Lowassa ashusha neema kwa wanaotafuta ajira

Lowassa ashusha neema kwa wanaotafuta ajira

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Du hii sasa imemaliza kila kitu..Jana jioni nilipata bahati ya kukutana na think tank ya Lowassa ambao ni wahadhiri wa vyuo vikuu maarufu hapa Tanzania, kama UDSM, Mzumbe, IFM, SUA, CBE na Tumaini.

Kikubwa kilichonifanya kuona hii kambi ni noma na hatari, ni sera mbali mbali zilizo kwenye maandalizi na jana walikuwa wanaangalia tatizo la ajira kwa ujumla.

Katika hilo Lowassa aliahidi kuwa, akiingia magogoni kila mwezi atakuwa anatoa allowance (kaela kadogo), kwa vijana ambao hawana kazi, na kwa awamu ya kwanza ataanza na waliomaliza vyuo ili waweze kupata ela japo ya kutoa photocopy na chakula ili waweze kuwa na nguvu za kufanya application na ili wawe fiti kufanya kazi katika viwanda vitakavyooanzishwa.

Kisha ataangalia utaratibu gani wa kutoa kwa wengine pia alizidi kusisitiza kuwa gesi ikitumika vizuri hakuna kisichowezekana katika hili na hiyo gesi ni neema kubwa sana kama itatumika vizuri.

Moja wa wajumbe katika kutetea hoja hii ya Lowassa, alitoa mfano wa libya enzi za Gadafi, ambapo wanafunzi waliokuwa wanamaliza vyuo walikuwa wanapata allowance za kusogeza maisha yao huku wakisubiri kupata kazi za kudumu na sio miujiza ni mafuta tu ndio iliweza kufanya haya yote, hivyo basi ni wazi katika mpango huu vijana mumeombwa kuendeleza mjadala na kuchangia mjadala na kuona ni namna gani uweze kuboreshwa kwa faida ya Taifa.

NB: Kwa hakika mimi kama kijana nasema asilimia 100% nimepokea hizi jitiada za Lowassa kwa furaha zaidi na zaidi, kwani kama kijana hili tatizo limekuwa ni janga na bomu sio tu litakalolipuka bali ambalo limeshalipuka (rejea interview ya Uhamiaji, watu 16000 kwa nafasi 70).

Ebu fikiria kijana katoka familia maskini, kamaliza chuo, ajira ni isuues, hana mahali pa kuishi hapa mjini, na kama ana mahali pa kuishi chakula ni tatizo, na kama hivyo vyote vipo basi ela ya photocopy ni issues.

Basi tunakushukuru Lowassa kwa kuona hili, sisi kama vijana hatuna la kukulipa zaidi ya kusema tuko na wewe katika harakati zako, umeonyesha wewe ni kiongozi wa namna gani, unauwezo wa kuthubutu, katika hili umethubutu kueleza vission yako yenye uamuzi mgumu sana sana, Baba tuko na wewe pamoja daima, na kamwe hatutakutupa mpaka mwisho.


 
Wewe ni mwehu, Lowassa anaanda sera zake binafsi kwani kawa mgombea binafsi ? Atatakiwa kutekeleza sera za CCM ......
 
Allowances? nadhani hata hao wahadhiri hawajui maana yake, anyway magamba mtajuana sie tunawasubiri kwenye kona tu. 2015
 
This is madness.

Lowasa huyu huyu anaefikiri suluhisho la ajira kwa vijana ni bodaboda?
Kwake yeye Vijana ni wa jinsia moja tu na wote hawana ujuzi.

Huyu si amepigwa marufuku kupiga kampeni baada ya yeye kuanza kuzunguka nchi nzima kwa kampeni zake za kugawa bodaboda kwa vijana kama suluhisho la ajira?

Huyu Lowasa akili zake kama mwenzie January Makamba.
 
Hahahahahaaa..............Serikali hii ya CCM inashindwa kutoa allowance kwa kazi za ziada za madaktari na wauguzi, leo hii iweze kutoa allowance kwa watu wasiofanya kazi?

Kweli kuna viazi nchi hii.
 
Wewe ni mwehu, Lowassa anaanda sera zake binafsi kwani kawa mgombea binafsi ? Atatakiwa kutekeleza sera za CCM ......


hahahahaha kamanda, kabla ujapewa sera na chama lazima wewe kama mwenye nia utueleze unapanga kutekeleza nini na nini na kwa namna gani......sio tu unakaa afu unapewa kajikitabu hicho cha sera then usimame majukwaani...very sorry
 
Wewe ni mwehu, Lowassa anaanda sera zake binafsi kwani kawa mgombea binafsi ? Atatakiwa kutekeleza sera za CCM ......
Ajabu, na hiyo gesi itatumikaje vizuri wakati mikataba imeshasainiwa!
 
Hahahahahaaa..............Serikali hii ya CCM inashindwa kutoa allowance kwa kazi za ziada za madaktari na wauguzi, leo hii iweze kutoa allowance kwa watu wasiofanya kazi?

Kweli kuna viazi nchi hii.

Kwa Lowassa everything is posible aisee, usicheze na jamaaa, duniani ogopa mtu anayeweza kuthubutu na kuchukua maamuzi magumu, mtu huyo ni hatari sana.
 
Allowances? nadhani hata hao wahadhiri hawajui maana yake, anyway magamba mtajuana sie tunawasubiri kwenye kona tu. 2015

Kwa msaada wako, Allowance is an amount of something, esp money or food, given or allotted usually at regular intervals
 
Wewe ni mwehu, Lowassa anaanda sera zake binafsi kwani kawa mgombea binafsi ? Atatakiwa kutekeleza sera za CCM ......
Ngoja kwanza...! Kwani inakuaje... Mgombea anapatikana ndio manifesto inaundwa au manifesto kwanza ndio mgombea? Tujuzeni wana Nambariwani eeeh.
 
Hii mada hainunuliki hii. Hiyo hela ataitoa kwenenye gesi au atatoa mfukoni mwake? Mikataba ya gesi na umeme yeye anajua anachopata kwa siku (ufisadi mtupu) sasa anataka kuja kutugawia hiyo ndio aseme amesaidia vijana? Sikubaliani na watafiti hao sijui wa vyuo gani. Badala ya kuja na sera mbadala jinsi ya kuinua uchumi wa nchi ili vijana wapate ajira anakuja na sera ya kugawa fedha ili tumpigie kura? Yeye atuambie ataboreshaje ufanisi serikalini ili wananchi wapate huduma bila rushwa na manyanyaso!
 
jamani mtu anaweza kuwa na mawazo na sera nzuri lkn tatizo ni anaingia kwa mgongo wa chama gani? je hicho chama hakina sera zake? . ..je chama kitampokea kwa mawazo hayo?mmmm...political is the deadly game
 
Kwa Lowassa everything is posible aisee, usicheze na jamaaa, duniani ogopa mtu anayeweza kuthubutu na kuchukua maamuzi magumu, mtu huyo ni hatari sana.
Anakurupuka tu.
Mwambie atulie, yeye na KJ ndo wale wale.
 
Picture1.jpg
 
Hii mada hainunuliki hii. Hiyo hela ataitoa kwenenye gesi au atatoa mfukoni mwake? Mikataba ya gesi na umeme yeye anajua anachopata kwa siku (ufisadi mtupu) sasa anataka kuja kutugawia hiyo ndio aseme amesaidia vijana? Sikubaliani na watafiti hao sijui wa vyuo gani. Badala ya kuja na sera mbadala jinsi ya kuinua uchumi wa nchi ili vijana wapate ajira anakuja na sera ya kugawa fedha ili tumpigie kura? Yeye atuambie ataboreshaje ufanisi serikalini ili wananchi wapate huduma bila rushwa na manyanyaso!

Nafkiri hapa hujaelewa hoja mkuu....hawa vijana watakuwa wanapewa allowance katika kipindi kigumu cha kutafuta ajira, which means hili swala ni katika kipindi cha mpito... at the same time uchumi utakuwa unazidi kukuwa kwa kasi, tena ukuwaji utakuwa ni wa kugusa wananchi wa hali ya chini (Economic growth will definitely reduce poverty), sio hali ya sasa ambapo economic growth ipo ila bado kuna idadi kubwa ya walalahoi.....ndio mana agenda zake kuu ni kwenye viwanda vikubwa na vidogo vidogo, elimu na kilimo.
 
Back
Top Bottom