Viongozi wa TZ ni wa ajabu sana!
(1)LOWASA-Alikuwa PM lkn HAKUTHUBUTU kuyasema mapungufu ya mfumo wetu wa elimu na KUYAPATIA UFUMBUZI alipokuwa madarakani!
(2)SUMAYE-Alikuwa PM na ndiye aliitumbukiza nchi kwenye rushwa ya uchaguzi alipoongoza Bunge litunge sheria ya TAKRIMA lkn sasa analia kuwa Mama Nagu alimuangusha kwa rushwa amesahau kuwa ni YY aliyeiasisi!
(3)Mzee Mangula nae juzi kasema atapambana na rushwa lkn KASAHAU kuwa ndiye yeye aliipamba kwa kutamka kuwa"mgombea kuwahudumia wapiga kura KABLA ya kupiga kupiga kura sio dhambi"lkn baadae akalalamika sana alipoangushwa kwa rushwa na Jah People kule Iringa!
INA MAANA VIONGOZI WETU WANAONA MATATIZO HADI WAKITOKA MADARAKANI?Lowassa na wenzake ni wa kupuuzwa na HAWANA JIPYA!
Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za bongo, utagundua kuwa udhaifu wa shule za kata Lowasa alianza kuuzungunzia kabla hajaondoka madarakani. Alikuja na program za dharura kukabiliana na uhaba wa waalimu na vile vile kuhiimiza vyuo vikuu kupanua intake ya wanafunzi wa ualimu. Baada ya kuondoka madarakani akaja mtoto wa mkulima na power tiller, elimu ikasahaulika. Baada ya kusema hayo, nadhani ni muhimu kwa viongozi walio nje ya serikali kutoa michango yao ili serikali ya Kikwete izinduke usingizini maana wakisema wapinzani wanaambiwa ni wachochezi na wasioona "mafanikio" ya ccm.