Lusekelo anakata tawi alilokalia?

Big up Bro Lusekelo.

Kwa kujitoa sadaka kwa kusema kitu ambacho kinatakiwa kufanyika lakini hakifanyika because of the interests of the few peole.How politicians forcing the writers what to writer?These are two things different serikali ikaharibu inabidi ikosolewe na chombo chake nyewewe not waiting for other media to write.
 
Dua, majaribio yanayofanywa yalifanywa na baadhi ya waandishi waliopinga sera zake za kijamaa. There have been this attempt of dictatorization of Mwalimu!

a. Katika utawala wa Mwalimu kuna watu waliwekwa kizuizini kama watu wanavyowekwa kizuizini sehemu mbalimbali duniani na hawafunguliwi mashtaka. Na niyeye aliyeleta mabadiliko baadaye ya sheria ya kuwaweka watu kizuizini (prevention and detention act). Nchi yetu ilirithi kwa kiasi kikubwa sheria ya kikoloni na kwa muda tulienda nayo hivyo hivyo hasa baada ya kugoma kwa jeshi in 1964 ambapo Mwalimu alitambua kuwa siyo wote weusi ni wazalendo na siyo wote wanaosimama kuapa wana maslahi ya TAifa.

b. Rais Nyerere alitumia uwezo wake wa kisheria, uwezo ambao hata Kikwete leo anao na anaweza kuutumia akitaka. Hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kuonesha kuwa Mwalimu alifanya jambo ambalo halikuwa ndani ya uwezo wake kisheria. Kama kuna wakati ambapo Mwalimu angetaka kuonesha ukiukaji wake wa sheria ni wakati wa kesi ya Uhaini. Leo hii wale wajemaa wangepigwa risasi na kuambiwa ni majambazi.

c. Siwezi kushangaa kuna watu ambao hadi leo hatujapewa maelezo nini kiliwapata. Mwalimu hayupo hai sasa na kama kuna watu wanatakiwa maelezo yao tunao viongozi ambao wanaweza kuruhusu historia yetu iangaliwe kwa karibu na iandikwe sawasawa. Kama Vaticani inaruhusu watu wapitie rekodi ya Papa Pius, nina uhakika kama kuna rekodi ya Mwalimu isiyo sahihi yenye utata inaweza kuchunguzwa.

d. Mzee Geeque, ni watu wangapi waliwekwa vizuizini wakati wa Mwalimu na kwa makosa gani. Tanzania ipo sheria ya Prevention and Detention Act ambayo bado inafanya kazi. Asikudanganye mtu hata Marekani sheria kama hiyo ipo, Uingereza wanayo na serikali nyingi zinazo uwezo huo duniani wa kuweza kumtia mtu kizuizini kwa muda fulani na kumuachia bila kumfikisha mahakamani. Zinatumika sana wakati wa maandamano au vurugu. Miye naomba nitajiwe mtanzania mmoja ambaye alikamatwa akatiwa kizuizini na hakufikishwa mahakamani. Inawezekana wapo lakini haiwezi kuwa kama ulivyosema. Hivi mzee mwenzangu umejuaje watu wengi waliwekwa kizuini bila kufikishwa mahakamani zaidi wakati wa Nyerere kuliko wakati wa marais wengine? Na mzee Geeque, Mwalimu alitumia dola vipi kuwadhibiti waliompinga. Mtei yupo. Babu karudi na kafia TAnzania, Kambona karudi na kafia Tanzania, Fundikira kaishi na kafia TAnzania na orodha goes on and on. Lakini msifanye makosa endapo kuna Mtanzania yeyote anafikiria uhaini ajue kabisa kuwa hakuna demokrasia au utawala bora utakaomuokoa. Hilo ni kosa kubwa katika jamhuri yetu. Wamerekani walishanyonga watu in the fifties kwa makosa ya Uhaini! Hata leo hii ukikutwa na hatia ya Uhaini umekwisha; ndio maana wale ndugu zetu wa Zanzibar waliodaiwa kufanya uhaini Zanzibar waliachiwa na Mahakama!

e. Katika utawala wake wa miaka 25 Mwalimu alitia sahihi hati mbili tu za kuruhusu waliohukumiwa kunyongwa wanyongwe. Yule aliyemuua Dr. Kleruu na mtu mwingine (sikumbuki moja kwa moja). Wakati wa utawala wa Mwinyi watu walikuwa wanapukutika kama njugu (nilipata nafasi ya kushuhudia akinyongwa mtu pale Butimba) in early 90s. Dikteta au kiongozi mwenye nguvu kama Mwalimu angewapukutisha waliompinga. Naomba mnishawishi wazee wenzangu kuwa Mwalimu alikuwa borderline dictator au ametumia madaraka asiyokuwa nayo.

Najua kuna watu ambao hawajamuelewa Mwalimu na hawataki kumuelewa Mwalimu. Madai mengi yanayotolewa dhidi ya Mwalimu hayana msingi katika ukweli ni fiction. Ndiyo maana alipokufa kuna waandishi wa habari wa Kimataifa waliripoti "The TAnzanian Dictator Died".. halafu wakashangaa mbona watu hawaruki ruki na kushangilia?.. Friends Mwalimu was a human being na alifanya makosa na yeye mwenyewe alikiri makosa (sikiliza hotuba yake ya Mei Mosi 1995) but he was not the terrible man and benevolent dictator some people are trying to potray him. No sir, he was not.

Babu na Kambona si walirudi baada ya kuanzishwa kwa siasa ya vyama vingi...tena wakati Nyerere keshastaafu....kwa hiyo hata kama walikuwa wanapingana enzi za utawala wake sidhani kama beef yao ilikuwa intense namna hiyo. Kwa nini hawakurudi 80,81,82,au 83? Au kwa nini kwanza walikimbia..?
Kwa jinsi unavyomhusudu Mwalimu mimi siamini hata kidogo kama unafikiri alifanya makosa pamoja na ubinadamu wake. Tutajie hayo makosa aliyoyafanya. Halafu hii hotuba ya '95, ni nini cha ajabu alichosema zaidi ya kuzungumza common sense? Sioni hata kidogo umaarufu wa hiyo hotuba zaidi ya yeye kuzungumza mambo ya kawaida kabisa.

NB: Hii haihusiani na mada hii lakini nataka niwakumbushe watu hapa. Mwaka '95 wakati wa kampeni za uraisi, Nyerere alikuwa kwenye moja ya kampeni za kumpigia debe Mkapa. Katika moja ya madongo yake kwa frontrunner wa upinzani (Mrema) alisema hata kama mtu anapenda kubebwa kama jeneza...msimpe kura au kitu kama hicho. Siku chache baada ya hapo magazeti binafsi yakachapisha picha ya huyo huyo Nyerere akiwa amebebwa na watu (kama jeneza) ktk moja ya mikutano yake wakati wa kutafuta uhuru. Nilicheka sana siku hiyo. Kumbe na yeye kuna kipindi alikuwa ana enjoy kubebwa kama jeneza.....
 
mzee ushawahi kusikia "self imposed exile"... ? Mambo yanaweza kumuendea vibaya akaamua kukimbilia nje ya nchi.. akajiita mkimbizi..
 
Sishangai kuona tuna ushabiki wa Baba wa Taifa. We all want heroes in our lives. Mwalimu alifanya mengi mazuri na ya kujitolea. Tusisahau alivyokazana kuwajengea nyumba wananchi wa Dodoma. Si kitu kidogo Rais kushinda juani siku baada ya siku akijenga nyumba za udongo.

Wale ambao hawakukubaliana na Mwalimu waligonga mwamba kweli kweli. Kasanga Tumbo alikuwa wa kwanza. Tunasikia alilazimishwa kukaa Sumbawanga miaka 10. Huko kulikuwa ni kuwakosea haki watu wa Sumbawanga vile vile. Ilikuwa Gulag ya Mwalimu.

Hatufahamu kwa undani Mwalimu alitofautiana nini na Kambona. Hatuwezi kuwauliza kwani hawapo tena nasi. Inasemekana tofauti zao zilihusu Azimio la Arusha. Ilikuwa haikubaliki hata kidogo kutofauitiana na Mwalimu kwenye mambo ya msingi.

Kassim Hanga alifanya kosa gani? Aliishiaje? Iko siku itabidi tuweke wazi Historia ya nchi yetu. Si vema kuendelea kuficha ficha kila kitu.

Kuna wakati wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, mwenyewe nikiwemo, tulifanya maandamano kupinga Wabunge kujiongezea mishahara na wakulima wa tumbako Tabora kukatwa 75% ya bei ya zao lao ili kulipa mikopo ya Benki ya Dunia. Ilitumwa idadi ya polisi kubwa kuzidi ile ya wanafunzi kutukamata. Ili kuhalalisha, Mwalimu akatangaza redioni kwamba tuligoma kupinga kupelekwa vijijini kama wataalamu! Kama singekuwepo mwenyewe singeamini Mwalimu aliweza kudanganya hivyo.

Tuwe na balance kuhusu Mwalimu. He won some and lost some.
 
Halafu kuna huyu mzee anaitwa Mzee KaziBure(Marehemu) mtaalamu wa Physics inasemekana alisoma na Nelkon.ninasikia(sina uhakika)kwamba alifanyiwa kitu mbaya na utawala wa mwalimu.

Kuna mzee mwingine anaitwa Tuntemeke Sanga, huyu alikuwa msomi aliyebobea, lakini nasikia alifungiwa asitoke nje ya mkoa aliokuwa anaishi kutokana na kutofautiana na utawala wa mwalimu, baadae alikuja kuachiwa na hatimaye kuweza kuingia katika ubunge.

sasa mambo ya namna hii ni mambo gani?.

Besides Vita ya Kagera ni Kweli Amini alituvamia au sisi ndo tulimvamia?

Yeye ndo alituchokoza au sisi ndo tulimchokoza?
 
Jamani eeeh..hatutaki mambo ya "nasikia alifanya hivi au vile" hapa. Tuzungumzie ukweli (facts). Je ni kweli wakati wa utawala wa Mwalimi vyombo vya habari binafsi (vya ndani)viliruhusiwa kufanya kazi? Nani anajua majina yake? Na sheria ya vyombo vya habari ya wakati ule ilikuwa inasemaje?
 
Wale ambao hawakukubaliana na Mwalimu waligonga mwamba kweli kweli...
Hatufahamu kwa undani Mwalimu alitofautiana nini na Kambona. Hatuwezi kuwauliza kwani hawapo tena nasi. Inasemekana tofauti zao zilihusu Azimio la Arusha. Ilikuwa haikubaliki hata kidogo kutofauitiana na Mwalimu kwenye mambo ya msingi.

Tuwe na balance kuhusu Mwalimu. He won some and lost some.

Kuhusu Mwalimu na Kambona habari za kuaminika zinasema kwanza walikuwa ni mabesti sana na waligombea uhuru kwa pamoja na kuupata. Walikuwa mabesti hivyo kwamba ni fact harusi ya Kambona bestman wake alikuwa Mwalimu. Halafu Kambona inasemekana alikuwa ni kiongozi pekee aliyekuwa na hoja na kuangaliana na Mwalimu in the same level, yaani hakuna hapa aliyekuwa bora kuliko mwenzake walikuwa in the same level na walishindana kwa hoja.

Mwalimu alimuheshimu sana Kambona, hata siku ile wanajeshi walivyogoma na kutaka kumpindua Mwalimu, mwalimu alifichwa na wana usalama ni kambona mwenyewe ndiye aliyewaface wanajeshi na kuwa-convince waache ujinga na wakatii, wakati huohuo alimshauri Mwalimu kuomba support kwa majeshi ya nje kama uingereza kuja kusawazisha mambo na soo likaisha, Mwalimu pia alimsifu sana kambona katika hili.

Tatizo lilianza mwalimu alipotembelea China na kukuta viongozi wanaabudiwa na kusujudiwa na nchi ikiwa na chama kimoja cha siasa, sasa alivyorudi na kutaka kuanzisha mfumo wa chama kimoja cha siasa ndio hapo Kambona hakukubaliana naye akisema ingekuwa rahisi nchi kuingia kwenye udikteta na pia rahisi kumpachika raisi yoyote bila kuconsider wananchi wanataka nini, somehow Mwalimu kama mkuu wa nchi aliweza kuwaconvince majority na mfumo ukabadilika.

Tatizo la pili lilikuwa ni azimio la arusha, Kambona alikuwa ana favour mambo ya soko huria na u-capitalism, hata pale Mwalimu alipotaka vijiji vya ujamaa na kupitisha sera zake, kambona akamwambia Mwalimu tusiwalazimishe hawa watu, acha tutengeneze vijiji vichache vya ujamaa kama plot projects halafu vikifanikiwa tuwaonyeshe wananchi kwamba hivi ni vitu safi kwa hiyo hatutakuwa na haja ya kuwahamisha kwa nguvu, namba one tutajua ufanisi wa hii sera na namba two tutawapa wananchi fursa ya kuchagua wenyewe. Hapa Mwalimu akang'aka na mahusiano yake na kambona yakaanza kuharibika. mwalimu akaendelea na sera zake, Kambona akaona mazingira ni very hostile akaamua kukitoa kinyemela, huku nyuma wakamvunjia nyumba yake, ndugu zake wakakamatwa nakadhalika.

Baada ya miaka mingi kupita sera za Nyerere za kijamaa na vijiji vyake zika-fail, sera za socialism zaika-fail vilevile, mfumo wa chama kimoja ukaonekana ni wa kidikteta.

Then Nyerere akatambua Kambona was right, alivyostaafu akaanza kuzi-campaign sera ambazo kambona alizitetea miaka 40 iliyopita na kurudisha mfumo wa vyama vingi, raisi aliyemfuata akaanza kuleta u-capitalism na Kambona akarudi Nyumbani, lakini Kambona ndo akawa ameshazeeka nyota yake ishafifia, Nyerere ashapandikiza mbegu kwa watanzania kuwa fikira zake ni sahihi etc. Kwa hiyo we now can never know if Mwalimu angekuwa anashaurika je tungekuwa hapa? je angetawala miaka 25? au Viongozi wengine kama kina Kambona labda nao wangegombea na kuuza sera? maana enzi zile ilikuwa Nyerere anagombea na kivuli sasa wewe utachagua kivuli au charismatic Nyerere?
 
Ndugu zangu, uongozi haupimwi wakati wa heri na fanaka; Uongozi hupimwa wakati wa adha na mashaka. Siyo Mwinyi, Mkapa, au Kikwete ambao wameongoza Taifa letu wakati wa Adha na wakapimwa. Mara zote ambapo tumekumbana na magumu tumeona jinsi gani character za viongozi wetu zilivyo.

Madini:
Nyerere alifahamu Tanzania imebarikiwa madini kwani baadhi ya maeneo yalisanifiwa tangu miaka ya hamsini hivi. Kwa makusudi kabisa alichelewesha sana kuingia kwenye madini na akajaribu kujenga Taifa akiwa msingi kwenye kilimo kama Uti wa Mgongo. Mwalimu aliona hatari ya wageni kuvamia madini yetu na jinsi gani hilo linahatarisha uhuru wetu. Akaamua tusubiri. Nchi zile ambazo ziliruhusu wageni kuingia na kuchota madini zikaishia kuwa DRC, Angola, Sierra Leone, Nigeria n.k Mwalimu aliamini kabisa kuwa siku moja tutaweza.

Siasa za dunia.
Watu wengi wanafanya makosa ya kumhukumu Mwalimu kwa kuangalia siasa za leo. Wakati tunapata uhuru 1961 na Mapinduzi 1964 Ulimwengu ulikuwa ndio umeanza kuingia katika kile ambacho kilijulikana kama "Vita Baridi". Wakati ule viongozi walihukumiwa kwa jinsi gani walichagua upande kati ya Kambi ya US (Nato) na Warsaw Pact (USSR).

Mgawanyiko huo ulilazimisha nchi nyingi hasa za "dunia ya tatu" kujikuta wanachagua marafiki na adui zao na kuacha marafiki zao kuwachagulia maadui zao. Mwalimu tangu mwanzo aliona hatari hiyo na kwa makusudi kabisa akaamua kuja na sera za kutofungamana na upande wowote (pamoja na viongozi wengine wenye mawazo kama ya kwake). Gharama ya kutofungamana na upande wowote ni kuwa hatukuwa karibu na Mshindi US kama walivyofanya nchi nyingine. Nchi zile zilizokuwa karibu na US viongozi wake wengi na siasa zake nyingi zikabakia kuwa za kibepari na viongozi wake wakawa vikaragosi vya Magharibi. Mobotu, Bokassa, Banda, n.k waliangukia upande huo na viongozi wote ambao walikuwa wanaonekana na hatari.

Ukipata nafasi ya kuangalia declassified reports za US Department of State za miaka ile utaona ni jinsi gani US walivyokuwa wanamshuku Mwalimu hasa alipokuwa anakaribiana sana na Urusi au Uchina. Kifo cha Patrice Lumumba na yaliyomkuta Nkrumah yalikuwa ni somo zito kwa Mwalimu. Hata hivyo Mwalimu aliamua kubakia na nchi masikini lakini huru, kuliko kuwa na nchi tajiri lakini haina uhuru! Ni kwa sababu hiyo katika umasikini wetu tukaweza kujenga Taifa la watu wenye umoja, ukarimu na linalojali kuliko Mataifa mengi ambayo yalikuwa na utajiri (wa vitu) lakini wakiwa na umasikini wa utu.

Makosa ya Uongozi.
Itakuwa ni makosa makubwa tena ya kihistoria kwa mtu kudai kuwa Mwalimu hakufanya makosa au hakufanya maamuzi yenye makosa. Yeye mwenyewe alijua hivyo na wanaoanglia historia yake kwa haki wanatambua hivyo. Suala la Vijiji vya Ujamaa lilitekelezwa kwa makosa makubwa na yeye mwenyewe aliriki hivyo; Hofu ya uongozi kupinduliwa ilikuwa ni hofu ya msingi wakati ule. Mgomo wa wanajeshi wa 1964 (Army Mutiny) haikuwa Tanzania peke yake kama baadhi ya watu wanafikiri. Ulikumba Kenya, Uganda, na kukawa na mgogoro kule Malawi wa Baraza la Mawaziri (Uliosababisha Kanyama Chiume kukimbia uhamishoni). Hivyo miaka ya mwanzo ya uhuru kulikuwa na hofu katika nchi nyingi za AFrika ambapo matishio ya mapinduzi ya kijeshi yalikuwa yananukia.

Mlolongo wa mapinduzi ya kijeshi Nigeria, Uganda, tishio la mapinduzi Kenya, n.k vilikuwa ni vitu ambavyo vimetuzunguka sisi. Mwalimu kama kiongozi yeyote makini asingeweza na asingepaswa kuvumilia mawazo ya kimapinduzi ya kijeshi au hisia za uhaini. Ndio maana nimejaribu kuwaonesha watu wengine hapa kuwa hata leo hii kama kuna mtu anaanza kuja na hisia za kimapinduzi au uhaini atakutana na mkono ule ule wa kisheria.

Leo hii hakuna nchi ambayo inaweza kuvumilia mawazo aidha ya kumuua Rais au kutishia uwepo wa Jamhuri; Hakuna nchi kama hiyo. Hata nchi ambayo tunaamini kuwa ina uhuru wa maoni kama Marekani hairuhusu maoni ya namna hiyo na kama hamuamini nendeni kwenye chati halafu andikeni mnataka kumuua Rais wa Marekani muone kama mtalindwa na "uhuru wa maoni". Wakati ule viongozi wengi wa AFrika na nchi nyingine za dunia ya tatu walikuwa very paranoid and Mwalimu was not an exception.

Hili linanileta kwenye pointi ya watu walivyoshughulikiwa. KUna watu ambao kutokana na maoni au mawazo yao walitishia uwepo wa jamhuri changa na kuachwa waendelee ni sawa na kuwapa mabomu mkononi. Ilipaswa washughulikiwe. Sasa tunaweza kujenga hoja na ni ya msingi kuwa sheria iliyotumika wakati ule (ambayo bado ipo vitabuni) ilikuwa ni sheria ya kikoloni na ambayo imepitwa na wakati.

Azimio la Arusha
Sijui kama kuna watu wameenda kusoma mazingira ya kutangazwa Azimo la Arusha na kwanini ilibidi tuwe nalo. Nawashauri mlisome tena halafu mje kunionesha ni vipengele vingapi hamkubaliani navyo; I can guess nationalisation, nationalization, nationalization! Kwa watu wengi kitendo cha Mwalimu kutaifisha mali ya watu binafsi na kuifanya iwe ya Taifa ni jambo ambalo halisameheki; Hata hivyo hakuna anayetaka kuangalia ukweli wa kihistoria kuwa nani alikuwa ana miliki mali, na nani alikuwa ana nafasi ya kumiliki mali wakati ule na kwanini kama Taifa tusingeweza kuacha hali hiyo iendelee.

Yawezekana kuna vitu ambavyo visingepaswa kutaifishwa na bila ya shaka kuna utekelezaji wa sera za Azimio. Ukweli ni kuwa kama tusingeshughulikia suala la Ardhi, mali ya umma wakati ule, leo hii tungekuwa tunahangaika na masuala ya kama ya Zimbabwe, Kenya au hata AFrika ya Kusini. Mwalimu alifanya jambo sahih pamoja na makosa yake.

Azimio lilikuwa na dira kama ya Taifa na lilikuwa na maono yaliyoeleweka. Azimio la Arusha lilikuwa ni kama taa ya kuangaza wapi tunataka kwenda, misingi yake bado ni kweli leo hii kama ilivyokuwa miaka 40 iliyopita. Ukiondoa vipengele vichache utaona kuwa Azimio lilijenga msingi wa ujenzi wa Taifa.

- Fedha si msingi wa maendeleo; ukweli huu wa Azimio la Arusha ulitusaidia kujenga nchi kwa kujitegemea sisi wenyewe. Nyumba bora tulizenga kwa nguvu zetu, mashamba tulilima wenyewe n.k Leo hii tunasubiri mjomba wetu aje kutoka ulaya kututengenezea vyoo, kutuangalizia wagonjwa wetu na kutuangalizia watoto yatima wetu. Tumekuwa tegemezi siyo kwenye vitu tu bali hadi kwenye utu ambapo mtanzania mwenzetu haaminiki kupewa nafasi ya kuongoza kampuni ya Kitaifa tunaenda kuomba wageni! Mwalimu pamoja na umasikini wetu wote aliwapa watanzania nafasi ya kuongoza hata walipoboronga; Mwalimu hakuwa tayari kwenda kupiga magoti kwa kina "Smith" kuwaomba waje watuandikie mikataba yetu ya madini! Leo hii sisi na viongozi wetu hatuna haya tunatangaza "Wamarekani wamsifia Kikwete"; "Kikwete apagaisha Ulaya"n.k Ni utumwa huu wa kifikra ambao Mwalimu aliupinga kwa kutetea utu wetu na haki yetu kama watu kujiamulia mambo yetu wenyewe hata kwa makosa.

Alifanikiwa alichotaka?
Ni mtu mwongo asiyekubali kuwa Mwalimu alishindwa kwenye mambo kadhaa na baadhi ya maamuzi yake hayakuwa sahihi. Mwalimu alifanya makosa mengi kama kiongozi na kama mwanadamu. Hata hivyo aliongozwa na kanuni bora zaidi kuliko zinazowaongozwa viongozi wetu wa leo hii ambao hawana hata kanuni za kuanzia. Mwalimu alikuwa na ujasiri wa kukataa na kuamua njia inayotufaa sisi. Uongozi siyo uwezo wa kuwaridhisha watu wote wakati wote; uongozi ni uwezo wa kuwaridhisha watu wengi karibu wakati wote. Kiongozi asiyekuwa tayari kukosea au kuwaudhi watu hastahili kuitwa kiongozi.

Ukinipa uchaguzi wa viongozi kati ya Mwinyi, Mkapa, Lowassa, Kikwete na Nyerere; bado nitamchagua Nyerere any given Day!! Call me naive or whatever but I still believe we as a nation were so blessed to have Mwalimu walk and lived among as; we were witnesses of a legend, witnesses of a great man albeit his many shortcomings! I believe that with all my heart, and so far, I'm still inspired by Mwalimu's legacy, records, ideas and yes even his personality. I'm not ashamed of that and neither should you!!
 
Good job! That is a very fair and synoptic assessment of Mwalimu. Me, like you, with all of his shortcomings as a human being, on any given day, given the choice of all four that we've had so far, without hesitation and enthusiastically, he will be my choice.

But I also feel like there is a need to have an in-depth discussion of where and what he did wrong during his rule. There are a lot of myths and half-truths about him that still dog him to this day and I think it is right about time we get the story straightened out and dispell everything (or try to) that is not true.
 
Kwanza Mzee mwanakjiji nashukuru kuweka hiyo mawazo hapo juu, that side of Nyerere is shining no Doubt!Nyerere sera nyingine zake zilikuwa safi sana, wazazi wetu walisoma bure, sisi tulisoma bure na sasa tunatesa.

Hapo Chini kama Mzee Nyani Ngabu alivyosema, mimi pia nina mawazo yenye huo muelekeo. Historia yetu tuichambue, historia ya viongozi wetu tuichambue, tujue wapi walicheza pele na wapi walicheza Taifa stars.
Na tusiwe wavivu wa kufikiria na wa kuchambua tusimuachie mtutu mmoja fikira zake pekee ziwe sahihi tutakuwa tunamuonea sana, lazima tumsapoti mtu mwenye fikra, tufikirie nae tumuongezee changamoto. Kwa hiyo enzi zile wazazi wetu walivyokuwa wanasalimiana kwa kusema zidumu fikra sahihi za mwenyekiti kwa maoni yangu walimuonea, Jamaa alishawaambia umoja ni nguvu kwa nini walimtenga afikiri mwenyewe? kwa hiyo tuchambue pamoja na kutambua wapi palikuwa safi na wapi hakukuwa na waliomzunguka mwalimu walichangia vipi?

....

But I also feel like there is a need to have an in-depth discussion of where and what he did wrong during his rule. There are a lot of myths and half-truths about him that still dog him to this day and I think it is right about time we get the story straightened out and dispell everything (or try to) that is not true.
 
Waacheni wafu wapumzike! Tangu aachie madaraka ni miaka 22 na sioni chochote kilichoongezeka cha maana ndio kwanza skendo zinazidi!
 
Waacheni wafu wapumzike! Tangu aachie madaraka ni miaka 22 na sioni chochote kilichoongezeka cha maana ndio kwanza skendo zinazidi!

Mze mzima FD, Mimi binafsi satamshau, Nyerere nitaendelea kumkumbuka kumuongelea na kujifunza kutoka kwake katika mazuri na mabaya. Nchi nzima pia Nyerere hatasahaulika, hata viwanja vya kimataifa vinabadilishwa majina na kuitwa Nyerere.

Yaani tumuache kumzungunmzia na kumkumbuka as if he never existed kwa kisingizio tuwaache wafu wapumzike hii si itakuwa dharau kwa Baba wetu wa Taifa jamani?
 
Back
Top Bottom