My God, I cant believe this! Of all people
masopakyindi, hata wewe umeshuka kiasi hiki! Una copy na ku paste mawazo ya mtu kama Le Mutuz! Kweli hujafa hujaumbika. Ngoja nikutonye tu mdogo wangu, UKAWA wanacheza ngoma nzito, ona jinsi kila mwana CCM, anavyohangaika na UKAWA. UKAWA ndio habari ya mjini, hakuna mwenye habari na Makomeo aka Makufuli aka Magufuli aka Pombe...yaani you have all danced yourselves lame before the main dance.
You are all dancing to the tune played by UKAWA. UKAWA ndio wanaamua nani atangaze nia ya kuiacha CCM kwenye mataa na lini watangaze. Hii ni katika kuhakikisha CCM inamomonyoka taratibu, wakijashtuka hamna aliyebaki. Hebu subiri kampeni zianze mwishoni mwa wiki. Watakaokuwa wamebaki ni kwa mipango maalum ya UKAWA, kuongeza sintofahamu ndani ya CCM hadi watu wasiaminiane tena, kila moja akimtolea mashaka mwenzie hadi wachanganyikiwe.
masopakyindi, CCM inakufa na ving'ang'anizi kama wewe nawafananisha na kupe...ng'ombe anachinjwa kupe yupo tu, anachunwa kupe yupo yu, ngozi inaanikwa juani ndio kupe anagutuka. Mtu mwenyewe aliempakata Magufuli naye kachoka kweli kweli, anatamani amdondoshe na yeye akapumzike UKAWA. Wengine siku kama hii tumeisubiri na tulijua itafika tu, amini usiamini CCM kwishnei ikichungulia kaburi na hakuna tena namna, lazima ipigwe chini.