Nyetk
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 1,648
- 1,701
na uzee wote ule?halafu afya yake yenyewe inaonesha he's weak kama swahiba wake alomsifia
Nyani haoni kundule mkuu.
na uzee wote ule?halafu afya yake yenyewe inaonesha he's weak kama swahiba wake alomsifia
Wameuza mbuga yote, kwanini asiwapige na changa la macho? na anjua hao ng'ombe ni pint ya faida ya wizi uliofanyika. hii wala siyo siasa ni mazingaombwe kwa lowasa kumpa sifa huyo mwizi mwenzake. labda sasa anabidi ajikombe anajua bill za afya yake zinaweza kumzidi kimo na akafilisika. maana kwenda kutibiwa nje siyo kama kwenda mikocheni hospital. lakini watanzania tumeshawajua zao wao waungane sana na sio masikini tunashikana taratibu mpaka kieleweke.
well, utuambie wewe kinachomuungizia nasi tujue! halafu mimi nimesema wote yeye na kikwete wezi, weye wamtetea lowasa wapigwa posho nini? maana kushadadia mwanamme mwenzako anapakwa ujue kuna jambo! lahasha...! kama swahiba yako tupe habari tujue maana pengine wapewa raha.hv we unaandika unachokijua au?unajua shivacom peke yake inamuingizia lowassa
WAZIRI MUU MTAAFU MWANAUME NDANI YA CCM LOWASA AMEMPONGEZA KIKWETE KWA KUWAJALI WAFUGAJI NA KUWA NI MSIKIVU SAANA.JUZI TU KIKWETE ALIMSAFISHA CHENGE NA KUSEMA HAKUNA UFISADI ULIOFANYIKA KWENYE CHENJI YA RADA
SASA NAPE UTAHEMEA WAPI ULIOWAPA SIKU 90 WANKULA MEZA MOJA NA MWENYEKITI WAKO SASA ELEWA CCM SI CHAMA CHA SIASA NI GENGE LA WAHUNI UTAIPATA FRESH MBWIGA RUDI CCJ MAPEMA MAANA HUKU MSUKUMA HUKU MMASAI SHINGO LAZIMA WAITOE HIYO![]()
Kwanza kabisa nilishtuka niliposoma hotuba ya Rais akikabidhi NGombe Longido na sasa Monduli.
Pamoja na kumheshimu sana maze Lowassa lakini sasa naona nae anapotoka.
Utaratibu wote uliopelekea WAMASAI kupewa hao NGOMBE haukufikiriwa vizuri.
Rais alitakuwa kutafuta majibu ya haya maswali kwanza Kabila ya Hilo zoezi kuanza.
Kwanini NGOMBE walikuwa? Jibu ni ukame. Je Rais ana uhakika gani kuwa hao Ngome wa mbegu nao hawatakufa kwa msimu ujao wa ukame?
Nashauri, washauri na wasaidizi aw Rais wamwaambie kuwa swala sio kutoa NGOMBE tu kisisa na kuondoka.
Lazima watafuta namna ya kufanya ili hao NGOMBE walionunuliwa kwa kodi zetu wasife.
USHAURI.
Wafungue centers huko umasaini yaan I small ranch, Ngome hao wa mbegu wawekwe na kutunzwa na serikali ya vijiji au Wilaya chini ya wizara ili watumike Kuzalisha mbegu in a sustainable manner.
NGOMBE wengi walikufa kwa sababu ya Kukosa maji, Wakati aw ukame.
Rais angeelekeza nguvu kubwa kwenye kuchimba mabwawa ya kuvuna maji ya mvua, ambao yatatumika kwa awamu tena kwa usimamizi wa serikali.
Mh. Lowassa, naomba kupingana na wewe kuwa huo utaratibu wenu na JK sio aw kudumu ni aw kisiasa tu!
Tunaomba tuambiwa results ya hao NGOMBE baada ya miaka Miwili ijayo.
Halo nimesema waanzishe centers za kutunza hao Ngombe w a mbegu. Maana ukame ukija watakufa. Na itakuwa hasara sio kwa wamasai tu na walipa kodi wotePingana na Lowassa na hiyo ni hiari yako. Rais ametoa mifugo na wakati huo huo kutoa fedha za kukarabati mabwawa ili yaweze kutunza majinyatakayotumika wakati wa ukame. Sisi wenye akili tunajua kwamba kiu na ukame ndiyo ulioua mifugo mwaka ule. Ulitaka afanyeje kwa wananchi hawa ambao walibaki hawana kitu? Je, wangejikimu vipi katika kipindi hiki ambacho sulushisho la kudumu la tatizo hili linatafutwa?
Lakini huu unafiki wa Lowassa unakera. Amekuwa mstari wa mbele kumshutumu, kumbeza na kumhujumu Rais halafu leo anajifanya kumsifia. Ni huyu huyu aliyenukuliwa huko nyuma akisema kwamba Rais huyu ni mwoga wa kutenda na kwamba serikali yake ina kigugumizi cha maamuzi. Kweli wanafiki hawatauona ufalme wa Mungu.