Nifah
JF-Expert Member
- Feb 12, 2014
- 31,530
- 65,286
Mnakumbuka wakati msiba wa Kanumba unatokea kulisemekana kutokea ugomvi uliopelekea Lulu kumsukuma Kanumba ndio kuanguka na kufariki?
Chanzo ni simu kutoka kwa Ali Kiba kwenda kwa Lulu.
Lulu alienda kwa Kanumba waliyekuwa na miadi naye, na in fact yule (Kanumba) ndiye alikuwa mpenzi rasmi, huku Ali Kiba akila kisela kama kawaida, ila kwa mapenzi mazito!
Basi… ndipo Lulu kusikika akiongea kwa simu na mwanaume kimahaba, alipotakiwa kusema ni nani ndipo ukazuka ugomvi ulioliacha taifa na simanzi!
PENZI NI ZITO!
Jamani mnaambiwa hawa watu ni wanapendana kuliko mnavyoweza kufikiri! Yale mahaba ya Vee & Rotimi hayaoni ndani!
Na wanavyoyaendesha mapenzi yao wanajua wenyewe! Maana kila mmoja ni mkavu hadharani, mwanaume akatangulia kuoa, mwanamke nae akaolewa!
Ila wakutanapo moto huwaka! Nyasi huchanika!
Ni wanapendana hakuna mfano!
Najua mtajiuliza kama mimi nilivyojiuliza wakati nahakiki huu ubuyu, inawezekana vipi?
Yule Majizo ni mume rasmi tu wa hadhira, na huku Ali akiwa ameshatengana na mkewe Amina (japo talaka bado) hivi sasa akiwa na Babe Sherie, kote huko wanazuga tu.
Moyo wa Lulu uko kwa Ali Kiba, Ali nae Lulu ndio mwanamke wa maisha yake!
ACHANA NA SALAMA…
Ndio, Lulu huwa anasagana na Salama Jabir, Ece Jay… huyohuyo! Kwa kitambo tu.
Na huwa ni pale Lulu anapokuwa na mastress yake anayopewa na mumewe anayetuhumiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja zaidi na mtangazaji maarufu kutokea Arusha, huwa anaenda zake kwa Salama wanatoana cheche stress zake zikipoa anarudi kuendelea na ndoa yake!
ACHANA NA NDAMA MUTOTO YA NG’OMBE!
Si mnaonaga Lulu anavyotuchamba “Catch the flight not the feelings “?
Ndio hivyo, akishapewa stress zake huko na mumewe au akiwa na shida zake za hela (Majizo bakhili)anamtafuta mubaba wake, anampandia ndege Ndama anaenda kutulizwa na kuondoka na maokoto yake.
ALI KIBA NDIO ZAIDI!
Achana na hao woooote! Hakuna aliyeweza kusuuza moyo wa Lulu kama Ali Kiba. Ali ndio kiboko ya wote, mwanaume wa maisha yake!
Wanapeana nini? Sitaki kusema zaidi, ila wote inasemekana ni mahodari wa mchezo mbaya, mchezo haramu uliokaripiwa kwa karipio kali katika vitabu vyote vya dini! Mchezo ulioangamiza kila kiumbe katika mji ulioshindikana kuishi kwa kiumbe chochote hadi hii leo!
Hayo ndio maisha ya mastaa na vimbwanga vyao!
Leo team kataa ndoa wataondoka na ushindi…
Wasalaam,
Nifah.