Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Ocampo four

JF Senior Expert Member
Joined
Feb 28, 2014
Posts
5,789
Reaction score
2,159
Waziri Mkuu mstafu na mgombea wa umoja wa Ukawa Ndg. Edward Lowassa katema cheche na kusema Ukawa wakipewa ushindi, ndani ya siku 100 ataziba mianya yote ya rushwa, ufisadi akianza na bandarini ambapo zaidi ya Billioni 21 upotea kwa siku..

Lowassa kasema kuwa serikali ya Ukawa itakuwa na wajibu mmoja tu, ambao ni kutoa huduma iliyobora kwa wananchi na kwa wakati. Hiyo ndio serikali ninayotaka kuiona, na hayo ndio mabadiliko wanayoyataka wananchi. Hili litaendana na kuziba mianya ya rushwa, na nawahidi ndani ya siku 100 mianya hiyo itazibwa.... Alisema

Kwa hii hatua na kauli ya Lowassa ni wazi wananchi wanaelekea kufaidi matunda ya nchi yao, na sio kikundi kidogo cha watu.. Hatua kama hizi zilifanikiwa sana Singapore, Malaysia, Taiwan na Korea Kusini.. Na hata Rwanda baada ya Kagame kuingia ndani ya siku chache alifanikiwa kuthibiti rushwa, ufisadi na aina zote za dhuluma...

Mytake: Nafurahi kuona serikali ya Ukawa kutupeleka katika speed ya maendeleo kama Singapore, Korea Kusini au Malysia....
 

Attachments

  • 1443331642945.jpg
    1443331642945.jpg
    42.9 KB · Views: 1,594
Elewa ujumbe. Atadhibiti maana yake zote zitakuwa zake. Hatakubali deal zichukuliwe na wengine.

Mafidasi ndani ya CCM mkimsikia tu Lowassa mnapata uharo..... Ataanza na wale jamaa wa Home Shopping Centre ambapo Prince na Bi mdogo wana pct pale
 
Hivi aliweza kuongea yote hayo au umeongeza na ya kwako?
 
Ha ha ha kituko cha mwaka shetani kusema ataanza kumuabudu mungu

Mafisadi kama Home shopping centre, Escrow, Richmond, Meremeta, Kagoda, zile Bl 8 za TCRA, waanze kukimbia mapema. Kiama kimefika, bado siku 27 tu
 
Mafisadi kama Home shopping centre, Escrow, Richmond, Meremeta, Kagoda, zile Bl 8 za TCRA, waanze kukimbia mapema. Kiama kimefika, bado siku 27 tu

Ni upofu tu wa pesa ndio umekufikisha hapo huko nyuma hukuwa hivyo

Fisadi huku kwetu nanjilinji wanajuwa n lowasa ambaye yuko ukawa
 
Iwe Lowassa, iwe Magufuli... Seriously tunahitaji hizi rushwa zitokomezwe.
Tunaweza kuongea kwa ushabiki wa vyama lakini beyond vyama vyetu tunahitaji nchi yenye maendeleo.
Haiwezekani miaka yote tunateseka na matatizo yale yale tu... maji, dawa, chakula, umeme... hadi lini?
 
ccm wanamwogopa lowassa kama nn

Zile episode zako za uongo zimeishia wapi? Baada ya kutueleza uongo Dr slaa kaja kukuumbua ,

Endeleeni kupiga hela za hilo fisadi lenu ila nchi n ya Dr Magufuli
 
Mods mnahujumu posts za Lowassa. Hii ipelekwe Jukwaa la Uchaguzi Tanzania. Mmeacha kule mambo ya kipuuzi ya ushindi wa yanga dhidi ya simba afu mmehamisha mada ya msingi kama hii kuileta kwenye jukwaa ambalo halina mvuto kwa sasa ili iwe je?
 
Back
Top Bottom