Lowassa aenda Ujerumani kwa matibabu

Lowassa aenda Ujerumani kwa matibabu

Hivi kuna ulazima gani wa kwenda kutibiwa nje ya nchi wakati serikali yao ya Ccm wanasema wamejenga Mahospital hata wakasema wanashangaa wapinzani wakisema kuwa serikali ya CCm haijafanya kitu so its so funny to hear if Edward lowasa he's in Germany.Lol
 
KICHWA CHA HABARI KINGEKUWA LOWASSA NA SIASA NCHINI KULIKO KILIVYO.

Ni ajabu sana jinsi watu wanavyohangaika na Lowassa!!!
 
Njia mojawapo ya kumpa umaarufu mtu ni kumsemasema na kufuatilia kila anachokifanya na kukiripoti. Ukifuatilia utaona hakuna siku ambayo imepita bila kupost EL. Kwa mtazamo wangu huku ni kumpa mtu umaarufu hata kama sio post za kumsifia. Kweli EL ni maarufu ila kweli amezidi kuwa maarufu sana hapa jamvini, na sisi wenyewe ndio tunachangia hilo kwa njia moja au nyingine. Kwani tusipomuongelea kabisa itakuwaje? Anyway nawapongeza wana kampeni wa EL, mpaka sasa mmefanikiwa kutufanya tuendelee kumuandika huyu Bwana, naona itafikia wakati tutaanza kufuatilia Chai yake anaweka vijiko vingapi vya sukari....kaenda msalani mara ngapi.....haja ndogo au kubwa n.k....Hata kama ni kiongozi Afya ya mtu ni siri kati ya yeye na D.k wake na watu wake wa karibu kama akipenda kuwaambia. Yeye mwenyewe atatuambia anaumwa nini pale atapoona inafaa, na kama ni ugonjwa usiotibika...hauna siri unapofikia hatua mbaya....utajulikana tu...tumwache baba wa watu ajiuguze na sisi tuendelee na kazi nyingine......ingawa kwa wengine inawezekana kumsema EL kila siku ndio kazi yenyewe....
 
pole kwa kushindwa kuhudhuria kiako cha NANE; Mungu akusaidie upone haraka
 
Back
Top Bottom