Kwa matokeo ya Uchaguzi mkuu uliopita, ikiwa CCM wanalia , Lowassa anacheka?. CCM inapopata Wabunge zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wote wewe unajiita mpinzani bado unashangilia? Malengo ya Lowassa na upinzani yalikuwa ndo hayo? Badala ya kujitathmini kwa nini wameshindwa wanabweteka. Unakuwaje na amani unapolipoteza jiji kama la Mwanza? Basi nimeamini Upinzani haujajiandaa kuongoza nchi na ndiyo sababu ilifikia hatua kusubiri CCM iwakate watu ndo wawachukue. Halafu katika akili ya kawaida inakuwaje mwanafunzi aliyefeli kabisa mtihani katika shule fulani akahamia shuleni kwako aonekana ndiye mwenye akili kuliko wanafunzi wote wa shule yako, halafu unakubali kwenda kumpambanisha na mwanafunzi aliyefaulu sana katika Shule ile ambaye huyo mwanafunzi wako alishindwa? Unatarajia nini?. Endapo Vyama vya Upinzani watakubaliana kuungana, tutaona upinzani wa kweli Tanzania. La sivyo mtaishia kususia Uwanja wa Taifa na kuandamana tu!!