Lowassa alifuata nini Iringa?

Lowassa alifuata nini Iringa?

Ni ujinga kumdhibiti Lowassa namna hiyo, hata akifanya yote hayo hofu ni nini kwa CCM? Ni nani anayeweza kukataa mwaliko wa kiongozi wake wa dini?
Kama umekuwa katika malezi ya imani ya dini, ni vigumu sana kukataa mwito wa kiongozi wako wa dini, na mara nyingi huonekana ni heshima maalum.
Hebu mwacheni Lowassa aishi anavyoweza, kwani mwisho wa siku si chama chenu wenyewe ndicho kitakachoamua nani awe mgombea wenu.
Kiukweli kwa namna mnavyoendesha suala la Lowassa, CCM mnajitia aibu sana. Mnaonesha mnavyoona alivyo juu ya chama chenu, alivyo na nguvu kuliko chama chenu.
Ova
 
ameonekana kwenye vyombo mbalimbali akiwa miongoni mwa wageni kwenye JUBILEE YA MIAKA 25 YA UASKOFU WA NGALALEKUMTWA , LAKINI IKUMBUKWE KWAMBA CHAMA CHAO CHINI YA KAMATI YA MANGULA KILIWAONYA WALIOITWA WASAKA URAIS kwa NJIA ZA PANYA KUTUMIA SHUGHULI KAMA HIZI ILI KUTAFUTA KUUNGWA MKONO , SASA CHA KUSHANGAZA AMEONEKANA KWENYE SHUGHULI AMBAYO SIDHANI KAMA WABUNGE WA KIGENI WALIALIKWA ! JE ADHABU YAO IMEISHA ?
Baba akija nyumbani unaruksa kumuuliza?
 
ameonekana kwenye vyombo mbalimbali akiwa miongoni mwa wageni kwenye JUBILEE YA MIAKA 25 YA UASKOFU WA NGALALEKUMTWA , LAKINI IKUMBUKWE KWAMBA CHAMA CHAO CHINI YA KAMATI YA MANGULA KILIWAONYA WALIOITWA WASAKA URAIS kwa NJIA ZA PANYA KUTUMIA SHUGHULI KAMA HIZI ILI KUTAFUTA KUUNGWA MKONO , SASA CHA KUSHANGAZA AMEONEKANA KWENYE SHUGHULI AMBAYO SIDHANI KAMA WABUNGE WA KIGENI WALIALIKWA ! JE ADHABU YAO IMEISHA ?

Kila kukicha Lowasaa Lowasaaa! Mangula na Kinana watafanya nini ndugu? Lowassa ni kama fupa lililomshinda fisi!
 
Nilibahatika kuhudhuria sherehe za kuwasimika Askofu Lobulu wa Jumbo la Arusha Kati na Askofu Shoo pale Moshi. Arusha Lowassa alizungumza Kwa niaba ya wanasiasa na Mh. Nagu Kwa niaba ya serikali. Lowassa alipewa nafasi ile na kanisa kwa heshima ya kushiriki shughuli za kanisa la Mungu tangu ujana wake na katika maisha yake tote.

Tulipokuwa pale Moshi mjini Askofu Shoo alizungumzia kuhusu viongozi wa kisiasa ambao wanajipitishapitisha makanisani. Pamoja na hoja yake nzito, alitoa angalizo kwamba kuna viongozi Wa kisiasa ambao wamekuwa wakishiriki kazi za Mungu siku zote. Alisema kwa hili Kanisa hslina shida na viongozi hawa!

Nasisi pia tusije tukaingilia Imani za watu na kuwazuia watu wanaotaka kumtolea Mungu sadaka zao za hiari. Sioni Kama ni vyema kwa chama changu cha mapinduzi kuingilia Uhuru Wa watu wakuabudu. Ifahamike kuwa Kwa hili la sadaka Mungu anaona vyema moyo wa mtoaji, kuliko tuanavyo sisi.

Yanayohusu Imani ya Mtu Kwa Mungu wake yaachwe. Hii itatusaidia sana katika kupunguza misiguano ambao haina manufaa kwetu.
 
Taratibu mkuu , mimi unanilaumu bure mjomba
! Masuala yote haya yaliletwa na kamati ya mangula , na kuna tetesi kwamba ile adhabu imezaa adhabu nyingine , sasa mimi nahusikaje huko ?

samahani mkuu, niliteleza maana humu kutwa kucha lowassa, i hope mods watamuanzishia jukwaa yake
 
ameonekana kwenye vyombo mbalimbali akiwa miongoni mwa wageni kwenye JUBILEE YA MIAKA 25 YA UASKOFU WA NGALALEKUMTWA , LAKINI IKUMBUKWE KWAMBA CHAMA CHAO CHINI YA KAMATI YA MANGULA KILIWAONYA WALIOITWA WASAKA URAIS kwa NJIA ZA PANYA KUTUMIA SHUGHULI KAMA HIZI ILI KUTAFUTA KUUNGWA MKONO , SASA CHA KUSHANGAZA AMEONEKANA KWENYE SHUGHULI AMBAYO SIDHANI KAMA WABUNGE WA KIGENI WALIALIKWA ! JE ADHABU YAO IMEISHA ?
Kwani alisimama na kuongea! Kama hakufanya hivyo basi ni sawa. Ana uhuru wa kwenda kokote. Na hawakukatazwa kutohudhuria sherehe yoyote
 
huwa najiuliza sana, hivi lowassa anautafuta urais wa nini wakati afya yake imedhoofu kiasi hicho? Na kama urais ndio unatafutwa hivyo, basi tujiandae kwa mateso.

nani alikuambia kuwa afya yake ni dhoofu bin hali? Aliyeko madarakani wapinzani wake 2005 walisemaje kuhusu afya yake? Usimtabirie mtu kufa mungu atakuondosha wewe kwanza. Wewe mchague tu akifa tutachagua mwingine second runner! Anafaa sana huyu jamaa
 
Lowasa anafaa sana. Hatutaki raisi msanii mwaka huu, tunataka ngangari, mwenye kuthubutu, muwajibikaji, asiyekubali kushindwa. Watu wanajiuliza kwanini haachi? Jibu ni kwamba anaamini katika maono aliyonayo na kwamba haoni mtu anayeweza kutekeleza yale anayoona ni ya maslahi kwa wananchi ndio maana hakubali kukata tamaa. Hii ni roho ya shujaa, jogoo hafi kwa utititri. Mwanamme hafi kwa majungu labda mwanamke
 
Lowasa ni mtanzania, haruhusiwi kutembelea iringa? What is so special with iringa?
 
Lowasa anafaa sana. Hatutaki raisi msanii mwaka huu, tunataka ngangari, mwenye kuthubutu, muwajibikaji, asiyekubali kushindwa. Watu wanajiuliza kwanini haachi? Jibu ni kwamba anaamini katika maono aliyonayo na kwamba haoni mtu anayeweza kutekeleza yale anayoona ni ya maslahi kwa wananchi ndio maana hakubali kukata tamaa. Hii ni roho ya shujaa, jogoo hafi kwa utititri. Mwanamme hafi kwa majungu labda mwanamke

Ha! Ha! Ha! Nimeipenda sana hiyo ' JOGOO HAFI KWA UTITIRI ' Hongera sana mkuu .
 
Back
Top Bottom