Lukuvi amfagilia Mnyika

Lukuvi amfagilia Mnyika

Mnyika ana uelewa mpana sana kuhusu sharia,na dhani Lukuvi ameliona hilo
 
hawa magamba japo wanatumia mabavu ila wataeleweka tu BRAVO JJ mnyika
 
JJ Mnyika ni makini hakuna mfano anakonga nyoyo za wengi
 
Huyu huyu lukuvi tunaemjua au mwingine!? lazima kuna mtu ameiba password ya ubongo wake :A S-confused1:
 
hali iliyowashitua wengi, mnadhimu wa bunge mhe. Lukuvi leo ametumia zaidi ya dakika tatu akimusifia kijana machachali aliyewahi kuweka wazi kuwa rais wa nchi hii ni dhaifu na baada ya kutafakali kwa miezi nenda rudi lukuvi amegundua john john mnyika ni kijana makini na anampenda sana pia amempongeza Freeman Mbowe kwa kumteua kuja naye ikulu..

mods naomba msiunganishe na thread nyingine
Ni mkweli; anataka kung"oa kucha nini! Gamba linasifu jembe? ???
 
Ndiye pia aliyefichua kuwa JK ni dhaifu! Anastahili pongezi kwa kuwa na msimamo na kutokuwa mwoga wala mnafiki!
 
Mnyika ana busara,lkn msomi Lisu ana jazba za kijinagakijinga,wakati mungine naona akili yake haijakaa sawa.
 
Na bado, atamsifia Chiku Abwao siku za karibuni tuu. Huo unaitwa mwendo mdundo.
 
Kama lukuvi amekubali kuwa huyu dogo ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja,maana yake anakubaliana na hoja ya Mh.Mnyika kuwa Baba ridhiwan ni dhaifu!?
 
Lukuvi amepata ufahamu.

Sio kirahisi hivyo mkuu, kama ulimwangalia mweshimiwa Lukuvi wakati anamsifia Mh. Mnyika na unauelewa wa kumsoma mtu kisaikolojia, utagundua kuwa ile ilikuwa ni self diffence against Mh. Lisu. Kwani wakati alikuwa anazungumza wasiwasi ulimtawala huku akizani Mh. Lisu ataomba muongozo wa spiker.
 
unasumbuliwa na wivu wa kike

wabheja nkoyi bujash kulikuwa na thread nyingine kama hii tena yenye maelezo yanayojitosheleza hakukuwa na sababu ya kumpangia mod eti asiiunganishe na thread nyingine hongera mod ulifanya kazi yako bila kupangiwa
 
Last edited by a moderator:
Mbunge wangu mnyika,naeshmu kazi yako kwa jinsi unavyojituma. Tambua sina maana mbaya pale ninapokwambia kuwa mwangalifu na pongezi unazopewa na baadhi ya watu ambao binafsi naamini ni adui zetu wa kisiasa.
Nichokuomba zichukulie za kawaida katika kukufanikisha kutekeleza majukumu yako ya kumtumikia mtanzania. Zisijekukufanya ukavimba kichwa na kujiona wewe ndiye wewe mwishowe ukashindwa kuelewana na wenzio ktk kuendeleza chama.
Tambua siku zote hakuna adui yako yeyote atakae kuombe mazuri ingali ya kwamba kufanya ivyo kwake pazidi kuwaka moto.
Mfano mzuri kilicho mtokea zito,kwani walianza kama wanavyoanza kwako. Wakitokahapo wanaanza kukutunuku vinafasi fulanifulani ili unogewe na vimalupulupu,kisha wataanza kukuita private kama ilivyo mtokea zito. Ila nakupongeza kwa kazi nzuri unayoifanya katika kukijenga chama.
 
Huyu mnyika ni kijana asiependa makuu, ana busara kuzidi hata baadhi ya wazee waliopo chadema, ni mvumilivu. Kuvumilia mambo yanayofanywa na bavicha pale chadema inahitaji uikane nafsi yako.
 
inahitaji uikane nafsi yako.[/QUOTE]

ki vp? Binafsi nimetoa ushauri kwavile namkubali. Ila nimemtahadharisha na vishoka na majangili waliopo ccm,kwani lengo lao kubwa kuwagawa viongozi na wanachama ili wafanikiwe malengo yao ya kukiua chadema
 
Back
Top Bottom