Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 123,250
- 98,243
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mara kimesema kinaandaa utaratibu wa kumuita katika vikao na kumhoji aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola ili awaeleze sababu zilizopelekea kuaibisha mkoa huo na Rais John Magufuli ambaye alimuamini na kumpatia nafasi ya uwaziri ili atumikie Taifa.
Hayo yamebainishwa jana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara, Samuel Kiboye wakati akieleza namna ambavyo chama hicho kinakasirishwa na viongozi wanaopewa nafasi ya kumsaidia Rais katika wizara mbalimbali lakini mwisho wa siku wanaliingiza Taifa katika mikataba mibovu.
Ama kweli usitukane mamba kabla hujavuka mto.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hayo yamebainishwa jana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara, Samuel Kiboye wakati akieleza namna ambavyo chama hicho kinakasirishwa na viongozi wanaopewa nafasi ya kumsaidia Rais katika wizara mbalimbali lakini mwisho wa siku wanaliingiza Taifa katika mikataba mibovu.
Ama kweli usitukane mamba kabla hujavuka mto.
Sent using Jamii Forums mobile app