Lowassa asisubiriwe anogewe na midundo, arejeshwe alipotoka!

Lowassa asisubiriwe anogewe na midundo, arejeshwe alipotoka!

Petro E. Mselewa Hawana ubavu wa kumtoa luwasa cdm, Luwasa yupo cdm ku stay, amefanya uwekezaji mkubwa na plan yake ni kugombea uraisi kwa tiketi ya cdm. Ndani ya cdm kwa sasa kuna watu wananyemelea kugombea uraisi kwa tiketi ya cdm sasa mzee ameona anaanza kusahaulika ametafuta kick kwa kutembelea ikulu na kutoa kauli tata,
 
Kiunkweli mamvi kazingua...daah nimejikia vbaya sana

Pole Mkuu asie Sikia la Mkuu huvunjika Guu

Sheikh Thabit Kombo alitushauri Tuweke Akiba ya Maneno

Zitto alitushauri tusiwaamini Wanasiasa

Jakaya akatushairi akili za kuambiwa changanya na zako

Ukizingatia misemo Hii Mitatu ukaifanyia kazi Siasa za Tanzania haziwezi kukuumiza kichwa
 
Lowassa pekee hatos hi, Mbowe inabidi ajitathmini yeye kama mwenyekiti na katibu wake. Haiwezekani eti chama kikuu cha upinzani kinapoteza wabunge na madiwani eti kwa kununuliwa na CCM, inamaana hata tukiwapa nchi mawaziri wao wanaweza kununuliwa. Inamaana wao hawana namna ya kupambana na hizo rushwa za CCM ?
Mnasusia uchaguzi, halafu baada ya hapo nini kinafuata ?
Toka jamaa alisema hajaribiwi mmeufyata kabisa, kutoa matamko na kurudi pangoni hakuonyeshi ukubwa wa tatizo mnalotaka kutuaminisha lipo kutoka utawala huu.
Kama uhuru na demokrasia ni muhimu ni lazima ipiganiwe, nyie ndio viongozi sasa tupeni hamasa ya kupigania huo Uhuru.
Huwezi kupambana na mtoza ushuru wewe!! at the end lazima utaumia tu.
 
Mnamrudishaje wakati nasikia ccm wanalalamika hamkuwalipa mabilioni yao ya ada ya uhamisho wa mda"loan" wa Lowasa...

Mjiandae kulipa na faini juu.
 
Huwezi kupambana na mtoza ushuru wewe!! at the end lazima utaumia tu.
Kwa maana hiyo hakuna umuhimu wowote wa kuwa na vyama vya upinzani
Vifutwe, wote tuunge mkono juhudi za Chama chetu Cha Mapinduzi, maana wanamaliza ruzuku kushiriki mpambano wasioweza kushinda. Kwa nini hizo hela zisihudumie jamii baadala ya Mbowe na kundi lake ?
 
Siku kadhaa zilizopita, niliandika humu JF hivi:Rais wetu tumeshamjua, twende na midundo yake!. Waliokurupuka katika kuelewa walivyotaka wakaniponda sana. Lakini, niliyaona yaliyokuwa yakitaka kutokea na yameshatokea.Leo sishauri, ila naomba. Nilishashauri:Ushauri wa mwisho kwa CHADEMA: Mfukuzeni Lowassa, Sumaye na wafuasi wao. Itumieni nafasi ya kurudi kwenye mstari wenu!

Kimsingi, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ameamua kujitokeza hadharani na kucheza midundo ya Rais Dr. John Pombe Magufuli. He appreciated and congratulated the national and fruitful deeds of our President. In fact, our President likes to be appreciated. He was sincerely moved.

Katika kumsaidia Lowassa kusema na kutenda kwa uhuru na amani, CHADEMA 'imrejeshe' CCM ili akaungane na 'wenzake' wanaoyaona mema ya Rais Magufuli.Apewe uhuru wake haraka iwezekanavyo kwakuwa alipo si mahala sahihi. Aende akashauri, akasifu na kutoa suluhisho kwa mambo mbalimbali. Asisubiriwe anogewe na midundo akiwa CHADEMA!
Picha tamu sana hii
IMG-20180110-WA0008.jpg
 
mbona umeandika mawazo yangu niliyotaka kuandika humu?Naunga mkono hoja afukuzwe haraka kabla ya kuchafua ama kweli "kinyesi walikitoa chooni na kukiweka sebuleni"Nukuu za Dr. Slaaa
 
Wote tunafahamu kuwa kilichowapeleka Chadema mzee Lowassa na Juma Duni Haji ni kupata fursa ya kugombea nafasi za juu za uongozi wa nchi na wala siyo itikadi ya chama. Sasa kama Lowassa hana mpango wa kugombea urais tena atabaki Chadema kufanya nini? Ndio maana kwa kutumia ukongwe wake wa kisiasa ameamua kuwaandaa kisaikolojia wanachadema kwa kuwaonyesha kuwa anaridhika kwa 100% na uongozi wa Rais Magufuli. Wenye akili wameshaelewa kuwa Lowassa ndio anarejea nyumbani ukizingatia CCM ni chama chake na hakiwezi kwenda kinyume na yeye. Nawasilisha!
 
Lowassa ni dosari kubwa ndani ya Chadema anapaswa kurudi ccm kwani ndio sehemu inayomfaa. Kitendo alichokifanya ni fursa nzuri kwa chadema kumtimua.

Chadema hawatapata sababu nyingine ya kumtimua bali wanapaswa kutumia mwanya huu. Atarudi hukohuko alikotoka na uzuri wa ccm wataanza kumsafisha
Kwa maana hiyo hakuna umuhimu wowote wa kuwa na vyama vya upinzani
Vifutwe, wote tuunge mkono juhudi za Chama chetu Cha Mapinduzi, maana wanamaliza ruzuku kushiriki mpambano wasioweza kushinda. Kwa nini hizo hela zisihudumie jamii baadala ya Mbowe na kundi lake ?
Cha kufanya wewe ongea na mtoza ushuru aruhusu vyama vya upinzani vifanye siasa; usifikiri upo safe saana kama tutarudi kwenye chama kimoja.
 
Back
Top Bottom