Nilisikia katika taarifa ya habari Lowassa akisema kuwa wamasai wasiuze ardhi yao bali watakao kuja kuwekeza wawaambie wawagawie 70% ya hisa.
Najiuliza, ina maana wananchi wa Nyamongo wadai 70% ya hisa kutoka mgodini? Wananchi wa Lindi wadai 70% ya hisa kutoka Dangote, wananchi wa Mtwara wadai 70% ya hisa kutoka Petrobras?
Je, formula hii itatumika kwa Vodacom, Airtel, na TANAPA kwenyewe tunafanyaje?
Mimi nilitegemea angeshauri kupitia NDC wananchi wanunue hisa za kiwanda cha magadi, au mkuu alimaanisha nini hasa?
Mwenye shamba akipewa 70% ya hisa wananchi wengine walioko nje ya hilo shamba inakuwaje?