Ciril
JF-Expert Member
- Jan 10, 2011
- 8,558
- 7,156
Kwa wale mliotaka kujua kama Lowassa akiwa Rais atakuja kukemea rushwa, Mzee huyu amewasikieni, hapa ni maelezo yake kuhusu Rushwa kwenye chaguzi za CCM kama alivyonukuliwa leo Jumanne na Gazeti la Mwananchi.
"Ninaendelea na matibabu mazuri katika jicho langu moja ambalo nilifanyiwa upasuaji miaka miwili iliyopita hapahapa, (Ujerumani), ninatarajia kurejea nyumbani wakati wowote kuanzia sasa kuungana na Watanzania wenzangu katika kulijenga taifa letu.".......
Haya maneno yamekuwa yakijirudia sana bila vitendo,ccm ni janga la kitaifa litatumaliza yaani wao ndio wameshikilia rungu lakini bado wanalialia na rushwa kana kwamba wala rushwa wamegeuka upepo hawaonekani!!!
Acheni kutupumbaza wananchi kwa ngonjera zenu za kila siku,kiongozi makini ni yule anaezungumza kupitia vitendo tu..Sumaye nae wimbo ni ule ule/Jakaaya nae vivyo hivyo mmetuchosha.