Nucky Thompson
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 1,817
- 4,058
Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh. Wiliam Lukuvi ametoa siku 30 kwa mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro kuhakikisha anatoa hati zaidi ya 100 kwa wamiliki wa viwanja na nyumba zilizocheleweshwa bila sababu huku akitoa siku sita kuhakikisha anatoa hati 60 za wakazi wa mtaa wa Bigwa barabarani waliokamilisha malipo yao katika mpango wa urasimishaji makazi.