Luhaga Mpina ndiye Waziri Mkuu ajaye

Luhaga Mpina ndiye Waziri Mkuu ajaye

Mhe. Luhaga Joelson Mpina MB, anafaa kuchukuwa nafasi ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa MB na Waziri Mkuu wa JMT; kwenye cabinet ijayo 2025.

Mhe. Mpina amedhihirisha kiwango cha juu cha uzalendo kwa taifa, ujasiri, ari, nidhamu ya kutolea mfano, weledi, kazi za matokeo makubwa nk.

Anafaa kuisimamisha serikali ya 2025 - 2035 kwenye nafasi ya utendaji ya PM.


Nani alikuambia sifa ya kuwa waziri mkuu ni uzalendo peke yake?
 
Mpina sio mzalendo. Uliza wavuvi wakuambie ubaya wake. Mpina ni kundi moja na Sabaya, Makonda, aliyekuwa DPP Biswalo, Musiba na makatili wengine enzi za JPM. Ila kama CHADEMA wanampenda atawafaa kuwa mgombea urais 2025.
Enzi za Mh. Mpina akiwa Waziri wa Masamaki, wale sangara wakubwa walianza kurudi. Samaki wakashuka bei kwa wingi wao. Leo tumerudi miaka ya 2005 - 2015 kabla yake. Nipo tayari kwa mjadala.
 
Huyu huyu anayekisame chama chetu hadharani?
AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote.
(3) Nitajitolea nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika
 
AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote.
(3) Nitajitolea nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika
Kiukweli hizi ni ahadi za J. K. Nyerere na Edward M. Sokoine
 
Yupo vizuri ila ajitokeze kujibu tuhuma za kupora ekari 1000 za wananchi Morogoro
suala la ardhi liko kisheria kama kuna shida ya kisheria lishaamuliwa mahakamani...ukiona hivyo hakuna mgogoro ila kuna walamba asali wanataka kuhamisha mjadala
 
Mara mseme Rais wa 2030 mara PM yaani mpaka hapo imekula kwake maana hakuna Rais au PM ambae amewahi tabiliwa na watu wakapatia.
 
Mhe. Luhaga Joelson Mpina MB, anafaa kuchukuwa nafasi ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa MB na Waziri Mkuu wa JMT; kwenye cabinet ijayo 2025.

Mhe. Mpina amedhihirisha kiwango cha juu cha uzalendo kwa taifa, ujasiri, ari, nidhamu ya kutolea mfano, weledi, kazi za matokeo makubwa nk.

Anafaa kuisimamisha serikali ya 2025 - 2035 kwenye nafasi ya utendaji ya PM.


Takataka
 
Mara mseme Rais wa 2030 mara PM yaani mpaka hapo imekula kwake maana hakuna Rais au PM ambae amewahi tabiliwa na watu wakapatia.
Makonda alimtabiria Samia kuwa rais; kwenye Bunge la Katiba.

Sheikh Yaya alitutabiria kuwa taifa litapata kiongozi shupavu lkn atayedumu kwa ngwe moja tu ya awamu yake na utabiri umetimia.
 
Back
Top Bottom