Lowassa asisubiriwe anogewe na midundo, arejeshwe alipotoka!

Lowassa asisubiriwe anogewe na midundo, arejeshwe alipotoka!

Lowassa pekee hatoshi, Mbowe inabidi ajitathmini yeye kama mwenyekiti na katibu wake Mashinji. Haiwezekani eti chama kikuu cha upinzani kinapoteza wabunge na madiwani eti kwa kununuliwa na CCM, inamaana hata tukiwapa nchi mawaziri wao wanaweza kununuliwa. Inamaana wao hawana namna ya kupambana na hizo rushwa za CCM ?

Mnasusia uchaguzi, halafu baada ya hapo nini kinafuata ?
Toka jamaa alisema hajaribiwi mmeufyata kabisa, kutoa matamko na kurudi pangoni hakuonyeshi ukubwa wa tatizo mnalotaka kutuaminisha lipo kutoka utawala huu.
Kama uhuru na demokrasia ni muhimu ni lazima ipiganiwe, nyie ndio viongozi sasa tupeni hamasa ya kupigania huo Uhuru.

Kupambana na CCM ya sasa kunahitaji mtu mwenye uthubutu, labda Mbowe aliweza kupambana na awamu ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania, ila hii ya kazi tu ni mchezo mwingine kabisa !

Mkuu samahani wewe binafsi umepambanaje na CCM au wewe ni Mwanaccm?
 
CDM must discard Lowassa and possibly Sumaye, to start afresh or rejuvenate.
However, that can not be done with the current CDM leadership at helm. Mbowe must go to make the starting afresh a reality.
The onus is on CDM.
 
Amani iwe nanyi, kitendo cha lowassa kutoka hadharani na kumsifu kumpongeza mwenyekiti wa ccm kwa kazi nzuri aliofanya ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, kuua separation of power na kamata kamata ya wapinzani na kuua Uhuru wa kujieleza in cha kushangaza kwani kabla ya hapo kulikua na tetesi kwamba katumwa kuua chadema.

Kwann nasema haya, kazi kubwa ya vyama vya upinzani ni kukosoa serikali ili siku zijazo kushinda chaguzi mbalimbali. Inashangaza na kusikitisha lowassa anatoka hadharani tena bila aibu anawasifu ccm.

Wakati lowassa anayafanya hayo, mwanasheria mkuu wa chama yupo kitandani kwa maumivu ya risasi, watu wamepotea na zinaokotwa maiti zinaelea nilitegemea angemshauri mwenyekiti nn cha kufanya au angeomba aruhusiwe japo yy lowassa pekee yake kufanya siasa na mikutano ya hadhara km ccm wanavyofanya.

Hitimisho nawashauri kamati kuu ya chadema kumwita na kumuuliza alikua na nia gani? Akishindwa kujieleza ni vema akatimuliwa chadema kabla hajaiua kabisa.

Mungu ibariki Tanzania ukombozi wa kweli umekaribia.
 
ukiangalia kwa umakini i bora wakati mwingine malaika mtoa roho ISRAEL AKAFANYA YAKE !
 
Duuuu!
Kama movie vile, ila ukawa ilikuwepo na ameikuta ikiwa ngangari, hata likitokea la kutokea upinzani hautatetereka kamwe.
[HASHTAG]#MunguIbarikiTanzania[/HASHTAG]
 
As long as you speak the truth, never mind kama utaeleweka au laa, ila ukweli ndio utasimama na kuwaelewesha.

P
Ukweli upi? Unajua ataweka wapi sura yake mbele ya mamilioni ya watu waliompigia kura na inaeleweka kuwa ndio rais wa mioyo ya watu? Anaiweka familia yake kwenye historia mbaya sana anafuta heshima yote aliyokuwa nayo then akisimama atadharaulika kama Doctor Silaa siku hizi
 
Siku kadhaa zilizopita, niliandika humu JF hivi:Rais wetu tumeshamjua, twende na midundo yake!. Waliokurupuka katika kuelewa walivyotaka wakaniponda sana. Lakini, niliyaona yaliyokuwa yakitaka kutokea na yameshatokea.Leo sishauri, ila naomba. Nilishashauri:Ushauri wa mwisho kwa CHADEMA: Mfukuzeni Lowassa, Sumaye na wafuasi wao. Itumieni nafasi ya kurudi kwenye mstari wenu!

Kimsingi, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ameamua kujitokeza hadharani na kucheza midundo ya Rais Dr. John Pombe Magufuli. He appreciated and congratulated the national and fruitful deeds of our President. In fact, our President likes to be appreciated. He was sincerely moved.

Katika kumsaidia Lowassa kusema na kutenda kwa uhuru na amani, CHADEMA 'imrejeshe' CCM ili akaungane na 'wenzake' wanaoyaona mema ya Rais Magufuli.Apewe uhuru wake haraka iwezekanavyo kwakuwa alipo si mahala sahihi. Aende akashauri, akasifu na kutoa suluhisho kwa mambo mbalimbali. Asisubiriwe anogewe na midundo akiwa CHADEMA!
Aaaah, yaani arudi kwao atuachie NGO yetu , siyo? Who is yetu? Nijuavyo mimi ni Mzee Ndesamburo na mabinti zake/wake zake/wakwe zake/ kwenye Viti Maalum, na Mzee Mtei na mkwewe Freeman kwenye safu ya uongozi. Hawo ndiyo wenyewe, Lowassa kapenyeza kwa uweza wake kifedha, na Nyalandu pia, wengine vuvuzela tu. Kwa hiyo unataka Lowassa aende kwao, wewe utaenda wapi? Maana NGO ina wenyewe - mwulize Jerry.
 
Waziri Mkuu(rtd ) Bwana Edward Ngoyayi Lowassa amebaki mtupu, amejivua nguo hadharani maksudi ili kumfurahisha mfalme..!!!Kitendo cha Lowassa kwenda kumsifiia Magufuli badala ya kumkosoa kwa utawala wake wa kidikteta ni USALITI MKUBWA KWA UKAWA NA KAMBI YOTE YA UPINZANI!!!!
Baada ya CHADEMA kumpa heshima kubwa mwaka 2015 ya kugombea Urais akishiika nafasi ya 2 nyuma ya Magufuli! Lowasa alipata kura millioni 6+ huku mpinzani wake JPM akiwa na kura 8m+ pamoja na wizi wa kura uliofanywa na CCM ikishiriikiana na NEC, Wasimamizi na Jeshi la Polisi!!!!!
Lowassa angesomekaa kama angelimhoji Magufuli kwanini ameamua ku-practize UDIKTETA Tanzania kwa kuwatesa,kuwanyanyasa, kuwaapiga risasi na kuwapoteza wapinzani kwa visiingizio vya Uchochezi...!
Lowasa angeli eleweka kama angemwuliza kwaniinii waliotaka kummwua Lissu mpakaa hiyo jana hawajakamatwa......!!!
Tungelimwelewa Lowassa angelihoji kupotea kwa Watz wenzetu Ben Saanane na Azorry Gwanda na wengine wanaoendelea kuokotwa kwene viroba kama takataka......!!!!
 
Ni mapema sana na ushauri wako ni wa kihisia kupitiliza maana huna vishikizo vya kushawishi wafanya maamuzi waone unachofikiri umeona.
 
Lowassa ni dosari kubwa ndani ya Chadema anapaswa kurudi ccm kwani ndio sehemu inayomfaa. Kitendo alichokifanya ni fursa nzuri kwa chadema kumtimua.

Chadema hawatapata sababu nyingine ya kumtimua bali wanapaswa kutumia mwanya huu. Atarudi hukohuko alikotoka na uzuri wa ccm wataanza kumsafisha
Halafu CDM wataanza kumchafua tena na ile ajenda ya ufisadi itarudi.... Wanasiasa mnafurahisha sana.
 
Back
Top Bottom