Lowassa kakosea, why now?


Inabidi wampe "charm offensive" mtu wanayemwita fisadi mkuu na kudai kuondoka kwake kumehamishia "choo" upande wa mahasimu wao? Bila shaka muda si mrefu tutajua uzito wa kete anayocheza Lowassa. Kama haitakuwa na manufaa kwa CHADEMA nahisi itakuwa kwake binafsi kuwazima wanaomsema ovyo ilhali "akiwazukia" ana kwa ana wanaishia kumtolea tabasamu tu huku mkulu mwenyewe akiuona "muujiza" wa kupata fursa ya kuushika mkono wa Lowassa!
 
Hii kauli ni ukweli mtupu Mkuu, na ipo mifano chungu nzima ya kudhibitisha hii kauli yako.

Hatimaye umeibuka. Mzee wenu jana alikuwa anafyonza mvinyo baridi wenzake wa ccm nyie Makamanda mnagoma kula huko mahabusu Arusha😀😀😀
 
Lowassa kakosea but why now


Waombe mods warekebisha kichwa kisomeke hivi:

Lowassa kakosea, why now

au usomeke:

Lowassa kapatia, but why now


Kila siku tuko hapa tunapiga kelele sijui Ndalichako lele lele lele, ooh NECTA sijui wamefanya nini, mikopo ya HESBL blah blah, walimu, madawati ya watoto wetu lele lele lele.... lakini mbona watoto wetu wakija hapa kutusoma wataona kama wazazi wetu hawa nao ni kama hawakusoma?

Lowassa kakosea but why now

What the hell is that?
 

Wajinga ndio waliwao. Yeye anafyonza mvinyo baridi na wenzake wa ccm wakati kamanda Lema anakosa hata uji mahabusu na kamanda Mwalimu anabeba mtondoo huko Maswa😀😀😀
 
Hakukosea, Wale walialikwa Kimkakati, Unafikiri aliyetuma Mwaliko kwa Lowassa, Salim, Magufuli etc alifanya Hivyo kwa Bahati mbaya? Lowassa amealikwa kwa ajili ya Hatua za Mwanzo za Kutafuta Usuluhishi na Amani ya Nchi

Mbona mlisusa futari ya Waziri Mkuu? Wajinga ndio waliwao
 


Lakini nyinyi so ndiyo mnaitwa nyumbu.Mwenzenu alikuwa anaombea aipate hiyo nafasi ya kukutana na kukaa na rais,kwa Bahati kaipata Ni Kama kipofu aliyeona mwezi.kwanza hakuamini kuwa watapangiwa hata kukaa karibu. Mbatia na genge lake sasa muamke.Mambo ya kususa hata kusalimiana,oneni mwenzenu anavyowaumbua sasa.
 
Alisema wamegraduate sasa wao sijui wamesup au wanaresit paper
 
Si ni Rais wa mioyo ya wanachadema huyo or? Zungusha,zungusha,zungusha!
 
Political maturity huonyeshwa na watu wazima.
Uzuri mmoja yeye sio muongeaji ila CCM wanajua hii ni move moja hatari kwao ndiyomaana wameweka propaganda machinery ila Magufuli kawa kinyume chao baada ya kukiri jukwaani kuwa amepata baraka kushikana mkono na Lowasa.
 
ivi wanaomtesa Lema na makamanda wengine huko rumande ndio babu anaenda kuwakumbatia ?
 
you have hit the nail on the head!umegonga mulemule!
Alisema wamegraduate sasa wao sijui wamesup au wanaresit paper
ahahahaha
 
Lowasa the Don!
 

Kutoshiriki shughuli za watu wa CCM ni azimio la Chadema na Lowassa ni mjumbe wa Kamati kuu ya Chadema, Punguzeni wingi wa Matamko na Maazimio ili muwe mnayakumbuka na kuyasimamia
 
Nchi ya ajabu hii,bado sijaona chama Kinachokidhi mahitaji yangu ya kisiasa,Natamani ningekuwa South Africa (EFF)
 
sa ungemuona mbowe anavyopewa mbinu za kuwaendesha na Mkuu wake ktk idara ya usalama wa faita si ungezimia
 


Tuache uchochezi.
Taifa hili linahitaji watu wenye hekima kama Kinana , Pengo na Lowasa.
Kinana hajawahi kuwa na uadui na mtu.
Tuache fitina na majungu.
Kinana ni mwanasiasa tangu enzi za JK , Kinana alisimama kidete kupambana kutetea chama chake kwenye majukwaa ya kisiasa.
Alifikia mahali akawa anapingana na wenzake kama akina Np kwa kueneza siasa za chuki binafsi na kumshauri ajikite kwenye kujenga chama badala ya majungu na fitina.

Kinana anajua umuhimu wa siasa za majukwaani na nadhani hata yeye angependa kuona siasa na mikutano ya jadhara inafanyika . Kinana sio muoga wa kuingia kwenye ulingo wa majukwaa ya kisiasa.
Kusema eti Lowasa asisalimiane na Kinana ni kufilisika kisiasa. Kinani ni mwanasiasa bora dana ndani ya CCM ndio maana wakati wa JK alipambana kwa hoja kujenga chama chake bila kuingiza vyombo vya dola.

Hata Magufuli anapenda kuona wapinzani wake wanakaa kwa raha kwa kuheshimiana alimradi kukosoana kwa staha bila maneno ya kuudhi.
Kila chama ni lazima liwe na wazee wenye hekima na busara wanaoweza kukaa mezani na kuzungumza juu ya amani ya nchi.
Ndio maana Warioba na Salmu A. Salim walidhalilishwa sana na vijana wa CCM kwenye mchakato wa katiba mpya lakini hawakuonyesha chuki na kupaniki. Walijua ni utoto tu. Wakaendelea kushirikiana nao. Kinana ni Mzee wa siku nyingi na ametoka mbali na Lowasa. Wametofautiana kisiasa tu lakini sio maadui.
Siasa mukiijenga kwa misingi ya uadui basi hamtufai kabisa. Siasa tunataka iwe ni tofauti za namna mtakavyotuletea maendeleo na sio namna mnavyoweza kutukanana na kujenga uhasama dhidi ya watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…