Lowassa mpango wa Mungu binadamu hawezi kupinga

Lowassa mpango wa Mungu binadamu hawezi kupinga

ALU255

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
2,089
Reaction score
2,125
Wana ukawa tusikate tamaa mungu habishani na mwanadam.KIPANDE CHA UNABII HIKI HAPA 'Kisha nikaona upepo uliotokea kanda ya ziwa ukipata alama nyingi za kukubalika siku ya kwanza ya uchambuzi wa alama kiasi kwamba ilisikika kila kona upepo huu utatawala miti ile.

Ghafla siku ya pili ya uchambuzi wa alama za kukubalika, upepo unaotokea mlima Meru ukapata alama zaidi na kuishangaza miti mingi, japo nguvu yake kubwa iliongezeka kutoka kwa miti mingi ya visiwani. Miti hii ya visiwani iliokoa na kuongeza zaidi alama za upepo uvumao kutoka Mlima Meru.

Kisha nikaona malaika akiandika alama katika ubao na hesabu yake ilikuwa mikono kumi na mmoja na nyongeza ya nukta kadhaa.

Naliona utata ukitokea katika kuwekwa wazi kwa alama hizo lakini baada ya msuguano Mungu aliingilia kati, kisha nikaona miti ikishangilia sana kwa sababu ya upepo utokao mlima Meru.

Haikuwa rahisi alama hizi, mikono kumi na mmoja na nyongeza ya nukta kadhaa kuwekwa wazi lakini Mungu aliingilia kati na nikaona ubaoni andiko hili (MITHALI 16:31).
 
Ni muhimu kujipa moyo maana hata hospitali hawajawahi kusema ugonjwa wako mkubwa utakufa ila wanasema utapona tu hali inazidi kuwa mbaya wao wanasema utapona tu
 
Ni muhimu kujipa moyo maana hata hospitali hawajawahi kusema ugonjwa wako mkubwa utakufa ila wanasema utapona tu hali inazidi kuwa mbaya wao wanasema utapona tu

kesho tutaheshimiana tu na msije mkajifanya na nyie mpo ukawa
 
Wana ukawa tusikate tamaa mungu habishani na mwanadam..KIPANDE CHA UNABII HIKI HAPA 'Kisha nikaona upepo uliotokea kanda ya ziwa ukipata alama nyingi za kukubalika siku ya kwanza ya uchambuzi wa alama kiasi kwamba ilisikika kila kona upepo huu utatawala miti ile. Ghafla siku ya pili ya uchambuzi wa alama za kukubalika, upepo unaotokea mlima Meru ukapata alama zaidi na kuishangaza miti mingi, japo nguvu yake kubwa iliongezeka kutoka kwa miti mingi ya visiwani. Miti hii ya visiwani iliokoa na kuongeza zaidi alama za upepo uvumao kutoka Mlima Meru. Kisha nikaona malaika akiandika alama katika ubao na hesabu yake ilikuwa mikono kumi na mmoja na nyongeza ya nukta kadhaa. Naliona utata ukitokea katika kuwekwa wazi kwa alama hizo lakini baada ya msuguano Mungu aliingilia kati, kisha nikaona miti ikishangilia sana kwa sababu ya upepo utokao mlima Meru. Haikuwa rahisi alama hizi, mikono kumi na mmoja na nyongeza ya nukta kadhaa kuwekwa wazi lakini Mungu aliingilia kati na nikaona ubaoni andiko hili (MITHALI 16:31).

Ninaomba unabii huu utimie kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
 
NIMEKUWA NIKIONA MAMBO HAYA: Naliona mti umemea na matawi yake kuenea bara na visiwani,kwenye shina lake ulionesha muhiri wa mwaka 1954 na kupata muhuri mpya 1977. *Mtii huu uliwapa kivuli wakuu wengi wa nchi hii kwa nyakati mbalimbali na ulitumainiwa kwakuwa ulikuwa pekee katika ardhi. Ghafla ilimea na kuibuka miti mingine mingi yenye chapa ya 1992 japo haikuwa na kivuli kwa wengi kama ule mmoja mkubwa wa kwanza. Ghafla miti mingi ya kundi la pili iliungana na kuwa na shina moja ili iwe na kivuli chakuwafanya wakuu wapate hifadhi chini yake. *Mti ule wa kwanza ulipoona hivo ukaaamua kubadili majani yake kuwa pesa na kuwapa wengi wapigao mbiu (wale wa habari) katika nchi ili wawe upande wa mtii huu na kukubali kivuli chake,wapiga mbiu hawa wengine walikubali kupokea pesa ili watoe habari za kuutetea mti wa kwanza na pia walitoa habari mbaya juu ya kundi la miti iliyoungana nakupotosha wengi watafutao kivuli.. Mti wa kwanza ulibadili magamba yake kuwa sumu na maji yake yalimwagwa katika mizizi ya miti ya kundi la pili ili ife na kunyauka. Miti iliyoungana kuona hivyo ilianza kupiga kelele kwa upepo hasa uliotoka Kaskazini mwa nchi na kudai haki ya kutoa kivuli bila kuzuiwa. Mgongano huu ulisababisha vita kali na miti hiyo,miti iliyumba na kuanza kuangukia nyumba na wengi katika nyumba kukimbia na wengine kujeruhiwa na wengine kufa. * Mwenye kuipenda nchi asome na kuelewa mafunuo haya. *Maombi yako yataisaidia nchi yetu iwe katika amani na kupata viongozi bora. Watu wa Mungu epukeni ushabiki wa kisiasa na pia msitumie nafasi zenu za uongozi wa kidini kuwanadi muwapendao,badala yake ombeni Mungu awe mwamuzi mkuu. (MATENDO YA MITUME 1:23-26 ). *Andika neno hili * Mungu tupatie viongozi uwatakao" endapo unaipenda nchi hii. APOSTLE Mtalemwa July 2015.
 
Last edited by a moderator:
Waafrika mambo mengine tunajipotezea muda kuamini vitu ambavyo havionekani wala havitusaidii
Na hivi vitu ndio vinatuongezea uoga waafrika.
 
....>>nauona ujambazi Wa kura kila upande!
.....>>majizi yameshupaza nyuso zao!
lipo jumbo moja Edo amepata kura 32,000.....
lakini bila woga wala aibu ,ilitangazwa amepata kura 6,000 tu....
@TUREJESHEHENI KURA ZA EDO 24,000......
 
....>>nauona ujambazi Wa kura kila upande!
.....>>majizi yameshupaza nyuso zao!
lipo jumbo moja Edo amepata kura 32,000.....
lakini bila woga wala aibu ,ilitangazwa amepata kura 6,000 tu....
@TUREJESHEHENI KURA ZA EDO 24,000......

hawa nec-ccm inabidi tuwapigie kelele haiwezekani watufanye wapumbavu kiasi cha kutuibia kura waziwazi
 
Waafrika mambo mengine tunajipotezea muda kuamini vitu ambavyo havionekani wala havitusaidii
Na hivi vitu ndio vinatuongezea uoga waafrika.

ni bora kuamini haya kuliko kuiamini ccm
 
Lowasa Mpango wa Mungu yupi huyo mwenye kibuyu na Usinga au?

LOWASA.jpg
 
Hata Mimi naweza andika maelezo mengi ni nikamalizia nabii Fulani ivi umnafikiri sisi wajinga mtu kwanza kujitangaza kwenye makanisa kila Kanisa anaingia na kujifanya mcha Mungu na mtatabili sana Mwaka huu tushamchinja akijitangaze kwa waganga Wa kienyeji sasa sauti ya Mungu ishaonyesha ni magufuli kazana kuwajaza funza vijana wasiojielewa
 
Hata Mimi naweza andika maelezo mengi ni nikamalizia nabii Fulani ivi umnafikiri sisi wajinga mtu kwanza kujitangaza kwenye makanisa kila Kanisa anaingia na kujifanya mcha Mungu na mtatabili sana Mwaka huu tushamchinja akijitangaze kwa waganga Wa kienyeji sasa sauti ya Mungu ishaonyesha ni magufuli kazana kuwajaza funza vijana wasiojielewa

hiyo sauti ya mungu umeisikia ikimtaja magufuli?
 
Mpango wa Mungu hauendani na ulaghai,matumizi makubwa. ya nguvu za dola,rushwa,hongo,nk
Mungu ni wa haki tu!
 
Wana ukawa tusikate tamaa mungu habishani na mwanadam.KIPANDE CHA UNABII HIKI HAPA 'Kisha nikaona upepo uliotokea kanda ya ziwa ukipata alama nyingi za kukubalika siku ya kwanza ya uchambuzi wa alama kiasi kwamba ilisikika kila kona upepo huu utatawala miti ile.

Ghafla siku ya pili ya uchambuzi wa alama za kukubalika, upepo unaotokea mlima Meru ukapata alama zaidi na kuishangaza miti mingi, japo nguvu yake kubwa iliongezeka kutoka kwa miti mingi ya visiwani. Miti hii ya visiwani iliokoa na kuongeza zaidi alama za upepo uvumao kutoka Mlima Meru.

Kisha nikaona malaika akiandika alama katika ubao na hesabu yake ilikuwa mikono kumi na mmoja na nyongeza ya nukta kadhaa.

Naliona utata ukitokea katika kuwekwa wazi kwa alama hizo lakini baada ya msuguano Mungu aliingilia kati, kisha nikaona miti ikishangilia sana kwa sababu ya upepo utokao mlima Meru.

Haikuwa rahisi alama hizi, mikono kumi na mmoja na nyongeza ya nukta kadhaa kuwekwa wazi lakini Mungu aliingilia kati na nikaona ubaoni andiko hili (MITHALI 16:31).

Hivi nyie mnamchukulia Mungu kama msela fulani hivi wa kitaa au siyo. Lowassa ni binadamu kama wengine na Mungu hana mpango wa ziada naye zaidi ya kumtumikisha kama binadamu wengine. Acheni kucheza na Mungu.
 
Hivi nyie mnamchukulia Mungu kama msela fulani hivi wa kitaa au siyo. Lowassa ni binadamu kama wengine na Mungu hana mpango wa ziada naye zaidi ya kumtumikisha kama binadamu wengine. Acheni kucheza na Mungu.
Huu mpango uliosemwa wa mungu sijui unaendeleaje sasa?
Bado uko Kwa mchakato bila shaka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom