Lowassa akichaguliwa, atarudi CCM Oktoba!

Lowassa akichaguliwa, atarudi CCM Oktoba!

Kuna wakati najaribu kuwaza mwenyewe, hivi hawa akina Mbowe, Lema, Tundu Lissu, Mnyika, Msigwa etc wanajua anachowawazia Lowasa moyoni mwake? Maana walizunguka karibu nchi nzima wakimwita fisadi na leo hii ameingia kwao kawapa na pesa zake na wamempa nafasi ya kugombea cheo cha urais. Nahisi akipata anaweza kugeuka ghafala na kuwashughulikia hawa watu. Ukiangalia hata sasa hivi kwenye kampeni namuona angalau Mbowe lakini ameshasuka team yake ya wana CCM B (Sumaye, Mgeja na Masha) wenzake ndo anazunguka nao. Ngoja tusubiri tuone mwisho wake, lakini nahisi jamaa ana uchungu na fundo la sumu ambalo atawatemea mara baada ya uchaguzi. Na akishindwa kamwe si mtu wa kukijega chama kama alivyofanya Slaa na kitapoteza imani kwa wananchi kabisa.
 
Hawezi kurudi ccm maana serikali itavunjika na uchaguzi kuitishwa tena
 
Tulishafanya maamuz toka alivyochaguliwa kwa hiyo mbwebwe yeyote haitubadilishi maamuz yetu
 
Haina shida.
Wacha iwe hivyo tu ili mradi kashatoka CCM na CCM ishatoka madarakani.
 
Hapo kwa Prof. Mutharika umedanganya. Prof. Mutharika ndiyo kwanza yuko kwenye muhula wa kwanza na hajajivua uanachama. Labda kakaye Hayati Bingu Mutharika.Kasome vizuri

Mzee Tupatupa

Kura yangu kwa Lowasa tuu
 
Mimi nitamchagua Lowassa awe Rais. Porojo nyingine sizitilii maanani.
 
akihama chama serikali inavunjika,tunarudi kwenye general election
 
Kwa sababu nikikuuliza Lowassa kakufanya nini mpaka usimpende....huwezi nijibu..
Labda utanijibu haya...
Serikali ya Tanzania chini ya CCM imefanya nini ndani ya Tanzania in 50 years?
Je tunasonga mbele au tuna-SURVIVE tu?
Serikali inafanya mambo yale yale kwa style zile zile na ndio maana hata katika nyimbo zao wanasema" CCM ni ILE ILE"na serikali itakuwa na mambo YALE YALE.....
Mie sina haja ya ENTRUST matumaini yangu kwa mtu ambaye najua ni binadamu ambaye anaweza kuwa INFLUENCED na external forces aidha kiuchumi, kisiasa,kitamaduni na hata kimazingira...
Lowassa najua ana tuhuma nyingi sana za kweli na zisizo za kweli...
Sawa ana tuhuma...
So what?
Labda kama haujui ni kuwa Tanzania hata kama itaingia UKAWA maisha ya wananchi hayatakuwa bora OVERNIGHT na wala uchumi hautakuwa wa juu Promptly...
Haja ya MABADILIKO msingi wake ni mwanzo mpya, Fikra mpya...
Katika kupambanua , utekekezaji na usimamizi wa mambo mbalimbali kama miradi ya maendeleo..
Na tambua kuwa ninatambua kuwa hata UKAWA ikiingia madarakani watu wote hawatakuwa wasafi....
Mie kitu ninachotambua kama UKAWA ikiingia madarakani mambo tunayoyaona kwa akili ndogo tutayaona kwa AKILI NA MAONO MAKUBWA.....
Na hiyo Akili kubwa itakuwa aidha kutoka UKAWA kwenyewe au NJE ya UKAWA.....
Kwa sababu najua hata kama CCM itashindwa katika uchaguzi huu namba yao katika VYOMBO VYA MAAMUZI itakuwa kubwa kulinganisha na namba ya wapinzani kwa sasa walivyo katika uwiano wa vyombo nyeti....
Kwa hivyo CHECKS & BALANCE itakuwa ni ya hali ya juu kuliko ilivyo sasa ktk serikali ya CCM...
Mtu akizingua na yeye anazinguliwa pia.....bila kujali yuko upande gani

Ni hayo tu.
 
Hivi sasa vituko, eti Lowassa akiingia ikulu, ikulu gani unayozungumzia hapa mwanajamvi? Wale waliokuwa gizani sasa

wameanza kutoka huko na hasa baada ya Dr. Slaa kueleza ukweli mtupu.
 
kabla hamjaandika haya yoooote jaribu kupitia KATIBA uone inasemaje? Tusiwe wavivu wa kusoma na tunaandika tu maneno ya mtaani na KATIBA ya Malawi ni tofauti na yetu
 
Kuna watu mnaandika tu pengine pasipo hata kujua katiba ya nchi ipo vipi...
 
tunajua Katiba inasema nini, Lowassa ni mgombea wa DHARULA, je, ni hekima kuwa na serikali ya DHARULA maana sio huyu Mheshimiwa akikaa CHADEMA kwa miaka 5 achilia mbali miezi mitatu.

Uteuzi wa mawaziri utaleta mgawanyiko mkubwa kati ya Mwenyekiti na Amri jeshi mkuu.
 
tunajua Katiba inasema nini, Lowassa ni mgombea wa DHARULA, je, ni hekima kuwa na serikali ya DHARULA maana sio huyu Mheshimiwa akikaa CHADEMA kwa miaka 5 achilia mbali miezi mitatu.

Uteuzi wa mawaziri utaleta mgawanyiko mkubwa kati ya Mwenyekiti na Amri jeshi mkuu.

Acha kutia aibu, soma katiba ya JMT ya mwaka 1977,
 
Back
Top Bottom