Hili lazima tulizungumze, Edward Lowassa ni mjumbe wa kamati kuu tena asiye na hata mwaka mmoja katika wadhifa huo lakini katika mikutano ya CHADEMA inashangaza kwani;
- Huingia wa mwisho na kulakiwa na mwenyekiti, ndugu Mbowe na, Makamu wenyeviti bara na Zanzibar, Katibu Mkuu na Manaibu.
- Hupanga mambo ya kujadliliwa katika mikutano
- Ana kura ya veto, kura yake ni ya turufu ni kubwa kuliko wajumbe wa mkutano wowote wa CHADEMA.
- Anakaa Meza kuu wakati wajumbe wa 'level' yake wanakaa viti vya kawaida.
- Posho yake ya kikao ni kubwa kuliko ya Mwenyekiti.
Hii ndio tunaita CHADEMA imegeuka kichwa chini miguu juu, watu wakisema kakinunua chama majibu ya hasira na matusi hutolewa, 'leta ushahidi'. kama kuna mwenye katiba ya CHADEMA atutolee ili tuweze kujua majukumu ya mbunge wa kamati kuu. Ikumbukwe Sumaye naye 'alizawadiwa' ujumbe wa kamati kuu kwanini hakai meza kuu?. Kuna maswali machache pia ya kujiuliza;
- Je thamani ya wajumbe wakongwe CHADEMA kama Prof. Baregu, Mabere Marando ni ndogo kulinganisha na Lowassa?
- Tundu yuko wapi wakati katiba ya CHADEMA inavunjwa?
Tujadili kwa mapana na si mihemuko kamwe usitukane.