Arafat
JF-Expert Member
- Nov 17, 2009
- 2,581
- 758
"...Jairo ambaye yuko chini yake, analazimika kwenda likizo kuanzia juzi ili kupisha uchunguzi wa awali ambao unalenga kubaini iwapo ametenda kosa la kinidhamu kwa mujibu wa sheria zinazoongoza Utumishi wa Mmma.(Philemon Luhanjo kwa mujibu wa nukuu ya Gazeti la Mwananchni)
Kwa mijibu wa hii kauli ya Luhanjo uchunguzi unaofanyika hauna haja na ni matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi kwa sababu makosa aliyofanya Jairo yameshapindishwa na si ya rushwa tena na hamna uchunguzi wowote wa rushwa dhidi yake, hivyo kamsafisha na tuhuma za rushwa, wanachofanya sasa ni kumpaka mafuta tu!
Kwa mujibu wa Sheria Na.6 ya 2001 (Public Finance Act) hakuna kosa watakalo mkumba nalo Katibu Mkuu wa Wizara maana yeye ndio Accounting officer wa Wizara na fedha yote ya serikali katika wizara husika ipo chini yake, yeye ndiye mwenye VOTE ya ku-control fedha hizo na matumizi yake hivyo matumizi yeyoye atakayofanya ili mradi yawe na lisiti halali ni sahihi na haki; swali lililo baki hapo na wanalotaka kuja nalo ni kama hayo matumizi si halali au la! Ni kazi rahisi sana, kuwa na lisiti za soda na hotel walizolipa zenye gharama sawa na matumizi yaliyofanyika sidhani kama inawashinda hawa watu ambao hawana hata chembe ya aibu katika nyuso zao.
View attachment 34348
Wanacho angalia watu wa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu ni kile kinachoitwa "General accepted accounting practice" yaani kama matumizi yaliyofanyika yakitunzwa vyema ki-hasibu na gharama zake ni bei halali ya soko huo ndio utakao kuwa mwisho wao, swali kwanini hawaku institute uchunguzi wa tuhuma ya rushwa? badala yake Luhanjo anaenda mbali hadi kusema kosa la kinidhamu! Kusema kosa la kinidhamu tayari ni kumsafisa na makosa ya kijinai ambayo ni fraud na corruption.
Ushauri wangu kwa serikali, badala ya kupoteza fedha zaidi kumpaka mafuta Jairo, rais atangaze kuwa Jairo hana kosa na kuwa anampangia kazi nyinge maana haina jinsi yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu na Majeshi yote bado yana mtii na kumpigia Mizinga hasiwe na shaka apunguze matumizi yasiyo lazima katika uchunguzi ambao tayari wameshau elekeza katika dimbwi, awe wazi na atangaze maamuzi yake juu ya Jairo, Pia Pinda kwa mujibu wa maelezo yake bunge alisema Jairo ni wakufukuza tu, ila anamsubiri rais sasa asimamie maneno yake ajiuzulu kama kweli hana unafki katika maneno yake na matendo yake akae pembeni maana ukitofautiana mtazamo na mawazo kiasi cha kuoneka kama hivi ni bora kupisha hili husiwe sehemu ya usafi au uchafu huo unao upinga.