Lukuvi DOWANS ni "petty issue"..........

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
‘CCM kinapitia wakati mgumu’
Saturday, 29 January 2011 08:33

Elias Msuya na Fredy Azzah

KIKIWA kinatimiza miaka 34 tangu kuzaliwa kwake Februari 5, 1977, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimelezewa kuwa, ingawa kimeendelea kushinda nafasi ya urais nchini, kinakabiliwa na wakati mgumu.

Wakizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, wabunge wa CCM walisema chama hicho hakiwezi kufa kwa sasa, lakini kinapitia tu wakati mgumu kama ilivyo kwa vyama vingine duniani.

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), William Lukuvi, alisema kwa kipindi cha miaka 34 ambacho CCM imekuwa madarakani, kimefanikiwa kufikia malengo yake hasa kwa kushinda chaguzi zote.


“Chama chochote kile duniani, malengo yake ni kushika dola. Kwa kipindi chote CCM tumefanikiwa kushika dola. Hata kwenye michezo, kama timu inashuka daraja mwenye timu huivunja,” alisema Lukuvi.

“Chama cha siasa ni taasisi endelevu, sio kwamba tumeongoza kwa maziwa na asali. Tunapitia kwenye milima, misitu na vichaka.

Ni jukumu letu kujitambua ili tuendelee kushika dola,” alisema. Kuhusu suala la Dowans ambalo limeonekana kukigawa chama hicho kabla ya wabunge wake kukutana na kuweka msimamo wa pamoja, Lukuvi alisema hilo haliwezi kukigawa chama.“Chama hakiwezi kugawanyika kwa ‘petty issues’ (mambo madogo madogo).

Chama kupitia mwenyekiti wetu alishasema jambo hilo sio kubwa. Ni uhuru wa maoni tu, kama ni mawaziri kupingana watakuwa wamevunja kanuni zao, sio chama,” alisema.

Naye Mbunge wa Uzini, Muhammed Seif Khatib, alisema sio kwamba CCM imepoteza mwelekeo, bali kinakwenda kulingana wakati ulivyo.

“Sioni kama chama kimepoteza mwelekeo, kinakwenda kulingana na wakati, dunia imebadilika, mahitaji yameongezeka, vionjo vimeongezeka kwa hiyo chama kinakumbana na mazingira ya wakati huu,” alisema. Alikitetea chama hicho kuwa, hakiwezi kuleta pepo duniani na kwamba, matatizo yapo duniani kote sio Tanzania pekee.

Kuhusu suala la Dowans, Khatibu alisema kilichotokea ni uhuru wa maoni sio kugawanyika kwa chama. Naye Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Stella Manyanya, alisema kwa kipindi cha miaka 34, chama hicho kimefanya mambo mengi mazuri ambayo yameifikisha nchi hapa ilipo, na bado kina uwezo wa kuongoza miaka mingi ijayo.

Hata hivyo, Manyanya alisema changamoto anayaoiona ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi, ni suala la mawasiliano.
 
PHP:
Ni jukumu letu kujitambua ili tuendelee kushika dola," alisema. Kuhusu suala la Dowans ambalo limeonekana kukigawa chama hicho kabla ya wabunge wake kukutana na kuweka msimamo wa pamoja, Lukuvi alisema hilo haliwezi kukigawa chama."Chama hakiwezi kugawanyika kwa ‘petty issues' (mambo madogo madogo).
Yaani huyu Lukuvi kwa kuita DOWANS ni suala dogo...............................inanithibitishia ya kuwa amelewa madaraka.................Haiwezekani bilioni 94 zikawa "petty issue".................................the man must be living in "wonderland"....................
 
mgawanyiko CCM upo na haukwepeki..... it is a time bomb.... hata mwalimu nyerere alishauona na alishauri sisiem imegeke ili iwe na vyama viwili....enzi za G 55..... mrema akapewa dili akakurupuka halafu ikashindikana..... sasa imebakia muda mfupi tu utaniambia
 
"Dowan ni petty issue" I like that one. Si Lukuvi kama ana haya mabillioni atulipie basi kama ni petty issue??
 
Siku hizi Lukuvu Ticha wa primary anabonga English.

Suala la Mabillioni ya fedha kuilipa Dowans analiita "Petty Issue "

Yale yale ya Vijisenti!!!

Lukuvi anaujasiri wa kuita suala la Dowans Petty Issue??

Kweli CCM wamelewa Fedha za wizi na madaraka
 
Matatizo yapo Duniani ni kweli lakini sio mgawo wa umeme usiokuwa na mwisho,wanafunzi kukaa chini wakati waziri anatembelea gari la milioni 150,mishahara kiduchu na hailipwi kwa wakati,barabara mbovu na nyingi zinajengwa chini ya kiwango,vituo vya afya dawa hamna..,wamelewa madaraka kiasi kwamba wanashindwa kuona ukweli kwamba wamefeli kwa kiasi gani...!
 
‘CCM kinapitia wakati mgumu’
Saturday, 29 January 2011 08:33

Elias Msuya na Fredy Azzah

KIKIWA kinatimiza miaka 34 tangu kuzaliwa kwake Februari 5, 1977, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimelezewa kuwa, ingawa kimeendelea kushinda nafasi ya urais nchini, kinakabiliwa na wakati mgumu.

Wakizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, wabunge wa CCM walisema chama hicho hakiwezi kufa kwa sasa, lakini kinapitia tu wakati mgumu kama ilivyo kwa vyama vingine duniani.

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), William Lukuvi, alisema kwa kipindi cha miaka 34 ambacho CCM imekuwa madarakani, kimefanikiwa kufikia malengo yake hasa kwa kushinda chaguzi zote.


“Chama chochote kile duniani, malengo yake ni kushika dola. Kwa kipindi chote CCM tumefanikiwa kushika dola. Hata kwenye michezo, kama timu inashuka daraja mwenye timu huivunja,” alisema Lukuvi.

“Chama cha siasa ni taasisi endelevu, sio kwamba tumeongoza kwa maziwa na asali. Tunapitia kwenye milima, misitu na vichaka.

Ni jukumu letu kujitambua ili tuendelee kushika dola,” alisema. Kuhusu suala la Dowans ambalo limeonekana kukigawa chama hicho kabla ya wabunge wake kukutana na kuweka msimamo wa pamoja, Lukuvi alisema hilo haliwezi kukigawa chama.“Chama hakiwezi kugawanyika kwa ‘petty issues’ (mambo madogo madogo).

Chama kupitia mwenyekiti wetu alishasema jambo hilo sio kubwa. Ni uhuru wa maoni tu, kama ni mawaziri kupingana watakuwa wamevunja kanuni zao, sio chama,” alisema.

Naye Mbunge wa Uzini, Muhammed Seif Khatib, alisema sio kwamba CCM imepoteza mwelekeo, bali kinakwenda kulingana wakati ulivyo.

“Sioni kama chama kimepoteza mwelekeo, kinakwenda kulingana na wakati, dunia imebadilika, mahitaji yameongezeka, vionjo vimeongezeka kwa hiyo chama kinakumbana na mazingira ya wakati huu,” alisema. Alikitetea chama hicho kuwa, hakiwezi kuleta pepo duniani na kwamba, matatizo yapo duniani kote sio Tanzania pekee.

Kuhusu suala la Dowans, Khatibu alisema kilichotokea ni uhuru wa maoni sio kugawanyika kwa chama. Naye Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Stella Manyanya, alisema kwa kipindi cha miaka 34, chama hicho kimefanya mambo mengi mazuri ambayo yameifikisha nchi hapa ilipo, na bado kina uwezo wa kuongoza miaka mingi ijayo.

Hata hivyo, Manyanya alisema changamoto anayaoiona ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi, ni suala la mawasiliano.

Hiyo yenye nyekundu inawezekana ni kauli ya kijinga kabisa. Kushinda uchaguzi halafu kiwe nini? Yaani chama kikae tu kula na kuiba pesa za watanzania na sio kufanya kazi kuifanya Tanzania iwe nzuri zaidi? ushindi maana yake nini kwa CCM? NI bora kama watu hawawezi kuongea wakae kimya, kuliko kuongea pumba!!
 
alibaba...Rostam Aziz

and

forty thieves....William Lukuvi.., Nazir Karamagi....
 
Du km Petty Issue walipe basi! Dowans hizo 94bn watakiona cha moto kinachompata Mubarak huko Misri au Tunis, Tunisia Baraza lote halitakiwi
 
Hivi hizi kauli za wana CCM ni dharau kwa Watanzania ama
Chenge = Visent
Kombani= nilkuwa napima Upepo
Warema = Hayo ni mawazo/maneno yangu binafsi
Lukuvi= Petty Issue
Mary = Askofu wavue majoho

ni balaa kabisa
 
Back
Top Bottom