Lowassa ni pasua kichwa

Lowassa ni pasua kichwa

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Leo Waziri mkuu wa zamani Mhe. Edward Lowassa alikuwa mkoani Kigoma katika mbio za urais akafanikiwa kupata zaidi ya wadhamini 11,000. Jana alipokuwa mkoani Tabora alipata wadhamini zaidi ya 13,000. Hili ni kubaliko la kutosha ndani ya jamii.
 
Ndo nani?
 

Attachments

  • 1434212469495.jpg
    1434212469495.jpg
    8.9 KB · Views: 2,996
Na kweli anawapasua kweli ila atawapasua kabisa siku mkikosa pesa ya kumrudishia
 
Huyu jamaa akipewa uraisi nakuhakikishia wahindi watatutawala zaidi ya wanavyotutawala sasa hivi..
 
Huyu ni fisadi tu, hana jipya wala hana tofauti na rafiki yake Kikwete. Ni DHAIFU mwingine huyu ambaye hastahili kupewa dhamana ya kuliongoza Taifa letu. Tumechoka kuongozwa na wasio na sifa ambao wanaifanya Ikulu yetu ni danguro la mafisadi na wapokea rushwa.
 
Leo Waziri mkuu wa zamani Mhe. Edward Lowassa alikuwa mkoani Kigoma katika mbio za urais akafanikiwa kupata zaidi ya wadhamini 11,000. Jana alipokuwa mkoani Tabora alipata wadhamini zaidi ya 13,000. Hili ni kubaliko la kutosha ndani ya jamii.

vigezo vya mangula #11 . Wadhamini 11,000 kigoma..
 
Leo Waziri mkuu wa zamani Mhe. Edward Lowassa alikuwa mkoani Kigoma katika mbio za urais akafanikiwa kupata zaidi ya wadhamini 11,000. Jana alipokuwa mkoani Tabora alipata wadhamini zaidi ya 13,000. Hili ni kubaliko la kutosha ndani ya jamii.

hata Lucifer akitafuta uungwaji mkono atapata wengi kuliko Lowasa,Je huyu Ibirisi anakubalika?
 
Dear Susan "Bashe" Lema Wadhamini wanatakiwa ni 450 kutoka mikoa 15 hizo nyingine mbwembwe tu...na kama mtu unakubalika huna haja ya kuflaunt na kuplay PR Pranks..na mwisho wa siku mgombea wenu hafai na mtakatwa tu.
 
Hivi wanapofika 450 wanaotakiwa hawezi kusimamisha zoezi mpaka awasumbue hao wote? Mbona anaanza kukiuka kanuni kungali mapema hivi? Hiyo ni dalili mbaya. Ni sawa na mtu anayejua uwezo wake wa kula nyama choma ni nusu kilo lakini kwa sababu mwenyeji anampenda hivyo akiweka kilo tano mezani lazima ale zote. Ni ulafi tuu.
 
ccm walichelewa sana kumdhibiti lowasa. alianza kampeni muda mrefu sana. na huko mikoani alishatapakaza wafuasi wake wengi tu. pia alishateka wajumbe wa mkutano mkuu na NEC zamani sana. nakwa sasa anamalizia mkakati wake wa kuiweka cc mfukoni mwake kabisa...
 
Hivi wanapofika 450 wanaotakiwa hawezi kusimamisha zoezi mpaka awasumbue hao wote? Mbona anaanza kukiuka kanuni kungali mapema hivi? Hiyo ni dalili mbaya. Ni sawa na mtu anayejua uwezo wake wa kula nyama choma ni nusu kilo lakini kwa sababu mwenyeji anampenda hivyo akiweka kilo tano mezani lazima ale zote. Ni ulafi tuu.

mkuu hapo lengo lake ni kukioneshachama chake kwamba anapendwa zaidi nakukitisha kwamba kisidiriki kumkata. lowasa ni mjanja sana...
 
Leo Waziri mkuu wa zamani Mhe. Edward Lowassa alikuwa mkoani Kigoma katika mbio za urais akafanikiwa kupata zaidi ya wadhamini 11,000. Jana alipokuwa mkoani Tabora alipata wadhamini zaidi ya 13,000. Hili ni kubaliko la kutosha ndani ya jamii.

Havina uhusiano na kukubalika. Hao ni fedha tu ndo zinawanunua na si vinginevyo. Overall wanaotakiwa na CCM hawazidi 500. Hao wengine ni mbwembwe na kuwatisha wagombea wengine. Hao nao amechukua kadi zao?
 
Ni ngumu kudhibiti kwa sasa, labda mbinu yao iliyoshindwa ni kumrestisha in peace ila wameshindwa
Lowassa nomaaaaaaaaaa!!!
 
Huyu ni fisadi tu, hana jipya wala hana tofauti na rafiki yake Kikwete. Ni DHAIFU mwingine huyu ambaye hastahili kupewa dhamana ya kuliongoza Taifa letu. Tumechoka kuongozwa na wasio na sifa ambao wanaifanya Ikulu yetu ni danguro la mafisadi na wapokea rushwa.

Una hoja nzuri kweli kweli.

Punguani wahed.
 
Ni ngumu kudhibiti kwa sasa, labda mbinu yao iliyoshindwa ni kumrestisha in peace ila wameshindwa
Lowassa nomaaaaaaaaaa!!!

mkuu uwezo wa kumdhibiti wanao wakiamua.ndani ya cc lowasa hakubaliki sana ingawa ana wachache wanaomkubali kama kina jerry slaa, sophia simba, samia nk. kwa upande wa marais wastaafu kama mwinyi na mkapa kwa kiasi kikubwa anakubalika. lakini wakitaka wahakikishe jina lake lisipite cc. nje ya hapo chama kitakuwa kimeshatekwa rasmi namafisadi.
 
Back
Top Bottom