Lowassa aache uchonganishi, hakuna njaa nchini

Mnajua tatizo lipo lakini mpo bizy kupiga propaganda za kisiasa kuwa halipo. Mnadhani njaa au ugonjwa ni sawa na vyama vya siasa ambapo ukikataza mikutano basi inabidi watii la sivyo wanapigwa virungu na vitu vyenye ncha kali na wengine kupoteza maisha au kufungwa? Njaa au ugonjwa fulani kama vipo, vipo tu hata ukipiga mkwara, bila kuweka mikakati ya kuvikabili vinazidi kuenea na kuathiri watu wengi zaidi.

Sasa sitaki kujibu uchochei mwingi ulioandika hapo ila nataka kuuliza jambo moja tu.
KAMA KWELI NJAA HAKUNA, KAULI KUWA KUNA NJAA INAWEZAJE KUWATISHA WANANCHI? YAANI UMWAMBIE MTU MWENYE CHAKULA CHA KUTOSHA KABISA AU ALIYESHIBA NA MWENYE UHAKIKA WA KUSHIBA KWA MWAKA MZIMA ATI KUNA NJAA, GHAFLA NA YEYE AHISI KWELI NJAA IPO NA AINGIWE NA HOFU?

Tupige porojo huku mkiwa mnatafuta ufumbuzi. Hizo takwimu mnazoleta msije mkazikana na kuzikanusha baadaye. Mwisho wa siku tutaambiwa chakula kilichokuwepo kimeenda kwenye mashule na magereza tu.

After all, nina hakika misalaba mingi bado haijapata watu wa kuibeba, na kwa kuwa tulishaambiwa kila mtu abebe msalaba wake, hali itaendelea hivi hivi hadi misalaba yote imalizike kubebwa na wahusika.
Swali zuri mkuu. Hawezi jibu. Alafu, cheki hii picha apa. Imepigwa na mtu wa kijijini huko Rombo Mkuu. Mazao yamekauka.. Watu wanasema hakuna njaa

a620c0d0b08a94a8bcb197d29495a536.jpg
 
Kwa hivyo wewe mfano ukivunjika mguu basi sio mwili wote unaumwa kwa sababu uliovunjika.ni mguu tu?
Du tatizo mfano wako sio ndugu yangu, na leo hii hakuna soko ambalo hakuna nafaka ya mahidi, mchele maaragwe wala mtama utasemaje kuwa Tanzania kuna njaa
 
Swali zuri mkuu. Hawezi jibu. Alafu, cheki hii picha apa. Imepigwa na mtu wa kijijini huko Rombo Mkuu. Mazao yamekauka.. Watu wanasema hakuna njaa

a620c0d0b08a94a8bcb197d29495a536.jpg
Kwani hata kama mvua ingekuwepo hayo mahidi ni ya kuvunwa leo? tunachosema ni kweli kuwa kuna tishio la ukame mwaka huu lakini mazao yanayotumika hivi sasa ni mavuno ya mwaka jana mkubwa
 
Mmbea tu Eli hiyo njaa kaiona wapi mbona bei za vitu hazina tofauti yoyote yakusema kuna njaa.
Kama huko Handeni washazoea kuuza chakula chote wanacho lima kisha wanaangaika na wamekata misitu kwa kuchoma mkaa ndio kaeaida yao.
Huko Bukoba asijifanye ndio mwema kisa tetemeko kwa upande wangu namuona lofa tu alivyokua ccm alisema alikua hana mamlaka ya kuamua jambo sasa hivi anaitoa wapi hiyo mamlaka yakuomba chakula kama sio unafiki
We vitu unanunuliwa ununui kwa hela yko utajuaje kupanda
 
Sisi wananchi tunataka vitendo na sio siasa kama hakuna njaa thibitisheni na sio kulia lia na Lowassa
 
Ni kweli Hakuna njaa nchini ila katika bahazi ya Maeneo ila inchi Inauaba wa chakula lakini serikali inachakula imeifazi ni sawa na baba kuwa na pesa mfukoni alafu familiar inakufa njaa huku baba akijitapa anapesa za kutosha. Ujinga mtupu
 
Njaa ipo na sio lowassa anayezungumzia njaa peke yake mpaka viongzi wa dini tuwe wakweli na wenye huruma kwa watawaliwa
 
Mkubwa hivi njaa inawezekana kuwepo leo Tanzania wakati uku kahama Mchele kilo moja ni 1,200 mpaka 1,500. nijuavyo mimi ni kuwa ni kweli kubna ukame ambao unaweza pelekea msimu wa mwaka huu kukawepo na njaa lakini kwa sasa hakuna njaa na sehemu iliyopo njaa ni kawaida ya wakulima kuuza chakula chote na kuanza kusema kuna njaa
Mfano ni meatu na kishapu miaka yate wao ni watu wa kusaidiwa tu hiyo huwezi kusema kwa sababu ya watu wa Meatu na kishapu leo hawana chakula ukasema kuna njaa njoo kahama au nenda Rukwa, Mbeya ndio useme Tanzania kuna njaa
Acheni ujinga hivi kwa nini hamjiulizi hicho kilichouzwa chote na wakulima na kumaliza hadi akiba kilienda wapi baada ya kuuzwa, je kipo kwenye mzunguko wa chakula ndani ya nchi ama kiliuzwa nje ya nchi?
 
[Mkubwa hivi njaa inawezekana kuwepo leo Tanzania wakati uku kahama Mchele kilo moja ni 1,200 mpaka 1,500] unachokisema ni uongo mtupu bei ya mchele madukani ni 1700 hadi 2000 , mashineni Kagongwa na Kahama ni 1500 na yenyewe ni kubahatisha sana na mia 6 hadi 1950 . Njaa ipo soon ndo utakanusha au kukubali mwezi wa pili tu
 
Nani mwenye mamlaka ya kutangaza hali yoyote ya hatari katika nchi? Mfano wa wazi kabisa ni pale tulivyovamiwa na Nduli Idd Amin Dadaa,Hayati Baba wa Taifa Mwl J.K.Nyerere akiwa amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Tanzania aliutangazia umma tena ktk mkutano maalumu na vyombo vya habari juu ya uvamizi wa nchi yao kutoka kwa Idd Amin Dadaa.
Mfano wa pili na hata baada ya kutokea kifo cha baba yetu au baba wa Taifa Mwl J.K.Nyerere ni Rais wa wakati huo ndugu Benjamin William Mkapa akautangazia umma wa Watanzania kupitia vyombo vya habari juu ya msiba huo.
Nachotaka kusema kila nchi inautaratibu wake wa kutangaza majanga ya kitaifa naweza kusema labda majanga makuu yanayotokea au yanayotishia kutokea ktk nchi,kwahiyo Watanzania tuwe makini kwa hilo kwani wahenga walisema 'Miluzi mingi ilimpoteza Mbwa muelekeo' kwahiyo Watanzania kama kunatishio lolote la njaa Rais wetu ni mtu wa watu na nimpenda watu na Rais wetu yupo ndani ya jamii hii hii ya Watanzania, kama kunatishio lolote ktk nchi atautangazia umma juu ya tishio hilo kwa sababu yeye ndiye kiongozi mkuu wa Taifa hili teule.
NJAA YA MWAKA 1974 ALIITANGAZA NANI ?
 
Du tatizo mfano wako sio ndugu yangu, na leo hii hakuna soko ambalo hakuna nafaka ya mahidi, mchele maaragwe wala mtama utasemaje kuwa Tanzania kuna njaa


Hayo mahidi, mchele maaragwe (sijui ni kitu gani hiki) yanauzwa au yanatolewa bure?
 
Back
Top Bottom