Lowassa: Elimu bure inawezekana Tanzania

Lowassa: Elimu bure inawezekana Tanzania

Hivi ni kweli unafikiria kwa akil zako zote na kumsemea rais wako vibaya...sikulaum ni elimu waliyokunyima ccm...na lengo la ccm tokea longtime ilikuwa ni kuandaa wajinga tz ili iwe rahis kuwaburuza...ona sasa tunabishana wenyewe ambao tunahitaji mabadiliko haya kutoka kwa rais wetu mtukufu sana Edward Ngoyai Lowassa
 
Watanzania CCM imetuzoesha na tumezoea Mambo na Vitu vidogovidogo sana.

Ndio maana leo Mtu akisema Elimu bure kuanzia Msingi hadi Chuo Kikuu au Vivuko vya Feri vyote bure tunamshangaa kwa sababu hii sio Mikato tuliozoeshwa na CCM.

Lowassa anayaweza haya kwa sababu ni Mtu anaefikilia nje ya uzio wa CCM.
Anaiona Tanzania nje ya Box linaloibana Tanzania.

Ukitaka kuiona Tanzania anayoiona Lowassa, Mimi na Wengine wapenda mabadiliko, fikiria lasilimali tulizonazo Tanzania na jinsi zinavyotumika.

Je Tanzania ilivyo sasa ndio Tanzania inavyotakiwa kua?


Ukijibu hili utaiona Tanzania ya Lowassa na UKAWA.
 
Kweli kabisa kabisa, si unaona hata hizi nenda urudi za kampeni ni mambo mapya kwa maccm. Tanzania Mpya inakuja
 
jitahidi sana hapo 10/25/2015 uamke asbh na mapema kapige kura ya ndiyo kwa Ngoyai; na pia jitahidi sana walau wewe binafsi uweze kwenda na watu angalau watatu watakao piga ndiyo kwa Ngoyai; ikiwa kila mwanamabadiliko atafanya hivyo, basi tz mpya haikwepeki ikiwa lengo ni kuiondoa kabisa chichiem ikulu; mimi binafsi nitafanya hivyo; nitahakikisha watu watatu wa ndiyo kwa EL nawapata
 
Hata kama akifikiria nje ya Sayari yetu ya Dunia nini boksi lkn haibadilishi maamuzi ya Mungu na WatanZania kwamba Raisi wa V wa JMTZ ni Dr.Pombe Magufuli!
 
Mkuu huwezi kuwa na utajiri ka wa lowasa kama hauna akili za ziada, huwezi kuwa organizer ka lowasa kama hauna upeo mkubwa. Watanzania wengi hatuna IQ za mtu kama lowasa. wengi tumeenda shule lakini uthubutu wetu wa kufanya mambo na kufiria nje ya box ni mdogo sana.
 
Kura zetu zinamsubiria yeye. Ushindi ni kwa Lowassa ili atupe maendeleo tunamwamini.

We mtoto maendeleo unajipa mwenyewe hakuna mtu atakayekupa maendeleo, hata mumeo inabidi mpambane nae.
 
Uloi nga mâché68;14060859 said:
mtu mwenye akili timamu na asiye mpumbavu wala lofa, hawezi kukubali ulaghai huu wa mtu kutaka kwenda IKULU kwa ahadi na gharama zozote! KUWENI MACHO WATANZANIA. AKILI NI KWA AJILI YA KUFIKIRI

Tatizo lako wewe ni mvivu wa kufikiri.
 
LOWASSA sio tu kuwa NI FISADI PAPA, bali pia ni muongo na mlaghai. Hiyo ppesa ya elimu ya bure mpaka chuo kikuu itatoka wapi wakati:


  1. Tunahitaji barabara mpya kibao
  2. Tunahitaji kuboresha elimu ya msingi kuanzia majengo hadi waalimu
  3. Tunataka kupanua elimu ya vyuo
  4. Tunahitaji kuboresha matibabu n.k, n.k.

Hiyo pesa ya bure chuo itatoka wapi wakati tunataka kupanua elimu ya chuo??

Anachotaka FISADI JENEZA LINALOTEMBEA EDWARD LOWASSA ni kuwalaghai wananchi halafu akishaingia aiibie nchi na kuwalipa marafiki zake wanaomdai.

Mama yako baado ni accountant wa Lowassa?
 
Hivi hawa wagombea wa vyama vya siasa wanalifikiriaje suala hili la Elimu?

Elimu bure itatolewa vipi?
Walimu watalipwaje?

Wanadai kukuza uchumi haliyakuwa wanafunzi wanaosomea degree za uchumi hawapewi kipaombele??

Wanadai kukuza sayansi na teknolojia ya nchi haliyakuwa wahitimu wa fani hizo hawana ajira kutokana na kazi nyingi kupewa watu wa nje??
 
Njaa zinawasumbua hamna cha elimu bure, ukiwa wanataka kupiga madili tu
 
We have Mt Kilimanjaro, Mt Meru, Serengeti, Selou, Tarangire, Manyara, Mahale, gombe, Udzungwa, Mikumi, Tanzanite, Uranium, gas, diamond, Gold, Nickel, Iron, Coal, Copper, Gypsum, Oil, Rufiji, Ruvu, Malagarasi, Beaches from north to south along indian ocean ... Hizi Assets CCM hawajui! ... Elimu Bure inawezekana hadi kuwalipa mishahara majobless inawezekana pia ..
 
RockSpider,

..wa-Tz tumezoea umasikini.

..tumezoea kushindwa. sasa kila kitu tunaamini hakiwezekani.

..ccm wamesema elimu bure mpaka form 4.

..sasa inashindikana nini elimu kuwa bure mpaka chuo kikuu?

..zile nchi zinazotoa elimu bure chekechea mpaka chuo kikuu zimeweza vipi?
 
RockSpider,

..wa-Tz tumezoea umasikini.

..tumezoea kushindwa. sasa kila kitu tunaamini hakiwezekani.

..ccm wamesema elimu bure mpaka form 4.

..sasa inashindikana nini elimu kuwa bure mpaka chuo kikuu?

..zile nchi zinazotoa elimu bure chekechea mpaka chuo kikuu zimeweza vipi?

Elimu bure inawezekana ni suala la priority tu,lakini tatizo letu sio gharama za elimu bali elimu isiyo bora.Wanafunzi wanaingia sekondari hawajui kusoma ,tuna graduate wengi wamejaa mtaani wanasubiri ajira hewa mtaani.
 
Elimu bure inawezekana ni suala la priority tu,lakini tatizo letu sio gharama za elimu bali elimu isiyo bora.Wanafunzi wanaingia sekondari hawajui kusoma ,tuna graduate wengi wamejaa mtaani wanasubiri ajira hewa mtaani.

..sasa hebu fikiria tunalipia elimu halafu haina viwango!!

..yaani hilo haliwafikirishi hawa ccm, na hawaoni hata aibu kwamba wananchi wanalipia elimu isiyo na viwango.

..tunahitaji elimu bora kwa kila mwananchi, bure toka chekechea mpaka chuo kikuu.
 
Back
Top Bottom