Lukuvi na Nape Wamethubutu

Lukuvi na Nape Wamethubutu

Aliyesema baa ifungwe naye alitaka auze jina kidogo, kilaza tu.
Tanzania imekua mbaya balaa, yaani diaspora wote waliokua na hamu ya kurudi wameahirisha, Tz imekua sehemu mbaya sana ya kufanya biashara, kilaza yoyote anauwezo wa kuifunga anytime anavyojisikia.
 
Utakuta sababu kubwa ni ati mtu alikipigia kura Chama fulani na si Chama fulani, au kikao kilifanyika ktk Bar yake, Lakini lazima tujue. Baada ya Uchaguzi Na Raisi kupatikana Nchi lazima irudi iwe kitu kimoja. Raisi au wateule wakianza kuwabagua watu ni Laana kubwa Kwa Mungu. Hivi kweli Tanzania hii Malaya wako Kona bar tu. Mambo mengine yanayofanywa na awamu hii. Hata fala kabisa anastukia. Viongozi fanyeni kazi. Acheni chuki na wananchi
 
Ni kweli brother, na Kama ndivyo basi hata hapo Dodoma Pindi bunge likianza vikao huwa Malaya wanajaa kila kona ya huo mji, kwa hiyo tuseme basi na Bunge lifungwe? Ifike mahali viongozi wafanye kazi kwa weledi. Hii mihemko haitatufikisha popote

Ninachokiona kuna chuki za UKANDA pia,inategemea mwenye mali anatoka kabila au ukanda upi.
 
Mambo mengine yanaudhi sana. Sasa Kama huyo kilaza aliyekwenda kumuweka Nabii Ngwajima Ndani akidai anatumia Madawa ya kulevya wakati akijua Kabisa ni Uongo, Halafu ati Mpaka sasa hivi hajajiuzulu!. Halafu ati bado tunasema tuna viongozi. Hawa hawana tofauti na Majambazi, maana mtu Muongo ni jambazi tu, Tanzania imekuwa Nchi ya hovyo haijapata kutokea,
 
Nasikia makonda anacompile report ya wanunuzi wa ngono na walalaji wa guest mchana na weekend, siku akiisoma Dar patakuwa hapatoshi manake kuna vigogo wengi washatajwa tayari.
 
Mkuu wa mambo ya ndani ni nyoka, ndumila kuwili, opportunistic to the extreme...... all are opportunistic, but this Mkuu wa mambo ya ndani goes to the extreme!
Ni dhahiri kabisa.
 
Tunapolipa kodi zetu maana yake Tunataka uzipangie vizuri kwa ajili ya maendeleo yetu, hatulipi ili zitumike kuwapa watu wasio na hatia mateso na kufedhehesha watu, manyanyaso na kubagua watu.Sisi tunaolipa haimaanishi hatuna Akili, wengine tunazo nyingi kiasi kwamba hata Uwaziri tunaona ni kazi ndogo, tena stress, hivyo, Tendeni haki ili Taifa lisonge mbele, Kwani Hado mpaka sasa hamjastuka tu kuwa hili Gari sasa hivi linarudi nyuma badala ya kwenda mbele! Na sijui tutatumbukia ktk mtaro gani
 
Kwa suala la mawaziri na Makonda nakuunga mkono kwa Corner Bar acha wafungiwe na sio hao tu Waende Bar nyengine zinazofuga mashoga na machangudoa, Hapi ana umakini katika maamuzi yake,sorry kama ulikosa huduma mkuu.
Watu kama Nyie ndiyo wanafki wakubwa!
Nyie ndiyo wakwanza huwa mnaenda kuwafata makahabaaa

Ova
 
Nasikia makonda anacompile report ya wanunuzi wa ngono na walalaji wa guest mchana na weekend, siku akiisoma Dar patakuwa hapatoshi manake kuna vigogo wengi washatajwa tayari.
Miaka inakatika, badala ya ku deal na vitu vya kupeleka Taifa mbele mna deal na vitu vya hovyo hovyo kwa kutaka sifa,wakati Wananchi wameshakosa Dira, hawaoni hata kiwanda kimoja, ati mmebaki na kupima watu mikojo ili mjue Kama wanatumia madawa, sasa hata Kama. Wananchi watanufaika na nini!
 
Raisi timu hawa watu mizigo haraka,wewe mwenyewe ulituahidi utakuwa Raisi wa watu wote, bila kubagua Rangi, Dini, Chama Wala Kabila.ila yanayofanyika sasa hivi, wenye akili Tunashangaa sana!
 
Hiki anachokifanya Happi ni kutafuta kick, navuta picha nakumbuka awamu hii ya tano ilivyoingia madarakani na mikwara. Nakumbuka kigwangwala aliwahi hosptal moja kufungia gate wafanyakazi waliochelewa bila kuangalia uhalisia wa usafiri. Huyo Happi hana tofauti na yale aliyosema Makonda eti waalimu watasafiri bure.
 
Niliangalia taarifa ya habari ya ITV Jana nikamwona Waziri Lukuvi akimtuhumu Makonda kwamba ametapeliwa, Pia ukisoma Post za Nape, yeye hamumunyi maneno. Anamchana Makonda wazi bila ya kupepesa. Nimeshangaa sana kumwona Waziri wa mambo ya ndani akiwa kimya

Anayoyaposti nape yalitakiwa yaongelewe na waziri wa mambo ya ndani, maana suala la kukamata na kuwataja watu hovyo hovyo bila ushahidi ni kosa la kijinai kisheria.

Kituko kingine nilichokiona, ni kijana mmoja naye ni mpenda sifa, ati Amemfungia mmiliki wa kona Bar ati kwa sababu kuna machangu doa wengi wanapenda kwenda kujiuza pale, huyu mwenye bar Ana leseni halali ya kufanya biashara husika, na amekuwa mlipa kodi kwa miaka Yote,

Cha kujiuliza, yeye Ana makosa gani mpaka afungiwe na bwana Hapi? Je Waziri wa viwanda na biashara hapo ofisini anafanya kazi gani ikiwa anaogopa kukemea upuuzi Kama huu?. Kazi ya kudhibiti machangudoa ni ya polisi ambao wanalipwa mishahara kwa kazi Yao. Au waziri Mwijage nae anamwogopa Hapi kwa sababu aliachiwa ofisi na Makonda alipokuwa likizo kwa hiyo naye anaonekana hawezi kuguswa hata akiboronga?

Huu ni mfano tu wa mawaziri waoga, Kwa style hii, hawa mawaziri watamsaidia vipi Raisi Ambaye kwa sasa anaandamwa kila upande kwa sababu ya hali mbaya ya maisha ya Watanzania iliyosababishwa na matamko Kama hayo yasiyo na tija yoyote kwa Taifa? Mwigulu Na Mwijage.
biashara ya kuuza miili nyie wadada ni mbaya, na ni dhambi. hata hivyo, ni vigumu kwa mwenye eneo kufahamu kuwa huyu aliyekuja ni chagu au la, hata wale wanaojipanga nje ukiwauliza watasema kuna mtu tunamsubiria....huwezi kufight dhambi kimli, utafight dhambi kiroho.hata wakifukuzwa hapo wataenda tu huko insta na badoo kwasababu iyo ni roho ipo moyoni, ni Yesu pekee anaweza kuiondoa baada ya kuokoka. kabla ya hapo hata ukiwapa pesa nyingi, au ukawafungia ndani, watatoroka tu na kwenda kujiuza. ni utumwa, ni kifungo kama vifungo vingine tu.
Jitafakarini, mnaogopa nini kuwaambia hawa vijana wafate taratibu?. Mkiendelea kuchelewa kuchukua hatua iko Siku hata Waziri mkuu ataingiliwa naye ataogopa, Heko Lukuvi Heko Nape.
 
Hiki anachokifanya Happi ni kutafuta kick, navuta picha nakumbuka awamu hii ya tano ilivyoingia madarakani na mikwara. Nakumbuka kigwangwala aliwahi hosptal moja kufungia gate wafanyakazi waliochelewa bila kuangalia uhalisia wa usafiri. Huyo Happi hana tofauti na yale aliyosema Makonda eti waalimu watasafiti bure!!
Hahahahaaaaaa, Kigwangala ni wale wale, Anafanya kazi kwa uoga, ati Juzi anataka kutupa Orodha ya Mashoga, are we serious? Sasa Hilo linawapa wananchi faida gani hata wakitajwa. Hopeless,
 
Kwani tatizo ni Bar au Mamlaka za kiutawala ambazo zinapaswa kuhakikisha hiyo biashara ya uchangodoa haifanyiki, kama ndiyo hivyo makondoe makaburi ya kinondoni, mitaa ya ohio na barabara ya shekilango yote,
Mwenye bar hana kosa lolote
 
Back
Top Bottom