The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,950
- 12,549
LOWASSA sio tu kuwa NI FISADI PAPA, bali pia ni muongo na mlaghai. Hiyo ppesa ya elimu ya bure mpaka chuo kikuu itatoka wapi wakati:
- Tunahitaji barabara mpya kibao
- Tunahitaji kuboresha elimu ya msingi kuanzia majengo hadi waalimu
- Tunataka kupanua elimu ya vyuo
- Tunahitaji kuboresha matibabu n.k, n.k.
Hiyo pesa ya bure chuo itatoka wapi wakati tunataka kupanua elimu ya chuo??
Anachotaka FISADI JENEZA LINALOTEMBEA EDWARD LOWASSA ni kuwalaghai wananchi halafu akishaingia aiibie nchi na kuwalipa marafiki zake wanaomdai.
Wewe ndiye tatizo, huelewi na pengine hufikiri vizuri.
Hiyo projections zote zinalenga kuongea mapato na makusanyo ili kuwezesha wanachosema CCM hakiwezekani (elimu bure chekechea - university) kiwe funded, kiwezekane.
Inaposemwa "ELIMU" as priority number one, two and three, maana yake ni mfumo mzima wa elimu kwa maana ya kufanya "overhauling" ya system nzima ya utoaji wa maarifa na ujuzi, miundo mbinu ya shule na vyuo vyetu (maabara, nyumba za walimu, madarasa, vifaa vya kufundishia na kujifunzia nk) na maslahi ya watumishi wa sekta hii.
By any means, hiyo haina maana ya kuathiri bajeti ya barabara, afya na sekta zingine kwa sababu zipo, zina bajeti yake na hata sasa ipo.
Halafu ni lazima tuelewe kuwa unapomwondolea mwananchi zile direct expenses anazolipa ktk eneo hili la elimu km ada na michango mingine na asipolipa hapokelewi shuleni, maana yake unampa nafasi mzazi wa mwanafunzi huyu kushiriki ktk uchangiaji wa maendeleo ya shule yake kwa namna nyingine pasipo na kinyongo, mfano ujenzi wa nyumba za walimu, madarasa, maabara nk sometimes inapohitajika.
Hapa hats wazazi wenyewe wataelewa ns hawatakuwa na kinyongo chochote kushiriki ktk maendeleo yao kwa namna hii.
Hii ni tofauti na sasa, haiko sawa na sasa hivi kwa sababu licha ya wazazi kulipa ada na michango lukuki mashuleni ambapo kuna baadhi ya shule za msingi na sekondari michango inafikia hadi Tshs. 300,000 kwa mwaka na wakati huohuo mzazi huyu analazimika kuchangia fedha nyingi tena kwa nguvu na lazima ujenzi wa madarasa, maabara, nyumba za walimu, chaki, tuisheni, vitabu nk!!
Ni kiasi cha kusema kwamba serikali imejitoa completely katika jukumu lake la msingi la utoaji wa huduma za msingi za kijamii kama hii ya elimu na wakati huohuo inakusanya na kubuni kila aina ya ushuru na kodi za kumkamua mwananchi huyu!!
Nitakupa mfano mzuri tena ndani ya serikali ya CCM hiihii wakati wa ujenzi wa shule za sekondari za Kara ambapo mpango huu ulipamba moto sana wakati EL akiwa PM na ukazima Mara baada ya yeye kuondoka serikalini mwaka 2008
Kwa sehemu kubwa shule hizi zilijengwa na wananchi wenyewe. Na sera ya CCM ktk hili ilikuwa nzuri tu na ilisimamiwa vyema na PM wa wakati huo Edward Lowassa kwamba wananchi wanyanyue majengo (maboma ya majengo) kwa nguvu zao kisha serikali inaanzia hapo hadi kukamilisha jengo lote. Ndiyo maana shule hizi zipo leo.
Si hivyo wananchi walitoa maeneo yao bure ili shule hizi zijengwe bila ya shuruti wala nini.
Mara baada ya Lowassa kuondoka na mpango wote ulisimama na sera hii kukosa mwelekeo. Tembelea leo ktk shule hizi zote za mjini na vijijini utakuta majengo aliyoyaacha Lowassa mwaka 2008, mpaka leo yako vilevile na mengine yameporomoka na badala yake serikali ikaja na kitu kingine kabisa eti KILIMO KWANZA anbacho na wenyewe sijui umekwamia wapi maana hauekezwi changamoto na mafanikio yake!!
Leo ukiwaambia watu wachangie shughuli yoyote ya maendeleo, wote utawafunga kwa sababu hawatakuelewa kwa vyovyote vile!!
Mfano hai ni huh wa mwishoni mwa mwaka jana ambapo Rais Jakaya Kikwete alikuja na agizo tu tena lililojaa vitisho kwa watumishi wa umma (DCs, RCs, DEDs na wengine) pamoja na wananchi linalohitaji mabilioni ya fedha out of budget la ujenzi wa maabara ktk shule za sekondari za kata zote Tanzania, ambalo lili fail kwa zaidi ya 75% na pale lilipofanikiwa, basi ni kwa kuacha majeraha na chuki kubwa kwa wananchi dhidi ya CCM na serikali yake!