Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
WanaJF
Mie nadhani E. Lowassa angechukua hatua ya haraka ya kukata mzizi wa fitina unaomuandama kwa kufanya yafuatayo:
Kwa kuwa tuhuma kubwa dhidi yake ni ufisadi wa Richmond/Dowans (nyingine hazijatajwa/hakuna) basi aombe kwa mama Rosemary Mwakitwange amwandalie mdahalo wa yeye kujieleza tuhuma zake kwa namna ya kujisafisha.
Watafutwe watu wenye kulielewa vema sakata zima la Richmond/Dowans kama vile waandishi wa habari, na watu wengine kwa ujumla wa kumuuliza maswali na kuomba ufafanuzi kuhusu role yake katika kashfa hiyo.
Najua mdajalo huo anaweza kuugharamia yeye mwenyewe kwani ni kwa faida yake kama kweli anataka kujisafisha.
Vinginevyo mtu huyu anatuvuruga tu kwa kuleta utetezi wa kijuu juu. Mwezi uliopita aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na wengi walifikiri alikuwa anataka kujieleza kwa ufasaha kuhusu tuhuma dhidi yake, kumbe alitaka kuwatisha tu... kwamba wakimwandika mambo ya uongo atawashitaki.
Sasa waandishi hawajui ukweli ni upi hasa kwa hivyo ni bora akajitokeza na kusema yote anayoyaona ya kweli na akubali kuhojiwa katika kupata ufafanuzi. Kuanzia hapo wakimuandika uongo atakuwa na haki ya kuwashitaki.
Over to you Mr EL . KAZI NI KWAKO!!!
Nawasilisha.