Lodge na Hoteli nyingi za Dar es Salaam hazina vyandarua vya mbu

Jawai

JF-Expert Member
Nov 20, 2011
530
405
Licha ya serikali kupiga kampeni kila siku juu ya mpango wa kutokomeza malaria. Nimeshangazwa na haya mazoea ya Hotel na Lodge nyingi za Dar es Salaam kutofungwa net za mmbu kwenye vitanda vyao.

Labda, lengo za hotel/Lodge hizo ni kuhudumia wateja wa short time lakini anapokuja mgeni anayehitaji kulala anaumwa na mbu usiku kucha jambo ambalo linakuwa kero na linaweza sababisha kupata magojwa yanayosambazwa na mbu.

Sijui ni mamlaka gani zinahusika na kufanya ukaguzi na uthibiti wa hizi nyumba za kulala wageni.

Binafsi nashauri nyumba hizo zifunge net za mbu ili hiwe takwa la mteja kutumia au kutotumia.
 


Unalala Guest/lodge ya bei gani? Sijawahi lala lodge Dar es salaam yenye net, na Mbu hakuna.
 
huwa ni maalumu kwa matumizi ya mchana tu, na au kama ni usiku basi ni mapumziko ya bila usingizi wa fofofo ya masaa ma2 au ma3 mnasepa.....

umetoka mkoa gani?
 
Lodge za Dar es Salaam hazijalenga wageni toka mikoani ambao wanalala siku nzima. Zile ni za wazinzi tu au "short time", ndiyo maana hawaweki neti.

Kimsingi wanakushanga unachotaka
 
Lodge nzuri hazina Mbu hata kama hazina net.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…