Mkuu, (full disclosure: Mimi ni mpenda mabadiliko na maendeleo). Mtu akilisoma atajua una-agenda ya U-CCM. Ila una hoja. Upinzani wanahitaji kukaa chini na kujitafakari. Walijipambanua kwa agenda ya Ufisadi. Leo wamebadilika. Kitu ambacho hata critics wa Magufuli watakubali (hata kimoyomoyo), Magufuli hana makando kando ya ufisadi. Sasa ukiangalia anadeal na yale yale ambayo upinzani wameyapigia kelele miaka nenda rudi (na wananchi wakawa-support). Leo Magufuli mnamuweka kundi lipi? Do you really think kweli kwa mwananchi masikini asiye na kitu...huu wimbo wa udikteta utamwingia?
Kwangu mimi Tanzania inahitaji Upinzani makini na strong. Lakini nina wasiwasi na upinzani unakoellekea. Ujikite kwenye hoja ambazo zina mashiko. Zinazoleta chakula mezani mwa mlalahoi. Ukiangalia hii kasi ya Magufuli waathirika wakubwa ni wale wale (usual suspects). Waliokuwa nacho. Kiukweli RAIS wanaomsupport wengi ni wale wanaoamini kwamba wizi ulikuwa umetamalaki na wanaolalamika kuhusu utendaaji wake ni wale wale waathirika wa sera za wizi kipindi cha Jakaya.
Nawashauri kaka na dada zangu upinzani. Kaeni chini mjitathimini tena. Mnahitaji kurudisha imani yenu kwa wananchi.