Lowassa: Sina mpango wa kutangaza nia

Lowassa: Sina mpango wa kutangaza nia

mwekundu

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2013
Posts
22,477
Reaction score
21,040
Lowassa: Sina mpango wa kutangaza nia

Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema hana mpango wa kutangaza nia ya kugombea urais kwa sasa, bali anapenda kushirikiana na waumini na wananchi katika shughuli zao za kimaendeleo.

Hayo aliyasema katika uzinduzi wa helikopta maalumu ya Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dar es Salaam jana.

Lowassa alisema alipopata mwaliko huo alifurahi kwa heshima aliyopewa, lakini alikutana na swali gumu linalohusiana na urais.

"Nilipofika hapa, kuna mmoja wa rafiki zangu akaniuliza, umekuja kutangaza nia? Nikamwambia sikuja kutangaza nia hapa...Sina mpango huo kwa sasa. Nimekuja kusali na kushiriki kanisani kwa ajili ya kuinua jina la Bwana," alisema Lowassa.

Alisema taifa linahitaji viongozi wenye maono ambao ndiyo wanaoweza kulivusha na kulipeleka mbele.

Akihutubia maelfu ya waumini kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, alisema viongozi wenye maono ndiyo mfano unaotakiwa kufuatwa kwa kuwa utaleta mabadiliko chanya.

"Hatuhitaji viongozi wenye kusimamia na kutunza hesabu. Tunahitaji viongozi wenye maono na kuhakikisha maono hayo yanatimia. Kanisa lenu lina bahati kwa kuwa lina kiongozi mwenye maono na anayeweza kuyasimamia," alisema.

Akielezea ununuzi wa helikopta hiyo, alisema amefurahishwa na hatua hiyo ambayo ni ya kihistoria nchini. Awali, Askofu Gwajima alisema anaumizwa na baadhi ya wanasiasa wanaoshindwa kusimamia uamuzi wao, huku akiwaita ‘ndumilakuwili.'

"Nawajua sana wanasiasa, wapo ambao wakikwambia umepata, usipumzike, tafuta zaidi kwa kuwa hawamaanishi hivyo. Lakini Lowassa akimwambia umepata, nenda kampumzike," alisema.

Chanzo: mwananchi.co.tz
 
Yes muda bado ukifika atatangaza na ataichukua nchi hii kama rais mwaka 2016.
 
Lowasa anainua jina la Bwana?..........Glory to God.
 
Lowasa na Gwajima ni maswahiba na wanashirikiana kisiasa. Lowasa anamtumia Gwajima kujijenga kisiasa kupitia kanisa lake. Soma taarifa ya hapa chini.

Edward Lowassa akutana na Maaskofu wa Tabora na Kagera na kufanya nao mazungumzo ya Faragha


Wadau, macho na masikio ya Watanzania wengi kwa siku ya leo yalikuwa mjini Dodoma ambapo shauku kubwa ilikuwa ni kujua matokeo ya kura zilizopigwa na wabunge wa Bunge Maalum la Katiba kupitisha Ibara za Rasimu Inayopendekezwa. Hakika ni siku ya kihistoria ambapo kila mbunge alikuwa na shauku kubwa ya kuwepo Bungeni kushuhudia moja kwa moja historia mpya ikiandikwa.




Pamoja na umuhimu huo, Mbunge wa Monduli ambaye pia ni Waziri Mkuu aliyejiuzulu kutokana na kashfa ya ufisadi, EDWARD LOWASA aliamua kukacha bunge hilo na kuamua kwenda mikoa ya Tabora na Kagera kuonana na Maaskofu kwa lengo la kupalilia njia yake ya kwenda Magogoni. Safari ya Lowasa kuonana na Maaskofu katika mikoa hiyo ilianzia Tabora ambapo aliwasili kwa ndege ya kukodi 5H- Lux akiwa ameambatana na Mchungaji Gwajima ambaye hivi karibuni amekumbwa na kashfa ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wa mtu, muumini wa kanisa lake lililopo Kawe, Dar es Salaam na muimbaji wa Muziki wa Injili, FLORA MBASHA.




Baada ya kuwasili Tabora, Lowasa na Gwajima walienda moja kwa moja nyumbani kwa Askofu wa Kanisa Katoliki, Mhashamu PAUL Ruzoka ambako waliongea kwa muda wa zaidi ya saa moja. Katika kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na Askofu Mteule Asante Mungu walijadili masuala kadhaa ambayo yalilenga kuhuisha mahusiano baina ya mwanasiasa huyo na viongozi wa kiroho hasa baada ya Harambee alizokuwa anatumia kujijenga kisiasa kudhibitiwa na Kamati Kuu ya CCM. Mbali na hayo, Lowasa na viongozi hao wa kidini walijadili hali iliyojitokeza bungeni ambapo Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Sammuel Sitta alisoma waraka ambao uliandikwa na viongozi wa kiroho na ambao ulikuwa unaingilia mamlaka ya Bunge. Lowasa kwa upande wake hakurudhika na msimamo wa Sitta wa kuwasema vibaya Maaskofu walioandika waraka huo na hivyo alitumia kikao hicho kumchonganisha kwa viongozi wa kiroho.




Baada ya Tabora, Lowasa na Gwajima walielekea Kagera ambako wamekutana na Askofu Methodius Kilaini. Mazungumzo ya Kagera yalifanana na yale ya Tabora. Lowasa ameomba msaada wa maaskofu hao kuungana na harakati zake za kujenga ukubalifu na imani kwa Watanzania ili safari yake ya kwenda Ikulu isiwe na mikingamo. Ameahidi kuwapa kiasi cha fedha ambacho haikufahamika kiasi chake ambazo zitatumika kumjenga mwanasiasa huyo kisiasa miongoni mwa waamini wa makanisa yanayoongozwa na maaskofu hao na kwamba harakati hizo zitakuwa ni za nchi nzima.




Wadau, huyu ndiye Edward Lowasa ambaye anajaribu kutumia kila fursa inayojitokeza kujijenga kisiasa. Kama kawaida yake, anaweka mbele matumizi ya fedha ili tu ainekane anakubalika miongoni mwa matabaka mbalimbali ya jamii ya Kitanzania. Kamera ya Chabruma itaendelea kummulika na kila kitu kitakuwa wazi.
 
Mie nadhani hana nia ya kutangaza kuwa hatogombea...ila kama ni ukulu wa kaya nia anayo na ndo mana kila siku anatumia mbinu kadha wa kadha kupata wafuasi. Lowasa asivyogombea nakuhakikishia kuwa UKAWA na CDM wata chukua nchi.
 
Last edited by a moderator:
Lowasa fisadi,au mmesahau kamati ya mwakyembe
 
Mie nadhani hana nia ya kutangaza kuwa hatogombea...ila kama ni ukulu wa kaya nia anayo na ndo mana kila siku anatumia mbinu kadha wa kadha kupata wafuasi. Lowasa asivyogombea nakuhakikishia kuwa UKAWA na CDM wata chukua nchi.
CCM bila ya Lowasa ushindi daima
 
Ni kweli tunahitaji viongozi wenye maono ya kujua ni fedha gani zipo kihasarahasara serikalini ili ziundiwe dili
CCM oyeeeee!!
 
mwenyewe anajua maovu aliyoyafanya kwenye ufisadi wa RICHMOND akitangaza nia atapigwa mawe bure
 
Ni kweli tunahitaji viongozi wenye maono ya kujua ni fedha gani zipo kihasarahasara serikalini ili ziundiwe dili
CCM oyeeeee!!
Endelea kuijazia damu maiti ccm
 
Back
Top Bottom