Lowassa akichaguliwa, atarudi CCM Oktoba!

Lowassa akichaguliwa, atarudi CCM Oktoba!

iArmaniAdamson

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2015
Posts
944
Reaction score
289
UTANGULIZI:

Kama inavyoeleweka vizuri kwa sasa, athari za maamuzi ya muda wa mwisho ya UKAWA kumteua mtu ambaye hawamfahamu vizuri, ni kwamba Lowassa ndani ya CCM alivunja kanuni akitaka achonganishe Mwenyekiti wa chama na wanachama wake kwa kutofuata itifaki za "kutangaza nia" huko CCM;

HISTORIA FUPI:
Athari za kumchagua mtu wa dharura ni kama ilivyo kwenye historia hii fupi.
Huko Malawi, Hayati Raisi Mutharika dakika za mwisho kabisa alichaguliwa kwa kipingamizi kikubwa kuwania uraisi (pamoja na kwamba alikuwa hata ajulikani na wanachama halisia) kwa tiketi ya chama cha zamani (UDF).

Baada ya uchaguzi, alipochaguliwa ilitokea akapishana mawazo na Mwenyekiti wa Chama (aliyemuomba kuwania Uraisi). Mutharika akajivua uanachama wa chama cha UDF (kilichomchagua) na kuunda chama chake kipya cha DPP akiwa ndani ya uRaisi.

UTAFITI:-

Kuna mambo makuu matatu yanachangia hili:-
1. Lowassa amechaguliwa kwa dharura sana, baada ya machungu ya kukatwa (na ni kama amenunua chama, maana mipango yote ya kujitambulisha, kutangza mali na kujisafisha yaliwekwa pembeni alipotua CHADEMA);

2. Lowassa sio mtu wa kufuata kanuni au sheria za chama, kama ilivyoonekana ndani ya CCM (kufanya kampeni kabla ya muda uliopangwa na kuendelea kufanya hivyo hata baada ya kuonywa na uongozi wa chama chake kwamba asifanye hivyo);

3. Lowassa HAJAWAHI KUVAA GWANDA na SIJAMWONA NA GWANDA hii inasema vizuri moyo wake uko wapi au hauko wapi kisiasa na sidhani atakaa chadema milele, (mkumbuke CHADEMA sio baba yake na wala sio mama yake);

SWALI:-

Lowassa akiingia Ikulu na wakapishana mawazo na Mbowe kuhusiana na uendeshaji wa chama, ukizingatia hawafahamiani vizuri kama ilivyo kwa Mbowe na Slaa etc.

JE, Lowassa (akiwa Raisi na Amri Jeshi Mkuu) na Mbowe (akiwa Kiongozi na Mkuu wake kwenye chama alichochaguliwa) wakipishana, NINI KITAMZUIA LOWASSA ) KUTOKA UKAWA/CHADEMA, ii) kujiunga na ACT, iii) kuanzisha cham chake, au iv) hata KURUDI CCM chama anachojua vizuri na kwenye club ya marafiki zake wa zaidi ya miaka 38 / chama cha mapinzudi / CCM !
 
Vizuri sana waambie makada wa CCM wampigie kura aingie kwanza IKULU
 
@ iArmaniAdamson

Hoja dhaifu sana,kwani Nyerere aliwahi kuvaa nguo za CCM?Mpe kura ili umwone katika ubora wake
 
CCM haina mpango wa kumchukua kapi. Naona mmeanza mbwembwe za kuwalaghai wana CCM baada ya kubaini kuwa Lowasa hakubaliki
 
Pole mkuu hujui hata katiba ya nchi yako inasemaje juu ya jambo kama hii na nini hufuata kwa mtenda baada ya jambo hii kutokea
 
CCM haina mpango wa kumchukua kapi. Naona mmeanza mbwembwe za kuwalaghai wana CCM baada ya kubaini kuwa Lowasa hakubaliki


Wewe ni mnafiki sana maana ulisema mtikisiko wa UKAWA ila hukuongelea kiasi cha fedha alichohongwa na CCM,Kama wewe ni msema kweli na ni mpenzi wa kutetea Watanzania ungesema ukweli wote leo hii kila kitu iko wazi kwa Mchezo uliochezwa na CCM kumhonga SLAA,najiuliza hizo bilioni 150 zinazosambazwa kwenye mitandao ya jamii kuwa CCM mmeziandaa kuwahonga UKAWA mtazirudishaje?Kwa nini msijiamini kama mlitenda mema kwa Watanzania?
Kuna kitu kikubwa kinalindwa pale ikulu ila mwaka huu Watanzania wanataka mabadiliko msiwarubuni
.
 
tulishafanya maamuzi ya kuipigia kura ukawa, hakuna porojo zozote zinazoweza kubadili kubadili huo msimamo.
 
Hapo kwa Prof. Mutharika umedanganya. Prof. Mutharika ndiyo kwanza yuko kwenye muhula wa kwanza na hajajivua uanachama. Labda kakaye Hayati Bingu Mutharika.Kasome vizuri

Mzee Tupatupa
 
Mbowe na lowassa wote wapiga dili, hapo pembeni kuna mengi nae anataka zile dili zilikuwa zinapita kushoto zimfikie, hii vita itakuwa kubwa sana, bila kusahau kuna wale mbwa mwitu wenye uchu walioizunguka chadema, wanajulikana hapa, kwa vipande 30 tu wamemshushia matusi ya nguoni babu yao aliyewakuza mpaka kujulikana,
Kweli serikali ya mchwa inaelekea kukamata ikulu
 
CCM haina mpango wa kumchukua kapi. Naona mmeanza mbwembwe za kuwalaghai wana CCM baada ya kubaini kuwa Lowasa hakubaliki

IHI MICHEZO,,,,:behindsofa:,,,,,IMESHABUMBURUKA..WATU MITAANI NI HIVI,,,😛eace:,,, KWA SANA...MMEKOSA HATA PENALT??? HAKI YA MUNGU IHI NI SIKU YA KUFA NYANI.
 
HISTORIA FUPI:
Athari za kumchagua mtu wa dharura ni kama ilivyo kwenye historia hii fupi.
Huko Malawi, Hayati Raisi Mutharika dakika za mwisho kabisa alichaguliwa kwa kipingamizi kikubwa kuwania uraisi (pamoja na kwamba alikuwa hata ajulikani na wanachama halisia) kwa tiketi ya chama cha zamani (UDF).

Baada ya uchaguzi, alipochaguliwa ilitokea akapishana mawazo na Mwenyekiti wa Chama Kenneth Kaunda (aliyemuomba kuwania Uraisi).
Mutharika ni wa Malawi na Keneth Kaunda ni wa Zambia. Ungekaa kimya wala tusingeujua ujinga wako. Sasa kila mtu amejua kuwa hata hiyo uliyoiita HISTORIA hauijui na kwamba huna sifa za kumuelimisha mtu, bali unatakiwa ukae pembeni ili uelimishwe na wanaojua mambo mbalimbali
 
sio hivyo, wataka "mabadiliko" ndio mmesimama kupata hasara. hadithi ya CCM A na CCM B.

Tumepata hasara miaka 54 kwa CCM sasa yatosha mkuu nchi siyo yao,kama waweza orodhesha mambo ya ufisadi na yaliyochukuliwa hatua na serikali ya CCM,Tunawasikia mafisadi ila serikali haitaki kuwapeleka mahakamani,tunawaza kuna nini kama serikali haihusiki?EPA hela zinarudishwa hatujui akina nani wanazirudisha,Sasa kuna hasara zaidi ya hizi ya kuwaambia watuhumiwa kwa maneno tu ingali kuna mahala pa kupeleka ili wapate adhabu stahiki.

Karibu UKAWA tutaona mabadiliko na nchi itapiga hatua zaidi kuliko sasa.
 
Mutharika ni wa Malawi na Keneth Kaunda ni wa Zambia. Ungekaa kimya wala tusingeujua ujinga wako. Sasa kila mtu amejua kuwa hata hiyo uliyoiita HISTORIA hauijui na kwamba huna sifa za kumuelimisha mtu, bali unatakiwa ukae pembeni ili uelimishwe na wanaojua mambo mbalimbali

makosa ya uchapishaji, ni Bakili Muluzi. mwanajamvi ukifuatilia body ya historia si inaeleka, kwanini umeona tatizo moja tu?

Si inaeleweka Bingu alipewa uongozi na akabadili allegiance alipokuwa Raisi ?
 
Back
Top Bottom