Mtaalam
JF-Expert Member
- Oct 1, 2007
- 1,370
- 234
Kuna mwanamke mmoja zamani za kale - nimehadithiwa na bibi yangu. Aliishi kwa taabu kubwa sana na mume wake ambaye alikuwa mkorofi kupindukia yani mwanamke hana kizuri atakachokifanya yule mume akaridhika . akianza kumpiga tena ndiyo usiseseme . so one time majirani kwakumhurumia wakamshauri huyu mama aede kwa mganga akajaribu kumtuliza mume wake, basi akaenda kwa mganga ... akamwambia mbona dawa ndogo sana .. yule mama kusikia hivyo akafurahi, mganga akamuuliza je utaweza masharti.. akajibu nko tayari kwa lolote ilimradi niondokane na adha hii .. mganga akamwambia nahitaji sharubu moja tu la simba .. yule mama akasema sawa nitakuletea .. yule mama akawinda simba na kumpata ... kila siku akawa anampelekea yule simba chakula mwisho wakazoeana.. akawa anamsogelea siku hadi siku mpaka akaweza kumvuta sharubu bila wasi wasi maana yule simba kishamchukulia kama rafiki .. kumpelekea mganga .. akamwambia mbona simba mkali na anaogopea umeweza kutimiza haya ... unanitania nini nenda ukamtulize mume wako hapa sina dawa ya kukupa!!!!!
i liked the story...kama aliweza mtuliza simba na kuweza mtoa sharubu iweje ashindwe kumtuliza mumewe waelewane ndani ya nyumba??!!lohh!!!