mrefu pasipo majibu.Tanzania tuna ardhi kubwa ambayo tukiweka mipango madhubuti, vijanawatawezeshwa kupata mafunzo rafiki na hatimaye kuleta faida kwa taifa kama vileuwepo wa chakula cha kutosha, uwepo wa ajira, kuondoa upotevu wa pesa zakulipia mafunzo yasiyo na tija kwa wananchi. Ikumbuke kwamba elimu ni uwekezaji, tukiwekezakwenye elimu rafiki na mazingira itatumia muda mfupi na matunda yake kwa mwekezaji (mzazi na serkali) yataonekanakuliko kujisifia kwa elimu ya sasa ambayo baada ya kuleta matunda inaongezamzigo wa tatizo la ajira.Pili kuanzisha viwanda vitokanavyona mazao yanayozalishwa hapa nchini kuliko kuuza mali ghafi nje ya nchi. Na kama nchi inataka kunufaikaviwanda hivi vimilikiwe na serikali kuliko watu binafsi ambao wanawanyonyawafanyakazi. Kama serikali itashindwa basi hivi viwanda vimilikiwe na vyama vyaushirika vya wakulima na serikali iviwezeshe.

Kwa kuwa ushirika umeuwawa nawezi/ wahujumu uchumi, iwepo sheria kali kwamba atakayegundulika akishiriki,kuiba au kutengeneza mazingira yoyote yanayoweza kuua shirika afilisiwe nakufungwa. Njia hii imetumika China ndiomaana tunaona imefikia hapo ilipo.
Tukiweka nguvu kubwa hapa kwakuanzia tutaweza kupata mitaji mikubwa zaidi na hatimaye kuwa na viwandavikubwa ambavyo vitaendelea kutengeneza ajira zenye tija. Dhana hii ya serikalikujisifia kwa viwanda vya watu binafsi si swala la kujivunia hata kidogo. Hatakama wanalipa kodi faida yake si sawa kama vingekuwa vinamilikiwa na serikaliau vyama vya ushirika vya wazalishaji kwani ukuaji wa uchumi utaonekana hatakwa watu wa kawaida. Ni lazima serikali ijiondoe kwenye huu utumwa wa utandawaziambao baadhi ya wanazuoni wanauita utandawizi wa kuachia kila kitu sektabinafsi. Tusipoangalia ipo siku jeshi litabinafsishwa na kuweka usalama wanchirehani.

Pili ni kuanzisha vituo vyawabunifu ambavyo vinamilikiwa na serikali. Vituo hivi viweke mfumo ambao kilamtu mwenye wazo ambalo likitekelezwa linaongeza wigo wa ajira na kukuza uchumikwa ujumla. Na wazo likionekana kuwa na tija serikali igharimie utekelezajiwake. Tunao watu wengi hapa ni wabunifu lakini hakuna mhimili ambao unawezeshakukuza vipaji vyetu. Kuna watu wamesoma wanataaluuma mbalimbali na wenginehawajasoma lakini wanamaono. Baadala ya fedha ya serikali kutumika kuinua wtukama hawa inaishia kutoa posho zisizo natija sambamba na anasa ambazo hazina mchango wowote katika mstakabali wa nchi. Nchi za wenzetu kama china na Marekaniwanapiga hatua kwa njia hii. Lakini simaanishi kwamba kiwango chetu cha maendeleo kiwe kama Marekani ambao wameendambali zaidi kuwa wachochezi wa mahuaji duniani na kuwa mstari wa mbelekuwaangamiza watu ambao itikadi zao ni shindani na za kwao. Mao Tse Tunganasema ni bora kujifunza kutoka kwawaliofanikiwa lakini si kila kitu unaweza kukichukua kwa aliye fanikiwa.Anaendelea kusema kuwa inabidi tuumize vichwa vyetu kufikiri vile tunavyoonavinaendana na mazingira yetu na kuvitumia.

Tujenge utamaduni wauwajibikaji pale tunaposhindwa kuletatija sehemu za kazi. Mtu akipewa nafasi mfano mawaziri, wakurugenzi na watuwengine katika mashirika ya umma. Kila baada ya miezi mitatu kila kiongozi atoeripoti ya kitu kipya kilichofanyika namatokeo yake katika maisha ya wananchi. Kama ni wizara ya viwanda tuelezweviwanda vingapi vipya vimepatikana, vimeajiri wangapi , ubora wa ajira ukoje?Hapa wengine wanaweza kutupa ripoti ya vibarua ambao kipato akitoshelezi hatakwa mtu mmoja. Tupewe ripoti faida kiasi gani imepatikana na iko wapi ilitusije tukaletewa taarifa hewa. Na kwa taasisi ambayo watendaji wakewatavuka kiwango kwa asilimia hamsini (iwe kwa taasisi zinazo zalisha faidakama TANESCO na viwanda vya umma) watumishi wake wapewe bonus. Tukisema kilataasisi basi wanasiasa na watu ambao si wazalishaji wataendelea kuneemekakupitia migongo ya wavuja jasho. Hivyolazima bonus zitolewe kwa wazalishaji au viongozi walioweza kubuni na kusimamia uzalishaji lakini skukrani hiyoiswe kwa viongozi wakuu bali ijidhihirishe kwa wavuja jasho.

Tuepuke kutoa zawadi kwa misingi ya ni nani alijitoa kulinda maslahi ya bosi wake balimaslahi ya umma uwe ndio msingi wa kuangaliwa.
Nasikitika kuona kuna baadhi ya mawaziriwameshika nyazifa tangia hawamu ya pili au ya tatu lakini ukiuliza kigezo kilichotumika kumteua akipo. Kama nikilimo bado wakulima ni kundi lillosahaulika. Nimebahatika kujadiliana na wazeembalimbali ambao wamesomeshwa na mazaokama pamba, kahawa n.k. Lakini sasa ndio maana migogoro Bodi ya mikopo na wanafunzi wa elimu ya juuhaiishi kwa kuwa watoto hawa wa wakulima na wafugaji wazazi wao hawanamatumaini na kilimo au ufugaji wao. Ukienda sekta ya viwanda mtu hakuna jipya amewahi kuleta tofauti na kuua vile vilivyoanzishwa enzi za mwalimu. Nawanao ua viwanda hivi au ushirika wa wakulima ndo hao wanaotumia gharama kubwaza umma kama mafuta , magari ya kifahari na kupigiwa saluti. Ningekuwa mimikila waziri angeanza na bodaboda akifanya vizuri na wananchi wakathibitisha ndoapande daraja ya aina Fulani ya gari.Nahitimisha kwa kusema kwambatatizo la ajira Tanzania pamoja na matatizo mengine yanayoikumba jamii nimatokea ya kuwa na viongozi wasiojali- viongozi wanaoingia madarakani ilikujineemesha wenyewe. Pia naombanipingane na kauli ya Rais aliyotoa kwenye mkutano wa wawekezaji huko Mpandatarehee 17/10/2011 kama ilivyolipotiwa na TBC kuwa , "Tanzania bila wawekezajiwanje hatuwezi kupata huduma yoyote" na Hawa Gasia akagonga msumari kuwa, "Wanaosemauwekezaji ni uporaji ni fikra potofu ambazo hazina msingi". Kwa mtizamo waoviongozi wangu nadhani hawana takwimu sahii kuhusu athari zilizotokana na hawawawekezaji wanaowatukuza. Hatuna haja ya wawekezaji wa nje na badala yaketuwajengee uwezo wananchi hasa vijana ambao ni nguvu kazi katika mstakabali wanachiyoyopte yenye kutaka kuwa na maendeleoendelevu. Wawekezaji wa nje wanaopigiwa chapuo, Wanavuna halafu asilimia mojaya faida waliyovuna kutoka kwetu ,viongozi wanaenda kuomba kama msaada ambao unakuja na masharti yanayodhalilishautu wetu na uhuru wetu kama ushoga. Mwisho vijana wote unganeni hakuna chakupoteza isipokuwa mifumo kandamizi naviongozi warafi. Nchi ya neema na maishabora kwa kila mtanzania inawezekana. Zinduka ajira zipo , ila zimekumbatiwa nawatu wasio kuwa na nia njema.
 
lema aweke mambo nuruni!jk ni mtu wa visasi sana.pia lema ajiangalie sana mienendo yake,hatutashangaa kusikia amekamatwa kwa kosa la ajabu ajabu!ccm huwa hawana cha kupoteza kwani wanajua hawatoboi 2015!
 
Naanza kupata hofu na UCCM Mfu wa huyu Mzee... Anachojaribu kusema hapa nini????? Kuna wadau wanasema huyu Mzee ni miongoni mwa waoiweka CCM Madarakani... Inasemekana ni miongoni mwa inteligent secrets wa CCM just imagine kwenye makala mmoja ya ZITO alimtaja kuwa tangu akiwa 1st year UDSM walishakuwa wana debate na aina ya Muungano ambao unatakiwa kuwepo......

Of course huyu mzee kwa Jinsi anavyocritisize CCM asingeendelea kuwa pale UDSM na kuishi kwenye zile Quarters za Chuo....

Wadau tusaidieni kumchunguza huyu mzee maana ni kama ni wa vuguvugu....

huyu mzee ni kati ya watu walionifanya nisipende kazi ya kufundisha chuo kwa maisha anayoishi. hata mawazo yake huwa simshangai maana nilishamzoe, labda kwa wasiomjua! aliwahi kufumaniwa oficn pale udsm akifanya ngono na mzungu ofcn, ilikuwa mwaka 2007...yaani ni wa ovyo sana. ni mtu anayependa kuwa kinyume na kila kitu. angalia alivyoanza hiyo mada yake, na alivyomalizia. n=yaani ni jitu la kung'ata na kupuliza. sijui mhaya wa wapi huyu ambaye haupo neutral...
 
Watu wa Arusha wanajua CCm na viongozi wake wanaililia Arusha kwa sababu ni wabia wa migodi ya Tanzanite,makampuni yote ya tours ni wahindi,waarabu na baadhi ya binamu zake Ridhiwan,Mtandao wa kumtafutia wanawake Jk,hoteli ya aliyemhonga suti Jk,viwanja vya farasi vya makabulu,hao ndio waleta fujo na wavunjifu wa amani wanakataa sasa hawawezi kuachia watu wakajitajirisha kwa kuwafanya wao manamba
 
Naanza kupata hofu na UCCM Mfu wa huyu Mzee... Anachojaribu kusema hapa nini????? Kuna wadau wanasema huyu Mzee ni miongoni mwa waoiweka CCM Madarakani... Inasemekana ni miongoni mwa inteligent secrets wa CCM just imagine kwenye makala mmoja ya ZITO alimtaja kuwa tangu akiwa 1st year UDSM walishakuwa wana debate na aina ya Muungano ambao unatakiwa kuwepo......

Of course huyu mzee kwa Jinsi anavyocritisize CCM asingeendelea kuwa pale UDSM na kuishi kwenye zile Quarters za Chuo....

Wadau tusaidieni kumchunguza huyu mzee maana ni kama ni wa vuguvugu....

Nafikiri haukumwwelewa kabisa Lwaitama, inahitaji kusoma polepole ili kunyumbua maana.
 
Mkuu Yericko,

Nilidhani na wewe ni great thinker kumbe hamna kitu unapoteza muda wako kusikiliza ujinga wa Lema kweli Tanzania ni masikini si kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya wananchi wake kuwaamini wanasiasa wa hovyo.

Ukweli ni kwamba Tanzania inafanywa maskini na watu wenye mawazo mgando kama yako popompo mkubwa!!
 
''haki ya mtu haidhulumiwi bali hucheleweshwa tu'' bwana Lema songa mbele.
 
Asante Dr. Lwaitama, hakika umeonyesha njia nzuri ya maoni na fikra pevu; Mhe. Lema (bado naona unasitahili uuheshimiwa, mimi naamini hivyo) tuletee waraka wa LEMA sehemu ya Pili, wakati Mhe. Mbowe akimnanga kiwete pia katika Part II yake.
Wasalaam wana mabadiliko na wapenda Utu na Haki ya Mtanzania wa kawaida.
Wsalaam Dr. Lwaitama
 
Weboroya, kila unapochangia kuhusu Lema lazima utaje suala la mimba ya Lowasa. Kumbe kusema yule ana mimba ya lowasa kunaweza kumdharilisha mwanamke kiasi hicho? Lowasa na mke na watoto, je ni ajabu akipata mtoto kwa mke mwingine. Kama ikiwa lema alisema yule mama kafanya mapenzi na mbwa,hapo una haki ya kumshambulia Lema,lakn kufanya mapenzi na lowasa, si dhani kama ni issue kiasi hicho

hauoni issue wakati imemuondoa ubunge!!?? kidding?
 
Back
Top Bottom