AshaDii
Platinum Member
- Apr 16, 2011
- 16,190
- 18,078
AshaDii
Je una amini katika dhana ya kupanga ni kuchagua? Naelewa msingi wa hoja yako, na tumefkia hatua ambayo tunahitaji a 'balancing act' kwani pamoja na ukweli kwamba sekta ya kilimo bado ndio mwajiri mkubwa wa taifa letu, lakini ajira katika non-farming sector nayo inazidi kukua ingawa haya sio matokeo ya sera za makusudi za serikali kukuza ajira, bali ni ujanja ujanja tu wa wananchi kukabiliana na nguvu za Privatization, Liberalization na Marketization.
Mbaya zaidi ni kwamba, tofauti na how wenzetu experienced na maendeleo ya sekta ya kilimo (mapinduzi ya kijani), sisi hizi non-farming activities hazina linkage ya maana na sekta ya kilimo. Sasa implication yake kisera ni nini? Je, tuongeze uhudi kwenye Elimu kuongeza poductivity ya watanzania ili waweze kujiendeleza kwenye non - farming activities? Na je, tunapoongelea Elimu katika mazingira ya kilimo, tunaongelea elimu ya jumla ambayo inaweza tumika sekta yoyote au specifically for kilimo?
I remain convinced kwamba Tanzanai tuna utafiti wa kutosha wa kilimo, tena mwingi tu unaozalishwa na vyuo na taasisi zetu za kilimo zilizopo. Kwa mfano Koffi Annan na pia Rais wa EU walikuja mapema mwaka huu kutembelea research centre yetu ya Kilimo kule Mbeya n.k na kujionea mengi. So tatizo sio ukosefu wa utafiti kuhusu Kilimo bora, bali linkage baina ya utafiti uliopo na shughuli au hali halisi huko mashambani.
Naamini ndio katika dhana ya kupanga na kupangua… Naomba nikujulishe kuwa naelewa where it is coming from na kwa nini hasa unaamini kuwa kuchagua moja ama lingine itakuwa bora zaidi. Ningekubaliana moja kwa moja na hilo iwapo kama viongozi wetu wangekuwa wanyoofu katika utendaji. Kwamba unajuwa kabisa kuwa EL (ama yeyote yule) akizungumzia 'Elimu Kwanza'; kweli kutakuwa na mabadiliko chanya for the better nchini na kwa wananchi.... vivo hivo MP akiongelea na kumaanisha upande wa 'Kilimo Kwanza'. Hio inakatisha tamaa Mchambuzi kuanza kujadili kipi bora kati ya hayo mawaili...
Najitahidi nitoe hoja sio kwa msingi wa kipi bora kati ya hayo mawili, bali nitoe kwa kipi ambacho hata kikijadiliwa ndio hasa ambacho inabidi kufanikisha ili kuweza fika malengo (malengo ambayo yameegemea maendeleo kwa kudhatiti na kuboresha maeneo husika). Kwa maneno mengine naweza Kimsingi na ki depth wa kipi bora zaidi mimi na wewe twaweza kuwa pamoja ila tutapishana padogo kwa kipi zaidi; kati ya kuboresha moja ya hayo mawili (Elimu na Kilimo) AMA kuwa lolote ni sawa na tatizo ni utendaji…
Nakubaliana na wewe na hio lack ya linkage kati ya non-farming activities na kilimo. Na ndio mana naomba nikurudishe nyuma, kuwa nimesisitiza kuwa kama moja ya hayo yakipewa uzito (in this case tuseme Kilimo kwanza); hata hilo tatizo la kutokuwa na link kati ya sekta ya kilimo na mengineyo yatajisolve automatically… Mchambuzi lets say ‘Kilimo Kwanza' ikapewa kipau mbele IPASAVO…
Kwa vyovyote ina maana kuwa mengi ambayo ni weaknesses kwa sasa yataboreshwa kama vile viwanda vya Processing vitafufuliwa, Taasisi za kujitegemea zihusuzo Kilimo zitaanzishwa na kuboreshwa, Watafiti/wajuvi/wadau wa Kilimo watasimamiwa na kupewa support vilivo na mengine mengi. Can you imagine namna gani change inaweza tokea iwapo pale manifesto ya Kilimo kwanza ikawa implemented vilivo from start to the full stop inavoweza leta change katika kila Nyanja? Iwe Elimu, iwe uchumi, iwe ajira, iwe soko la ndani na la dunia… (Haya maelezo ni applicable kama pia Elimu ikasimamiwa vile ambavo kweli inatakiwa isimamiwe… Sio kama ilivo saizi ambapo inakuwa more out of obligation zaidi ya Malengo ya kuoboresha).
Umeuliza kuwa; tunapoongelea Elimu katika mazingira ya kilimo, tunaongelea elimu ya jumla ambayo inaweza tumika sekta yoyote au specifically for kilimo? Kwa hapo naomba niwe wazi kwa kusema nililenga kuzungumzia kuwa Elimu ya kilimo itapewa kipaumbele kuliko ilivo sasa.
Hio paragraph yako ya mwisho, kaka nakubaliana na kila ulilo zungumza hapo. Kwamba nimetoa impression kuwa kuna ukosefu wa utafiti kuhusu Kilimo bora? Hapo basi sijajieleza vema sababu siamini hilo. Naomba niongezee kuwa NAAMINI kuwa Tanzania tuna karibu kila kitu kwa sasa on paper kinachohusiana na sector nyingi, ikijumuisha matatizo, namna ya kuboresha, namna ya kunufaika n.k. Narudi pale pale kuwa haijalishi kipi kinaanza, what matters ni utendaji wa hao viongozi katika kile ambacho wataamua kusimamia na kuhakiki kinafanikiwa kwa kuweka kabisa timeframe ya malengo yao.