Lowassa: Harusi yageuka matanga

Lowassa: Harusi yageuka matanga

Ndugu wana Jamvi Asalaam Aleykum or Bwana Asifiwe !! , Hatimae Mr JK azuia mafuriko ya Mr EL kwa Mkono. Hongera sana JK na Pole sana EL. Hii ndiyo SIASA na JK ni mwana Siasa Bora. Mr. EL please achana na SIASA kwani UMESHINDWA !!! Elewa Siasa ni Zaidi ya Mshiko ulio nao, na nasema tena POLE SANA. Kwa Ushauri wangu Elekeza Mshiko wako katika kusaidia Jamii hasa Vijana kiuchumi na Kielimu kwani Unamshiko Mwingi kiasi wa kukutia wazimu !! Ndugu wana Jamvi wakati wenye nguvu CCM wanaungana baada ya kumdondosha bepari wao ili kuendelea Kumnyonya Mnyonge wa Nchi hii, ni Vizuri sisi wanyonge Kuungana pamoja ili Kumkabili Mwenye nguvu huyu CCM ili asiendelee Kutunyonya !! Kwanza tujipange kupunguza wingi wa wabunge wa CCM ili kumpunguzia nguvu Bwanyenye Huyu , Hivyo basi kila mmoja wetu atumie nafasi yake kuelimisha wa TZ wenzetu hasa Vijijini waweze Kuelewa SOMO hili , na Pale tunapoona kuna wa Bunge Mahiri wa Upande wa pili ni Wajibu wetu kuwaunga mkono kwa hali na Mali. Wanyonge lazima Tuungane pamoja Kupunguza nguvu za Bwanyenye CCM !! Wasalaam.
 
Lowassa ni mwana CCM lakini inaonekana alikuwa hajatambua kuwa CCM ina wenyewe ndiyo maana alijizamisha mzimamzima bila kujua ni kitu gani kinachokwenda kumpata.
 
Sipati Picha Lowassa angekuwa ndo Mgombea Familia ya Mh.Rais ingehimili kejeli na dhihaka za hali ya juu?
 
nyie nyongeeni tu si safari ya ikulu ilishaanza...kilichomkalisha kimya dodoma ni nini kama ile kitu ilikuwa 'rough'? alafu lowassa ni nani yeye kila atakalo liwe kama alivyolipanga? hya ni maisha yanayohusisha binadamu ambao hawatabiriki..na kumbuka lolote linalomhusisha binadamu halitabiriki. Lowassa alijisahau kwamba mipango anapanga na "binadamu"ambao kubadilika ni sekunde.
Jamani Lowasa alishakatwa na hajasema kitu. Kanyamaza kama wale wengine mf. pinda, bilal na wengineo. Lakini naona watu wanamsemea kwani amewatuma? Au yeye hakutakiwa kukatwa? Mwacheni mzee apumuwe jamani.
 
Hakuna kitakachobadilika,siyo yesu kuwa atafufuka,kwa kifupi ni simanzi mwanzo mwisho.
 
This is just the beginning my friend..... This is like the sleeping volcano my friend....!!!
This is the state of something dreadful my friend...!!!
I disagree with you! Nothing will happen- Nothing! The person is too weak and timid
 
Hivi ile thread ya team lowasa special thread humu mbona ipo kimya sana vijana hawaleti mrejesho
 
Alivyo jikampenia kabla ya hata kujua ka atapeperusha chama chake, hapo ndipo hadi kesho sielewi ilikuwaje. Kwani angesubiri baada ingekuwaje?

Bungeni alikaa muda gani maana barabarani kila siku?
 
Zile kauli za patachimbika,hakatwi mtu,Lowasa ndio rais ajaye nk zimepotelea wapi? Kingunge alisema patachimbika,how and when? Hatusikii akiongea na vyombo vya habari,ukitaka kujua usaliti wa hali ni huu.

Wamemlia hela zake,wamemdanganya kuwa tutakuwa nawe kwenye shida na raha leo hii yako wapi? Suala la patachimbika waachie Dr Slaa,Mbowe,Lissu,Lipumba,Lema ama upinzani wote kwa ujumla wake.

Hawa akina Nchimbi,Simba na Kimbisa,ni lini walishawahi kulala hata lock up,ni lini alishawahi kutishiwa tu mkong'oto licha ya kupigwa marungu kama Prof Lipumba? Wamechimbwa mkwara tu mara moja,kimyaaa!!

Chama cha mapinduzi wakiwa upinzani itakuwa ni kama mbwa kibogoyo,wamekuwa wakilitumia jeshi la polisi kama jeshi la CCM,siku chama kingine kikishika dola na virungu viwageukie wao kazi itakuwa rahisi sana kuwanyamazisha maana hawajawahi hata kusikia sauti ya askari ikiwaamuru watulie.

Huu usaliti wa akina msukuma,mgeja ama wenyeviti wote wa mikoa wa CCM,kingunge,sofia simba,Nchimbi nk tujifunze kitu. Huu ndio usaliti wa hali ya juu kutokea,wamemlia hela zake,matokeo yake wamemkimbia na wamekaa kimya,njaa mbaya sana.
 
Sagacity

TISS KAZINI,hivi kwanini msiende hata kupepeleza hao raia wa kigeni wanaojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura mnahangaika na propaganda za kijinga au ndo hivyo maadili ya kazi yenu hamuyajui tena
 
Last edited by a moderator:
Soma tena tena na tena,halafu ujiulize,je ulicho-comment kinaendana na post hii? Halafu unijibu kama kinaendana or not,then nitakuja kukujibu.
TISS KAZINI,hivi kwanini msiende hata kupepeleza hao raia wa kigeni wanaojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura mnahangaika na propaganda za kijinga au ndo hivyo maadili ya kazi yenu hamuyajui tena
 
ha ha ha kumbe alikua hawajui? si huyo tu hata Rostam Mhindi sasa hatamtaka, ngoja uone ngoma itakavyoenda tuone kama sasa ataweza kutoa hela zake za maua kufuga watu, maana zile alizokua anahonga ni zile zetu walizoiba, ha ha hahha kweli mungu akiwa upande wetu hakuna atakayekua against us, thank you jesus walikudhihaki wakitembea kwenye nyumba zako wakizinajisi na pesa za wizi, hawakujui lile neno linalotuonya kuhusu vitu vitakatifu, walikimbilia kwaya washikaji wenyewe walinaowatumia hawajaiva ki hiyvo, kumbuka saga la Rostam la kanisa la kiluteri Kinondoni kwa kuisaidiwa na Mume wa Jojia, nakwambia na hiyo vodacom mrija wao kupitia Shivacom tutaona sasa kama bado watakuw wanatamba kwa hela za wizi. na bado mungu alisema atawaharibu adui zetu, na kusimama juu ya nchi, hawa mpaka wafe
 
Zile kauli za patachimbika,hakatwi mtu,Lowasa ndio rais ajaye nk zimepotelea wapi? Kingunge alisema patachimbika,how and when? Hatusikii akiongea na vyombo vya habari,ukitaka kujua usaliti wa hali ni huu.
Wamemlia hela zake,wamemdanganya kuwa tutakuwa nawe kwenye shida na raha leo hii yako wapi? Suala la patachimbika waachie Dr Slaa,Mbowe,Lissu,Lipumba,Lema ama upinzani wote kwa ujumla wake.
Hawa akina Nchimbi,Simba na Kimbisa,ni lini walishawahi kulala hata lock up,ni lini alishawahi kutishiwa tu mkong'oto licha ya kupigwa marungu kama Prof Lipumba? Wamechimbwa mkwara tu mara moja,kimyaaa!!
Chama cha mapinduzi wakiwa upinzani itakuwa ni kama mbwa kibogoyo,wamekuwa wakilitumia jeshi la polisi kama jeshi la CCM,siku chama kingine kikishika dola na virungu viwageukie wao kazi itakuwa rahisi sana kuwanyamazisha maana hawajawahi hata kusikia sauti ya askari ikiwaamuru watulie.
Huu usaliti wa akina msukuma,mgeja ama wenyeviti wote wa mikoa wa CCM,kingunge,sofia simba,Nchimbi nk tujifunze kitu. Huu ndio usaliti wa hali ya juu kutokea,wamemlia hela zake,matokeo yake wamemkimbia na wamekaa kimya,njaa mbaya sana.

Hivi kumbe jeshi la polisi liko kwaajili ya wapinzani??bora leo umesema ukweli
 
Back
Top Bottom