Lowassa kuizindua Helcopta ya Ufufuo na Uzima

Lowassa kuizindua Helcopta ya Ufufuo na Uzima

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2011
Posts
1,487
Reaction score
913
Nduguzetu

Jumapili hii ya tarehe 9-Novemba, kwenye viwanja vya wazi vya Tanganyika packers , eneo la Kawe ndani ya Jiji la Dar-es Salaam ile Helcoptel iliyotajwa sana na vyombo vya habari Itazinduliwa na Mheshimiwa Edward Lowasa aliyekuwa Waziri wetu mkuu. Helcopter Itatua katika viwanja hivi saa nane mchana kwenye eneo maalum ilipo tengewa.

Mbali na Mheshimiwa lowassa pia Maaskofu wakuu zaidi ya 40 Kutoka makanisa ya Kipentekoste nchini watahudhuria. lakini pia Maaskofu wa makanisa ya Lutheran, Englican na Catholic sambamba na masheick kutoka BAKWATA nao watahudhuria uzinduzi huu wa kihistoria.

Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima, ambao ndio wamiliki wa helcopter hii limemaliza taratibu nyingi za kusajili hadi kupata ruhusa ya Kuruka zilizochukua miezi Toka ilipo wasili nchini. Mbali na shughuli za kanisa lakini kanisa limeitoa helkopter hii ifanye shughuli za kijamii na ndio lengo mama hasa. shughuli hizi ni pamoja na Uokoaji wakati wa majanga.

helkopter hii aina ya Robinson R44 ambayo kwenye dunia ya vyombo vya angani inaitwa 'TOP-Vision' imeundwa kwa muundo wa kisasa zaidi wenye kioo kikubwa kinacho saidia abiria na rubani kutazama pande zote wawapo ndani. muundo huu unasaidia sana kwenye majanga kama mafuriko au vyombo vinavyozama majini. Chopaa hii ina uwezo wa kunyanyua mzigo unaokaribia tani moja ikiwa na maana inaweza kuwainua watu zaidi ya kumi kwa kamba.

lakini pia Chopaa hii ina uwezo wa kutua juu ya maji na kuendelea na safari zake. ni moja kati ya helcopter ambazo zinapendwa zaidi ulimwenguni kwa sasa. Robinson zimeundwa kwa mtindo wa kuinua pangaboi lake JUU sana kuepusha ajali. Chopaa hili halina makelele mengi wala Vumbi. watu wengi kwenye ulimwengu wa sasa huitumia kwenye sherehe na harusi mbalimbali. viongozi wengi wa siasa huzitumia kwenye kampeni.

baadhi ya watu wanahoji gharama za mafuta, Robinson inatumia kimiminika cha +petrol inayoitwa AV-Gas ambayo kwa lita ni Tsh3,200 tu. kutoka hapa hadi dodoma na kurudi unaweza kutumia mafuta ya 540,000 tu sawa na gari dogo. Robinson R44 inakimbia hadi kilometa 300 kwa saa. ina maana ni dakika 32 kutoka Dar hadi Morogoro.

uzinduzi wa Chopaa hii ni mwangaza mzuri kwa Watanzania. ni chachu kwa kila mmoja apendaye maendeleo kununua mashine zinazoleta faida sana kwa jamii. sisi sote tunakumbuka Ndugu zetu wengi wamemezwa na maji kwa kukosa nyenzo za kuwaokolea. tatizo la helikopter nyingi ni ukosefu wa marubani mahiri "Compitent pilot" Toka kanisa limeweka mawazo ya kuanza Kumiliki vyombo hivi vya angani pia tumeweka nguvu nyingi Kusomesha vijana wetu wenye akili safi nje ya nchi ili wawe marubani wazuri kwenye Ulimwengu wa anga tunao ukaribia. Ni maono ya Mchungaji Kiongozi kuwa na Chuo cha urubani Tanzania ambacho maandalizi yake yameshaanza. lakini pia kanisa limeanza mchakato wa kuagiza ndege ndogo za abiria sita na nane Jet aircraft zenye uwezo wa kukimbia kwa kasi kiasi cha kilometa 1200 kwa saa, kiasi cha kutumia dakika hamsini (50 minutes) kutoka Dar hadi Kigoma.

mbali na hapo kanisa linatarajia kuleta ndege 'cessna aircraft' zenye uwezo wa kuchukua hadi abiria 32, hizi zitafanya huduma za jamii kwa ujumla. Yote haya ni kufanya miji ifikike kwa urahisi na wepesi ili nchi yetu ipige hatua za kasi kwenye maendeleo. Mtu anaweza kutumia Jet Aircraft ndani ya masaa 11 akaitembelea Mikoa Yote Tanzania.

Kanisa linakamilisha ujenzi wa Kiwanja Cha ndege eneo la Kinzudi Salasala na wakaazi wote wa jiji hili la Darisalam na mikoani wanakaribiswa kupata huduma hizi ambazo hapo awali tulikaririshwa kwamba ni za watu wenye pesa nyingi mno kitu ambacho si kweli. Ikumbukwe kanisa halitumii mashine hizi kibiashara. mara nyingi tunaamini Mungu amesababisha tukawa na vyombo hivi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi. hivyo shughuli zote za lazima kwa washirika wa kanisa na wananchi zitatolewa bure na kama gharama itakuwepo basi ni ndogo sana kama kuchangia mafuta na si vinginevyo. Ni maono ya mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima kuhakikisha kila tulicho fikiri hakiwezekani sasa kinawezekana tena si kwa gharama ambazo wengi tunaziogopa bali kwa gharama za kila mtu hasa mtanzania wa kawaida kuzimudu.
 
hiyo chopa mboba ina kazi .....mara pinda ataizinduaa sahvi mnasema lowasa
 
Vip maandalizi ya kujenga kanisa kubwa yamefikia wapi?maana haipendezi miaka nenda rudi hamna kanisa mnakaa viwanja wa serikali.Nadhani hili ka kujenga kanisa lilipaswa liwe la kwanza kabla ya ndege ya "uokozi" na "chuo cha urubani" kama unavyosema.
 
Vip maandalizi ya kujenga kanisa kubwa yamefikia wapi?maana haipendezi miaka nenda rudi hamna kanisa mnakaa viwanja wa serikali.Nadhani hili ka kujenga kanisa lilipaswa liwe la kwanza kabla ya ndege ya "uokozi" na "chuo cha urubani" kama unavyosema.

wapigaji tu hao, wamepata hela kutoka kwa haooo wasiyojitambua mpaka akanunua chopa
duh kweli wajinga hawaishi
 
Wakuu samahani.
Je,Askofu Josephat Gwajima ana mke au ....... ? Tafadhalini, naomba picha ya Gwajima na mkewe hapa Jf !
 
..samahani Wadau.... Je huyu Gwajima ndiye yule aliehusika na kisa Cha Flora Mbasha?
 
Vip maandalizi ya kujenga kanisa kubwa yamefikia wapi?maana haipendezi miaka nenda rudi hamna kanisa mnakaa viwanja wa serikali.Nadhani hili ka kujenga kanisa lilipaswa liwe la kwanza kabla ya ndege ya "uokozi" na "chuo cha urubani" kama unavyosema.
Nadhani watu wanatutafsiri tofauti, Kanisa Kubwa tunalo hapa maeneo ya Ubungo nadhani wote tunalifaham hili, Kanisa ambalo limechukua zaidi ya Skweamita 8,600 zaidi ya ekari mbili lakini Bado halitoshi ndipo Serikali imetupatia Kwa Muda hapo Kawe. Lakini pia tumeanza Ujenzi Mkubwa Mwingine ambao taarifa zake tutazitoa tupapofikia hatua tuliyo ipanga.
 
Wakuu samahani.
Je,Askofu Josephat Gwajima ana mke au ....... ? Tafadhalini, naomba picha ya Gwajima na mkewe hapa Jf !

Ndio ANAYE anaitwa Grace Gwajima, ukitembelea Facebook page ya Ufufuo Crew utamwona
 
Wazee wa misukule dah, unajua mwanzoni nilikua naamini haya makanisa mchicha kama ni kweli yana Mungu ndani yake na ilibaki kidogo niangukie huko. lakini siku nilipokuja kugundua issue ya misukule na jinsi wanavyowapata hawa misukule nilishtuka sana. na sitaki kabisa kusikia haya makanisa mchicha.
 
RC wao wamewekeza zaid katika elimu na hospitali wakiamini kua ndo maeneo yanayogusa zaidi jamii. Hawa wamewekeza zaidi kwenye helcopta na magari ya kifahari wakiamini kua ndo maeneo yanayogusa jamii. Hapa akija mgonjwa ni kuombewa mpaka anapona
 
Wazee wa misukule dah, unajua mwanzoni nilikua naamini haya makanisa mchicha kama ni kweli yana Mungu ndani yake na ilibaki kidogo niangukie huko. lakini siku nilipokuja kugundua issue ya misukule na jinsi wanavyowapata hawa misukule nilishtuka sana. na sitaki kabisa kusikia haya makanisa mchicha.

wanawapataje mkuu
 
Nadhani watu wanatutafsiri tofauti, Kanisa Kubwa tunalo hapa maeneo ya Ubungo nadhani wote tunalifaham hili, Kanisa ambalo limechukua zaidi ya Skweamita 8,600 zaidi ya ekari mbili lakini Bado halitoshi ndipo Serikali imetupatia Kwa Muda hapo Kawe. Lakini pia tumeanza Ujenzi Mkubwa Mwingine ambao taarifa zake tutazitoa tupapofikia hatua tuliyo ipanga.

Hongereni.chapeni kazi msisikilize maneno ongezeni hizo ndege ili nchi ifikike kwa urahisi.hao wanaowabeza sasa 2015 watapigana vikumbo kuikodi
 
Nadhani watu wanatutafsiri tofauti, Kanisa Kubwa tunalo hapa maeneo ya Ubungo nadhani wote tunalifaham hili, Kanisa ambalo limechukua zaidi ya Skweamita 8,600 zaidi ya ekari mbili lakini Bado halitoshi ndipo Serikali imetupatia Kwa Muda hapo Kawe. Lakini pia tumeanza Ujenzi Mkubwa Mwingine ambao taarifa zake tutazitoa tupapofikia hatua tuliyo ipanga.

Mhandisi, mimi issue yangu ni moja tu, kwa nini uzinduzi usifanywe na mmoja kati ya Maaskofu hata kama ni wastafu. Kwa nini Lowassa?

Mipango mizuri, ufunguzi unafanywa na Fisadi
 
nyie waamuni wa hyo gwajima nyie ndiyo mna mtajirisha bila nyie kujua mmefungwa macho na akili zenu
siku mtakuja kugutukaaaa na mtajiona mlikuwa mnapumbuwazwa
 
Asanteeee kwa taarifa njema, nadhani it's high time na nyie muanze kulipa mapato TRA sasa
 
Nadhani watu wanatutafsiri tofauti, Kanisa Kubwa tunalo hapa maeneo ya Ubungo nadhani wote tunalifaham hili, Kanisa ambalo limechukua zaidi ya Skweamita 8,600 zaidi ya ekari mbili lakini Bado halitoshi ndipo Serikali imetupatia Kwa Muda hapo Kawe. Lakini pia tumeanza Ujenzi Mkubwa Mwingine ambao taarifa zake tutazitoa tupapofikia hatua tuliyo ipanga.

Mmepangishwa kwa muda...na ni zaidi ya miaka mitatu, hamna kanisa linalotosha kuwajaza washarika wenye and yet mipango ya kujenga kanisa haijakamilika lakini mnakamilisha kwanza mipango ya ndege au hummer na kahirisha mipango y kujenga kanisa?priority zenu zipo wapi?hili ndilo mlitakiwa muelekeze nguvu zenu zote kulikamilishe kwanza kabla ya kuanza kuwaza miradi ya biashara ya ndege.

Ninayo heshima kubwa kwako na kwa Gwajima lakini kwenye hili mmeshindwa kuweka priority zenu panapopaswa kuwekwa, haya mengine mngeweza kuja kuyafanya baadae sana lakini hili lilipaswa lifanyike KWANZA kabla ya ufahali wa kidunia usio na faida kwa Mungu wala kwa utukufu wa Mungu bali ni kwa utukufu wa kibinadamu.

Ziwekeni priority zenu sawa na anapokosea Gwajima muwe na ujasiri wa kumwambia hapa sipo.
 
Back
Top Bottom