VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mambo hadharani, Edward Ngoyai Lowassa hatimaye amefanikiwa kupenyeza hoja yake ya CCJ ili kukwamisha hoja ya Kujivua Gamba. Habari za uhakika kutoka ndani ya vikao vya CC vinavyofanyika hapa Dodoma zinaeleza kuwa Lowassa, akipewa nguvu na Chiligati, Kinana na Mukama, amefanikiwa kumpa kigugumizi Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Kikwete kwa kuweka mezani hoja ya CCJ ambayo wachambuzi wanadai kuwa itawatia tunduni akina Samwel Sitta na Nape Nnauye.
Kutokana na hilo, hoja/mada juu ya kujivua gamba huenda isijadiliwe. Hadi nakwenda laptopuni jana, ajenda moja tu juu ya uchumi wa CCM ndiyo iliyojadiliwa hapa Dodoma. CC kikiwa ni kikao cha juu kabisa cha maamuzi kimeshindwa kumgusa kabisa Lowassa, Chenge na wafuasi wao. Wafuasi wa Lowassa wameapa kumpigania Mkuu wao hadi mwisho na kuhakikisha kuwa hagusiki.
Nimemnukuu mtu wa karibu wa Lowassa akitamba kuwa Lowassa hataguswa kamwe. Si mwingine ila ni Ole Millya, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha. Maji yanazidi unga....Mimi ni Vuta-Nkuvute kutoka Dodoma nikiripotia JamiiForums.
Kutokana na hilo, hoja/mada juu ya kujivua gamba huenda isijadiliwe. Hadi nakwenda laptopuni jana, ajenda moja tu juu ya uchumi wa CCM ndiyo iliyojadiliwa hapa Dodoma. CC kikiwa ni kikao cha juu kabisa cha maamuzi kimeshindwa kumgusa kabisa Lowassa, Chenge na wafuasi wao. Wafuasi wa Lowassa wameapa kumpigania Mkuu wao hadi mwisho na kuhakikisha kuwa hagusiki.
Nimemnukuu mtu wa karibu wa Lowassa akitamba kuwa Lowassa hataguswa kamwe. Si mwingine ila ni Ole Millya, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha. Maji yanazidi unga....Mimi ni Vuta-Nkuvute kutoka Dodoma nikiripotia JamiiForums.