monges
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 1,040
- 392
Kitu wasichojua ni kuwa ukiiba kura humuibii Lowasa bali unawaibia wale waliochagua Lowasa ambao kwa vyovyote ni mamilioni ya watu. Na mbaya zaidi na la kuogopa ni kuwa wengi wa hao mamilioni ni wale walio kata tamaa na maisha na wanaona hawana la kupoteza zaidi ya kupata iwapo fujo zitatokea. Ndivyo ilivyotokea kwa nchi nyingi.
Wanaonufaika na CCM ikiiba kura ni wale ambao wengi wako ndani ya mfumo na maisha ya purukushani hawayawezi hata kidogo, tusidanganyane kuwa watawala na familia zao wataishi kwa raha tena nchi ikichafuka. Haya maneno ya kejeli na dhihaka mnayasema tuu kwa vile hamjatembea na kujionea nchi ambazo utaratibu huo wa kuiba kura umezifikisha. Please ni wajibu wetu sote kuhakikisha kuwa uchaguzi unakwenda kwa uhuru na haki na mshindi anatangazwa aliyeshinda, hawa watawala wasitusababishie hali ya sintofahamu hata kidogo maana wao walishajiwekea mapesa nje na wanaweza kuishi huko maana hata watoto wao wako huko wanasoma na kuishi tayari.
Kwanza ya nini ugomvi? Mbona ndani ya familia zetu waweza kukuta Baba ni Ukawa na mama ni CCM? Na uchaguzi ukiisha ndoa zinaendelea? Hawa wakina Bulembo na Mwigulu wasituletee zao za kuleta maana kama uchaguzi wa haki haupo kulikuwa na sababu gani ya kuuitisha si bora hayo mabilioni yangeenda kulipa deni la MSD ili tupate dawa hospitalini, madawati kwa watoto wetu na vitanda hospitalini kwa wajawazito kuliko kujifungua kama makundi ya nguruwe zizini?
Tatizo kubwa hamlijui lakini naamini mnalijua, haiwezekani kama akili yako inafanya kazi vizuri alafu unaongea mambo ya kipuuzi namna hii, huu co muda wa kulalamika tena, ni muda wa kujikosoa, tatizo linafahamika vema kuwa tume si huru, ss unachotaka ni nn kama si ujinga huo, mm nilitegemea sana kwamba UKAWA tuna viongozi makini, kumbe ni tabu tuu, tatizo la nchi hii si Urais, lakini kwa ujinga wetu tumewekeza sana kwenye Urais, na huu Urais hauna msaada kwetu cc watu wa chini, unaposema unataabika sana na hali ngumu ya maisha, dawa yake ni serikali za mitaa/kijiji, udiwani na ubunge, cc hatuna shida na urais, kama wabunge hawatoshi kufanya maamuzi bungeni wakati huo Rais ni Lowasa hayo mabadiliko utayapata vipi? sheria zote mbovu zinaondoka tu endapo una wabunge wa kutosha bungeni, ni ujinga sana kuongelea Urais kuliko ubunge, unapowalaumu akina Mwigulu, kimsingi ww ndo unaonekana kichwa chako kina matatizo, na huo ndo umekuwa ugonjwa mkubwa wawapinzani kulalamika, tunayo nafasi kubwa ya kufanya haya mageuzi kwa kupitia wabunge tutakao wachagua, na kwa bahati nzuri ubunge unahojiwa mahakamani, ww unataka kitu ambacho hakihojiwi mahakamani, huo ndo tunauita umburula, haya Mwl.Nyerere aliwahi kuyasemea kwa kuwashauri wapinzani kwamba, watafute nafasi za kuwawakilisha wananchi wao bungeni hakuwa mjinga kusema hivyo- sasa UKAWA akili zao zimeishia kwenye Urais, viongozi wanaongea mpaka mishipa ya kichwa inataka kuchomoka eti Urais, hiyo nguvu ingetumika kwenye nafasi za uwakilishi tungekuwa tumepiga hatua kufikia kuomba Urais na wananchi wangekuwa wamepata hamasa ya kutosha.
Kwa upande wangu ninaye penda mabadiliko, nasikitika sana kuona viongozi tulionao ni wa namna gani, UKAWA hawawezi kushinda, na kwa bahati mbaya tumeweka kiongozi ambaye na yy anaipenda hiyo tume kama akifanikiwa kuingia ikulu, angekuwa anaichukia asinge poteza muda wake kugombea Urais.