Martin Maranja Masese
Member
- Apr 24, 2011
- 29
- 542
Luhaga Mpina leo amenukuliwa na vyombo vya habari anasema January Makamba ni mhujumu uchumi anayepaswa kuwa gerezani siyo Ofisi ya wizara ya nishati. Binafsi sina tatizo na hilo alilosema. Lakini Luhaga Mpina wewe hupaswi kuwa mbunge wa Kisesa. Hukuchaguliwa uchaguzi wa 2020, mgombea wa CHADEMA, Francis Kishabi alitangazwa mshindi usiku, asubuhi ukatangazwa mshindi wewe. UJAMBAZI!
Nhundu Francis kishabi, aligombea udiwani kata Mwandoya, Jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, Simiyu na pia aligombea ubunge jimbo la kisesa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisesa kwa tiketi ya CHADEMA, viti vyote viwili alishinda.. Matokeo ya udiwani yalibandikwa kabisa Francis Kishabi mshindi baadae kidogo yakachanwa kwa madai matokeo ya udiwani na ubunge yote yanatolewa Mwanhuzi
Kesho yake kilichofuata..
Hata udiwani aliokuwa ametangazwa kwamba ameshinda wakasema kashindwa, ubunge kapokwa akapewa Luhaga Mpina, Magufuli akampa uwaziri wa Mifugo na Uvuvi (alitueleza sababu akisema aliamua kuchagua mtu kichaa-kichaa kama yeye amsaidie). Yote haya yanafanyika kwenye mkoa ambao RC ni mtakatifu Anthony Mtaka.. Hakuweza kuruhusu demokrasia kushamiri
Kilichofuata!
Nhundu Francis Kishabi alikuwa anakabiliwa na shauri la Arson 1/2018 lenye mashtaka matano (5) ndani yake likiwepo shtaka la kuchoma kituo cha polisi Mwandoya, katika jimbo la Kisesa, Meatu, Simiyu, akihusishwa na wapiga kura wake wapatao 24. kati ya mwaka 2015—2020 Francis Kishabi alikuwa diwani wa kata ya Mwandoya (Chadema) pia Mwenyekiti wa Chadema Meatu.
Shauri hilo liliendeshwa kwa miaka mitatu, Mwishoni kabisa wa shauri hilo, hakimu aliyeanza na shauri hilo tangu mwanzo, akapandishwa cheo na kuhamishwa mkoa mwingine kikazi na jalada likapokelewa hakimu mwingine (mgeni) aliyepokea mwishoni wakati wa kufunga utetezi kwa Upande wa mashtaka.
February 2021 Francis Kishabi akahukumiwa miaka 3 gerezani pamoja na wenzake. Kishabi alikata Rufaa. Na 30/7/2021 Mahakama kuu kanda ya Shinyanga ikamuachia huru NHUNDU FRANCIS KISHABI na wenzake wanne waliokuwa wamehukumiwa miaka 3 gerezani, Feb 2021 kwa tuhuma za kuchoma moto Kituo cha polisi Mwandoya-Simiyu.. 2015/2020 Kishabi alikuwa diwani kata ya Mwandoya, pia mwenyekiti wa Chadema-Meatu, mgombea ubunge Kisesa 2020.
Luhaga Mpina sasa ni mbunge wa jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, mkoa wa Simiyu, leo amenukuliwa anasema January Makamba anastahili kuwa gerezani kwa Makosa ya uhujumu uchumi (Binafsi sina tatizo na hilo), lakini swali langu ni, Je, Luhaga Mpina anastahili kuwa bungeni? Alishinda ubunge? Nani alimchagua? Misimamizi wa uchaguzi, Meatu Fabian Manoza alipora uchaguzi kwa niaba ya CCM.
#MMM, Martin Maranja Masese
Nhundu Francis kishabi, aligombea udiwani kata Mwandoya, Jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, Simiyu na pia aligombea ubunge jimbo la kisesa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisesa kwa tiketi ya CHADEMA, viti vyote viwili alishinda.. Matokeo ya udiwani yalibandikwa kabisa Francis Kishabi mshindi baadae kidogo yakachanwa kwa madai matokeo ya udiwani na ubunge yote yanatolewa Mwanhuzi
Kesho yake kilichofuata..
Hata udiwani aliokuwa ametangazwa kwamba ameshinda wakasema kashindwa, ubunge kapokwa akapewa Luhaga Mpina, Magufuli akampa uwaziri wa Mifugo na Uvuvi (alitueleza sababu akisema aliamua kuchagua mtu kichaa-kichaa kama yeye amsaidie). Yote haya yanafanyika kwenye mkoa ambao RC ni mtakatifu Anthony Mtaka.. Hakuweza kuruhusu demokrasia kushamiri
Kilichofuata!
Nhundu Francis Kishabi alikuwa anakabiliwa na shauri la Arson 1/2018 lenye mashtaka matano (5) ndani yake likiwepo shtaka la kuchoma kituo cha polisi Mwandoya, katika jimbo la Kisesa, Meatu, Simiyu, akihusishwa na wapiga kura wake wapatao 24. kati ya mwaka 2015—2020 Francis Kishabi alikuwa diwani wa kata ya Mwandoya (Chadema) pia Mwenyekiti wa Chadema Meatu.
Shauri hilo liliendeshwa kwa miaka mitatu, Mwishoni kabisa wa shauri hilo, hakimu aliyeanza na shauri hilo tangu mwanzo, akapandishwa cheo na kuhamishwa mkoa mwingine kikazi na jalada likapokelewa hakimu mwingine (mgeni) aliyepokea mwishoni wakati wa kufunga utetezi kwa Upande wa mashtaka.
February 2021 Francis Kishabi akahukumiwa miaka 3 gerezani pamoja na wenzake. Kishabi alikata Rufaa. Na 30/7/2021 Mahakama kuu kanda ya Shinyanga ikamuachia huru NHUNDU FRANCIS KISHABI na wenzake wanne waliokuwa wamehukumiwa miaka 3 gerezani, Feb 2021 kwa tuhuma za kuchoma moto Kituo cha polisi Mwandoya-Simiyu.. 2015/2020 Kishabi alikuwa diwani kata ya Mwandoya, pia mwenyekiti wa Chadema-Meatu, mgombea ubunge Kisesa 2020.
Luhaga Mpina sasa ni mbunge wa jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, mkoa wa Simiyu, leo amenukuliwa anasema January Makamba anastahili kuwa gerezani kwa Makosa ya uhujumu uchumi (Binafsi sina tatizo na hilo), lakini swali langu ni, Je, Luhaga Mpina anastahili kuwa bungeni? Alishinda ubunge? Nani alimchagua? Misimamizi wa uchaguzi, Meatu Fabian Manoza alipora uchaguzi kwa niaba ya CCM.
#MMM, Martin Maranja Masese