Lowassa Afunika Iringa

Lowassa Afunika Iringa

Abdul Mohammed

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2013
Posts
1,331
Reaction score
860
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa amesema amechoshwa na manyanyaso wanayoendelea kuyapata wakulima hapa nchi kwa kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na serilkali bila ya wao kupata faida yoyote.

Lowassa alisema punde atakapochaguliwa kuongaza nchi kitu kikubwa atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao kuhakikisha wakulima wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.

Lowasa ameyasema hayo leo wilayani Mufindi alipofanya mkutano wa hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, mjini Mafinga.

Lowassa alisema watu wamekuwa wakizungumza kuwa CCM ni wezi wa kura kwasababu ni wajanja sana katika kufanya michezo michafu katika chaguzi na maneno hayo si yakuyabeza wala kuyafumbia macho.

"Mimi nataka kila mtu akihifazi vizuri kichinjio chake (kadi ya kupigia kura) na siku ya kupiga kura ikifika nawaomba wanawake na wanaume wajitokeze kwenda kupiga kura ila wakina baba nawaomba mkishapiga kura fanyeni kazi ya kuzilinda kura zenu" alisema Lowassa

Katika mkutano huo, waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai alipanda jukwaani na kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini kupitia Chadema, William Mungai ambaye ni mtoto wake.

Mungai aliwahi kuwa mbunge kwa miaka 35 kupitia CCM na aliweza kuteuliwa nafasi mbalimbali za uwaziri ikiwamo Wizara ya Kilimo, Mambo ya Ndani na Wizara ya Elimu.

Mungai alisema wananchi wa jimbo hilo wanatakiwa kumchagua William Mungai kwa sababu mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo hilo hakuweza kuongoza kama alivyofanya yeye.

Source: Mpekuzi
 
Sunday, August 30, 2015

Lowassa AFUNIKA Iringa.....Maelfu Wahudhuria Mkutano wake, Awataka Wafuasi wake Wazilinde Kura Zisiibiwe

Mpekuzi blog

Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa amesema amechoshwa na manyanyaso wanayoendelea kuyapata wakulima hapa nchi kwa kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na serilkali bila ya wao kupata faida yoyote.




Aisee, kumbe Jangwani sasa ni Iringa. Hivi uongo mtaacha lini nyie UKAWA?
 
[h=1]
[/h]

11951818_395557573970180_6555662516321838281_n.jpg






"Umati huu unajitokeza katika mikutano ya UKAWA na barabarani kupunga linawapa ccm tumbo joto" Mhe. Edward Lowassa akiwa Iringa katika viwanja vya Gagilonga leo Jumapili 30/08/2015

11951894_395557247303546_6431550544954976844_n.jpg





11230909_747620412048502_3239609026534776674_n.jpg



11914023_747620538715156_5376023588550759366_n.jpg



11918949_1083874168291148_3831450274819966865_n.jpg



11903700_1083874214957810_5844171194670860905_n.jpg




11954774_1083874308291134_7430651950241375118_n.jpg
 
Mleta mada amecopy kutoka kwenye blog ya mpekuzi, hivyo han kosa lolote.
 
Ukiona mtu anashabikia ccm licha ya ugumu wa maisha uliopo ujue ni miongoni mwa wale maiti ambao kenyatta alimwambia nyerere kuwa anaongoza maiti
 
Iringa haiwezi kuwa na idadi yote ya hao watu
 
Leo naona kimya .................Tutawanyoosha mjini na vijijini?
 
Back
Top Bottom