Mzee Lowasa kama mzee wangu tuna toka njia moja nina kushauri achana na kuhama chama maana kwa hakika hutofanikiwa sana sana unajiandalia matatizo ambayo hata dkt wakukutibu hatokuwepo at that time.
kwa nini na sema hivyo nasema hivyo kwakuwa ukweli unaujuwa na mfumo wa serikali unaujuwa na kamwe serikali haiwezi kutengeneza watu wakushindana nayo sana sana nikukutengenzea zengwe zaidi ya lile la kwanza
1. Hafai
2. Hafai
3.Hafai
4 Hafai na NIMTU HATARI KTK SERIKALI
5.?
Soma vitabu vyote nasasa ni zaidi ya miaka hamsini ya uhuru wetu ni nani alie wahi kupingana na serikali akafanikiwa ukimpata nijuze nifute kauli
Nikupe mfano mdogo tu Mh Mrema yupo wapi mtu alie tikisa taifa hili kila mtu akajuwa hakuna kama mrema yupo wapi yupo wapi wapo wapi maadui wa ccm ndani ya ccm? achana na hii habari kuwa mpole Mungu akupenda utawale hili taifa na wala sio Kikwete maana hata Kikwete hakujuwa vile atakuwa rais ila ilijulikana atakuwa rais kama ilivyojulikana hutokuwa rais.
Simama na utafakari na uone maamuzi yako ni kiza kinene kwa familia yako na watu wako na ni jambo la busara kuwa mjinga nakuendelea kumuunga mkono mgombea alie pitishwa maana mwisho wa yote nilazima utahadhirika kias napata shida kama atakuwepo dkt wakukutibu madhara utakayo yapata.
Mungu anaupima utii wako ktk hili kabla ajashuka nakukwambia kwa makofi sikukuchaguwa wewe!!!!!
Napingana na wewe kwa nguvu zote.
Hii nchi ni ya demokrasia .Hizo siasa za kutishana zepitwa na wakati.
Na mpango wowote wa kumdhuru Lowasa utatibuliwa na Mungu mwenyewe. Kumbuka jinsi CCM walivyosubiri dili lao la kifo cha Lowasa kwa muda mrefu huku wakishangilia afya yake ikizorota lakini cha ajabu afya yake iliumarika kwa kasi kuelekea mchakato. Huu ni ushahidi wa kuona jinsi Mungu atakavyoiangusha CCM .
C CM ni chama kilichoumiza na kuwatesa watanzania wengi sana. Watu wamedhulumiwa sana ndani ya mfumo wa CCM . Watanzania wengi wanakilio kikuu kwa Mungu juu ya dhuluma za mfumo mbaya wa CCM.
Lowasa hana cha kupoteza ndani ya CCM kwa umri alio nao.
Hata Dr. Slaa alitishiwa maisha sana lakini mpaka leo yupo. Mrema mpaka ngozi yake imebabuka lakini yupo. Sokoine aliuawa na hakuna hatua zilizochukuliwa zaidi ya unafiki wa kumuenzi.
Loliondo watu wameporwa ardhi yao wakapewa wageni huku nyumba zao zikichomwa moto.
Bulyanhulu watu walipoteza maisha ,Mwembe chai waislam waliuawa ,Zanziba watu waliua kwa chuki za CCM,Mtwara ,Arusha n.k. Damu za watu wema za wazi zimejaa kupitia hiki chama cha kijani. Leo wanatudanganya kwamba Liwasa ni hatari kwa usalama wa nchi.
Sio kweli bali Lowasa ni hatari kwa ustawi wa CCM na dhulma zao.
Kitengo cha kuwatisha watu sasa basi. Wao nao sasa wajiandae kuishi kwa hofu. Haiwezekani nchia maakini kama hii tuendelee kutawaliwa na chama jimoja bila upinzani imara na wabunge wanaojitambua.
Lowasa atapata heshma kubwa akitoka hadharani na kujiondoa kwenye siasa za CCM.
Lowasa akiendelea kubaki CCM ni wazi kuwa atakuwa ni msaliti wa taifa hili na atakua amewasaliti watu waliosimama na kuonyesha ukiukwaji mkubwa wa kanuni uliofanywa na chama chake.
Kitengo maalum ndani ya CCM ni janga kwa taifa hili lenye mfumo wa vyama vingi. Hakuna mtu atakayeendelea kukubali Nape atumike kuchakachua kura za mamilioni ya watanzania watakaomchagua mpinzani kwa manufaa yake mwenyewe.
CCM walipaswa kumkatalia Lowasa wakati wa kuchukua form ili ajue kuwa hastahili. Walichofanya ni kutumia ubabe kumdhalilosha ili atakapotumia uhuru na demokrasia yake kwa wananchi basi watumie vitisho kumuogopesha.
Kuna uovu mkubwa uliojificha ndani ya CCM na sio kwa Lowasa kama mnavyodai. Lowasa kinachotumika ni ukanda anotoka na dini yake na sio vingine. Na wale waliotumia muda mwingi kumchafua wameaibika kwani nao wameambulia patupu.
Na bila shaka CCM mwaka huu itaaibika sana pamoja na kuanza kampeni mapema.