Arafat
JF-Expert Member
- Nov 17, 2009
- 2,581
- 763
Kama ikiwa huyo Mzee wa Umasaaini huko Lolindo ni Mganga wa EL na kuwa kila atakaye kunywa hayo maji yake 2015 huta mwambia lolote juu ya EL, basi tumeliwa tena tuhesabu 2025.
Napata mashaka makubwa juu ya taarifa zake, napata shida kwanini wizara ya afya haitoi tamko lolote. Kwanini wizara ya afya wasipereke wataalam wao na wagonjwa ili kupata sample za wagonjwa waliopona kwa ajili ya kutoa taarifa elekezi? kwanini serikali imelala!
Niliwai kusoma kitabu cha Prof.Gabriel Ruhumbuka; Janga kuu la Wazawa, ambaye hajakisoma akitafute, ni riwaya ilitumika sana katika Vyuo vikuu mbali mbali Amerika na nadhani pia ni miongoni mwa vitabu teule Tanzania. Mambo yote yanayofanyika hapa Tanzania mengi yake Ruhumbuka alikwisha yaona katika riwaya. mtunzi anaongelea Ushirikina na madhara yake akitumia Tanzania kama jukwaa la kufikisha ujumbe, utakuta mauhaji kwa imani za kishirikina kama yale ya Albino yalikwisha andikwa na huyu mwana falsafa wa kitanzania, alikuwa UDSM 1970 hadi 1985 kabla ya kuamia USA.
Siyo kwamba napinga kuwa huyo mzee hana dawa, hapana na uliza kwanini serikali haitoi tamko elekezi kutoka wizara husika ya Afya? ilitujue watu wetu wanaomiminika huko Loliondo kupewa maji wapo salama!
Hili swala linavyotolewa maelezo si la kiimani tena, maana ukisha kuvuka kuponyesha kwa maombi ukaanza kutoa dozi iwe ya maji au vidonge tayari hiyo siyo Kuponyesha kwa imani ni kuponyesha kwa tiba asilia, kwa kweli hapo siyo imani peke yake.
Hisije ikawa kama 2005; Kama dawa inatibu lazima itaonyesha katika vipimo vya kitaalam na kama haionyeshi maana yake haitibu huo ndio ukweli. hizi dini sasa zinaweza kutupereka katika uchawi nasi tukatumbukia bila kujua, Mwaka 2005 Askofu wa Katoliki ndie aliyekuwa wa Kwanza kutangaza kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu, leo hii imedhiirika ni kazi ya Uchawi na Majini, watanzania kama tumelala hivi mbona tuta-tawaliwa hadi 2105!.
Kumbukeni ya Kibwetele na ya Makanisa yalioibuka kama uyoga na baade kushiriki biashara ya unga hasa mikoa ya Mbeya, Iringa na Dar es Salaam.
Napata mashaka makubwa juu ya taarifa zake, napata shida kwanini wizara ya afya haitoi tamko lolote. Kwanini wizara ya afya wasipereke wataalam wao na wagonjwa ili kupata sample za wagonjwa waliopona kwa ajili ya kutoa taarifa elekezi? kwanini serikali imelala!
Niliwai kusoma kitabu cha Prof.Gabriel Ruhumbuka; Janga kuu la Wazawa, ambaye hajakisoma akitafute, ni riwaya ilitumika sana katika Vyuo vikuu mbali mbali Amerika na nadhani pia ni miongoni mwa vitabu teule Tanzania. Mambo yote yanayofanyika hapa Tanzania mengi yake Ruhumbuka alikwisha yaona katika riwaya. mtunzi anaongelea Ushirikina na madhara yake akitumia Tanzania kama jukwaa la kufikisha ujumbe, utakuta mauhaji kwa imani za kishirikina kama yale ya Albino yalikwisha andikwa na huyu mwana falsafa wa kitanzania, alikuwa UDSM 1970 hadi 1985 kabla ya kuamia USA.
Siyo kwamba napinga kuwa huyo mzee hana dawa, hapana na uliza kwanini serikali haitoi tamko elekezi kutoka wizara husika ya Afya? ilitujue watu wetu wanaomiminika huko Loliondo kupewa maji wapo salama!
Hili swala linavyotolewa maelezo si la kiimani tena, maana ukisha kuvuka kuponyesha kwa maombi ukaanza kutoa dozi iwe ya maji au vidonge tayari hiyo siyo Kuponyesha kwa imani ni kuponyesha kwa tiba asilia, kwa kweli hapo siyo imani peke yake.
Hisije ikawa kama 2005; Kama dawa inatibu lazima itaonyesha katika vipimo vya kitaalam na kama haionyeshi maana yake haitibu huo ndio ukweli. hizi dini sasa zinaweza kutupereka katika uchawi nasi tukatumbukia bila kujua, Mwaka 2005 Askofu wa Katoliki ndie aliyekuwa wa Kwanza kutangaza kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu, leo hii imedhiirika ni kazi ya Uchawi na Majini, watanzania kama tumelala hivi mbona tuta-tawaliwa hadi 2105!.
Kumbukeni ya Kibwetele na ya Makanisa yalioibuka kama uyoga na baade kushiriki biashara ya unga hasa mikoa ya Mbeya, Iringa na Dar es Salaam.